Unakuta mmama/mbaba wa nguvu tu katulia mwenyewe yupo serious kwenye simu yake kumbe anasoma udaku mtupu

Unakuta mmama/mbaba wa nguvu tu katulia mwenyewe yupo serious kwenye simu yake kumbe anasoma udaku mtupu

Braza Kede

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2012
Posts
3,840
Reaction score
6,844
Ni habari za ujinga ujinga tu.

Habari za nani anatoka na nani?

Nani kalala na nani?

Sijui tunatengeneza taifa la namna gani huko mbeleni.

Acha mwarabu achukue nchi aisee.
 
Ni aibu kwa kweli kufuatilia umbea, yapo mambo mengi muhimu kufuatiliwa ya kielimu, kwani elimu haina mwisho ila wapuuzi na wajinga wamekuwa wengi ndio hao wanaofuatilia udaku kwenye simu
 
Ni habari za ujinga ujinga tu.

Habari za nani anatoka na nani?

Nani kalala na nani?

Sijui tunatengeneza taifa la namna gani huko mbeleni.

Acha mwarabu achukue nchi aisee.
Taifa limeharibika, lina watu wanapenda umbea kuliko kujifunza, lawama zote ziende kwa CCM kwa kuharibu misingi na maadili ya taifa letu
 
KEYWORD: Simu yake.

Ikiwa anasoma kwenye simu yake, kwa bundle lake, muda wake. Tatizo liko wapi??

Nadhani tumekuwa na taifa la ovyo mno la watu kutaka kupangiana aina ya maisha ya kuishi kwa kipimo cha kile wanachoona bora kwao.

Kuna maana gani mtu kusoma mambo ya siasa ikiwa siasa yenyewe haieleweki.
 
KEYWORD: Simu yake.

Ikiwa anasoma kwenye simu yake, kwa bundle lake, muda wake. Tatizo liko wapi??
Ukikekengeuka hata kama unamiliki kila kitu, utaonywa tu. Ni kweli simu na bando ni vyake ila in the end tunatengeneza taifa bovu. Hadi leo tunapewa misaada kwa vile tumeamua kuwekeza kwenye ujinga.
 
Ni habari za ujinga ujinga tu.

Habari za nani anatoka na nani?

Nani kalala na nani?

Sijui tunatengeneza taifa la namna gani huko mbeleni.

Acha mwarabu achukue nchi aisee.
Br. Unataka sisi mapaparazi tukale wapi ? Waache wapite pite kwenye page zetu na sisi tupate mkate wetu wa kila siku.
 
Binadamu ni social animal. Kupiga soga, kushare taarifa na kutoa ni sehemu ya kusocialize.

Sasa unapokuwa hana access ya hivi vitu katika mazingira yake anamoishi ndio mtandaoni kunakuwa kimbilio lake.

Mitandaoni kuna taarifa mbali mbali sasa aina ya akili aliyonayo mtu ndio inaamua aina gani ya taarifa anatafuta.

Mfano watu wanaopenda kufuatilia Maisha ya watu utawakuta wanafuatilia umbea, watu wanapenda maswala ya kifedha utawakuta wanafuatalia taarifa za uwekezaji, watu wanaopenda mambo ya kiimani utaona wanafollow pages za mafunzo ya kiimani, na kadhalika.

So nadhani inategemea na mtu sio wote wanapenda kufuatilia udaku. Kama mimi udaku umenishinda kabisa kufuatilia sababu naona kazi sana kuamka nikiwaza leo nani litakuwa limemkuta lipi ila kuna watu akimka asubuhi kitu cha kwanza anakwenda kwenye page ya mtu fulani anayepost sana matukio ya watu ili akaone kuna jipya lipi asubuhi ya leo.
 
Mwisho wa siku kila mtu ana needs na wants; hizo needs ni Chakula; Mavazi na Malazi..., Sasa hizo wants ni tofauti kwa kila mtu..., yaani mtu anafanya shughuli ili apate ujira na kukidhi mahitaji na matamanio...; Sasa kwenye Matanio huwezi kumpangia mtu (to each their own)..., Hata kama mtu anapenda tu harufu ya noti yaani azitafute ili azichome na kunusa Moshi (binafsi nasema good for him / her) Sio vema kupangia watu maisha...

LAKINI kama unayesema ni mwajiriwa / mtumishi na anatumia muda wa waliomuajiri kufanya kile ambacho halipwi (hata kama anasome Bible au ku-solve Quantum economics) hapo atakuwa anakosea...

To each their own.... (Ingawa binafsi sipendi wapenda umbea sio sababu ya matumizi ya muda wao bali sababu ya kufuatilia maisha ya watu...., it goes beyond my motto - To each their Own)
 
Back
Top Bottom