Unakumbuka nini kwenye graduation(mahafali) yako?

Unakumbuka nini kwenye graduation(mahafali) yako?

Kichwa Kichafu

JF-Expert Member
Joined
Apr 13, 2017
Posts
44,855
Reaction score
189,385
Leo kwenye shughuli na mihangaiko ya kila siku nikakutana na vijana wakipiga shangwe, kelele na kila aina ya hamsha hamsha unazozijua za vijana wa sasa.

Ndipo nikamuuliza mwenyeji wa eneo hilo kulikoni? Ndipo aliposema ni watoto wa form four wana sherehe za kumaliza shule.

Hapo ndipo nikakumbuka mimi kipindi hicho. Nakumbuka nilikuwa naamini graduation kama nikunipotezea muda maana nilikuwa wa kusoma kweli( enzi hizo).

Basi ilivyofika siku ya graduation wala nilikuwa sina habari kama kuna shughuli muhimu ipo shuleni. Nikawa nafata ratiba yangu niliyojiwekea(maisha ya boarding) nikaamka asubuhi nikaenda zangu class kupiga kitabu japo nilikuwa na umakini mchana swala la chakula.

Wali kilikuwa ni chakula special sana kama mnavyokumbuka maisha ya boarding yalivyokuwa.

Sasa wakati wa sherehe sakata likafika kwenye ugawaji wa vyeti na zawadi pale ndio kukaleta mtafaruku.


Kiukweli enzi hizo nilibahatisha bahatisha kuchukua vyeti vingi vya masomo mbalimbali ukiongeza na mbwembwe za waalimu wakaongeza na cha nidhamu. (Kama mwanafunzi bora)

Wakati vyeti vinagawiwa kila wakiita mwanafunzi bora kwenye somo husika sipo.

Hili swala lilileta kama mshangao kwanini huyu mwanafunzi hajatokea wengine wakahisi labda naumwa ikabidi waanze kunitafuta.(waalimu wa zamu)

Walikuja kunipata almost shughuli imekaribia kwisha nikalazimishwa kwenda kuungana na wenzangu japo tayari ilikuwa imefika muda wa kula.

Muda wa picha hata sikutaka kwenda sababu kama walikuwa wamenikurupua nikaendelea na mambo yangu.

Nikawasalimia salimia baadhi ya wazazi wa marafiki zangu maana mimi hata home sikutaka wajue kama kuna graduation.

Kiukweli waalimu wengi walinilalamikia sana wa ushauri walitoa ushauri kipindi hicho. Nilijisikia vibaya sana maana mimi nilikuwa naona ni jambo la kawaida tofauti na wao.


Muda ulivyokwenda nikikumbuka najiona nilivyokuwa Mwehu kwa huu upuuzi niliowahi kufanya.


Wewe unakumbuka nini kwenye graduation yeyote ile katika maisha yako?
 
Nakumbuka fujo za hapa na pale zilipelekea kupigwa marufuku shughuli za mahafali shuleni pale toka 2002.

Waalimu walipigwa na wanafunzi wasiojulikana.
 
Nililetewa keki nyingi Sana. Plus kuweka private part baada ya chakula iliyo nifanya kuonekana wakishia kumbe wapi[emoji848]. Ila nilifanya kusudi kuwakomoa walio pewa ma vyeti ya masomo
 
Mkuu nawe ulikuwa miongoni mwao?
Nakumbuka fujo za hapa na pale zilipelekea kupigwa marufuku shughuli za mahafali shuleni pale toka 2002.

Waalimu walipigwa na wanafunzi wasiojulikana.
 
Nikikumbuka naumia Sana
Kwanza shule ya msingi, sikuwa na ndugu hata mmoja pale kwenye hiyo kitu
Hii ilitokea coz mchango wa hii kitu ni 5k
Na Mimi hiyo 5k sikufanikiwa kuipata
Sikuishi na Wazazi wangu mjini pale,

Kilichofanya nihudhurie hii kitu Ni uigizaji wangu

Nilikuwepo kwenye ratiba ya uigizaji

Nilinogesha igizo kwakweli.

Kwenye msosi walienda kula kwa kuponi
Mie niliambiwa na mwalimu subiri wote waishe

Kwenye kupiga picha nilidandia picha za marafiki tuu na Wazazi wao
Aisee narahisha stori ila nikikumbuka nilikosa konfidensi
Kwenye uvaaji
Kuvishwa taji kwenye cheti hakuwa mtu wa kunivisha
Nilijiona junior Sana..

Watu na makeki yao, mie nilichekacheka tuu

Wapo walikuwa wananiita nipewe nami kipande Cha keki
Kwakweli acha tuu..
Nikifika kwenye meza ya keki kwakweli wananishangaa nilivyo vululuvululu
Confidenceless

Ila Mungu fundi sana nilifaulu shule nzito
Now nasubiri graduation ya chuo ,Ni degree yangu ya Kwanza[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Congratulations mkuu.
Nikikumbuka naumia Sana
Kwanza shule ya msingi, sikuwa na ndugu hata mmoja pale kwenye hiyo kitu
Hii ilitokea coz mchango wa hii kitu ni 5k
Na Mimi hiyo 5k sikufanikiwa kuipata
Sikuishi na Wazazi wangu mjini pale,

Kilichofanya nihudhurie hii kitu Ni uigizaji wangu

Nilikuwepo kwenye ratiba ya uigizaji

Nilinogesha igizo kwakweli.

Kwenye msosi walienda kula kwa kuponi
Mie niliambiwa na mwalimu subiri wote waishe

Kwenye kupiga picha nilidandia picha za marafiki tuu na Wazazi wao
Aisee narahisha stori ila nikikumbuka nilikosa konfidensi
Kwenye uvaaji
Kuvishwa taji kwenye cheti hakuwa mtu wa kunivisha
Nilijiona junior Sana..

Watu na makeki yao, mie nilichekacheka tuu

Wapo walikuwa wananiita nipewe nami kipande Cha keki
Kwakweli acha tuu..
Nikifika kwenye meza ya keki kwakweli wananishangaa nilivyo vululuvululu
Confidenceless

Ila Mungu fundi sana nilifaulu shule nzito
Now nasubiri graduation ya chuo ,Ni degree yangu ya Kwanza[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
Back
Top Bottom