Unamfahamu Idris Sultan kwa Uigizaji, Uchekeshaji au kama Mtangazaji?

Unamfahamu Idris Sultan kwa Uigizaji, Uchekeshaji au kama Mtangazaji?

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
1721062548168.png

Mfahamu Idris Sultan

Amezaliwa Januari 28, 1993 jijini Arusha. Anafahamika kama mwigizaji, Mchekeshaji na mtangazaji wa vipindi vya radio

Safari yake ya mafanikio ilianza baada ya kushinda shindano la "Big Brother" mwaka 2014 na kuzawadiwa zaidi ya milioni Tshs. 514 akiwa na umri wa miaka 22.

Idris Sultan amekuwa Mtanzania wa kwanza kuigiza Netflix katika filamu ya ‘Slay’ mwaka 2021. Na baadaye mwaka 2023 alipata fursa ya kushiriki kwenye filamu nyingine iitwayo ‘Married to Work’ iliyoongozwa na muongozaji mahiri Philippe Bresson

Amewahi kushinda tuzo mbali kama vile:
Mtangazaji wa Vyombo vya Habari Mwenye Mavazi Bora Afrika - 2016

Tuzo za Mitindo na Mavazi za Abryanz - Mwanamume Mwenye Mitindo/Mavazi Bora (Afrika) - 2017
 
Vichekesho hachekeshi analazimishia......kuigiza sijamuona ..ila anavaa vzr na good personality
 
Idris sio mchekeshaji ni Content Creator ila title ya uchekeshaji aliaanza kujipa baada ya umaarufu wa Big brother baada ya hapo hakufanya uchekeshaji ila amesimama sana kama Content creator tu kiujumla.
 
Kuchekesha sio mchezo hajui kuchekesha ila alitakiwa aende hollywood akaigize na akina denzel washingtone
 
Mshkaji nimecheza nae sana pale olacity... Now nikimpigiaga simu hata apokei, mshkaji katukataa sana wadau
 
Jamaa alidakwa faster alafu akatupwa kule faster...


Cc: Mahondaw
Akawa anachezeshwa kuch kuch....wanapost video wakiwa ndani Iddy anamkimbiza kimbiza wema ameze dawa, wema na kile kisauti anakataa eti dawa chungu hadi ampe halua 🤣🤣🤣

Mambo yao tuwaachie wenyewe.
 
Akawa anachezeshwa kuch kuch....wanapost video wakiwa ndani Iddy anamkimbiza kimbiza wema ameze dawa, wema na kile kisauti anakataa eti dawa chungu hadi ampe halua 🤣🤣🤣

Mambo yao tuwaachie wenyewe.
Akili zilivyokuja kumkaa sawa, akakiri kwamba, matumizi ya wema kwa siku yalikua sii chini ya million 3 mpaka 5, alafu utamu anapimiwa...


Cc: Mahondaw
 
Back
Top Bottom