Unamkumbuka Said Ngamba "Mzee Small" kwa yapi?

Unamkumbuka Said Ngamba "Mzee Small" kwa yapi?

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
download.jpeg

Mfahamu Mzee Small.
Said Wangamba (Mzee Small) alizaliwa 1955 mkoani Lindi. Na baadae alihamia Dar mwaka 1970 ambapo alipata umaarufu kupitia uchekeshaji na uigizaji.

Alipewa jina la utani la Mzee Small kutokana na mwili wake kuwa mdogo. Alipata umaarufu kupitia baadhi ya kazi zake kama vile kama 'Hamsini Hamsini Mia' na 'Mjini Shule'.

Aliwahi kujiunga na vikundi mbalimbali vya sanaa vikiwemo Agizo Group, Muungano Culture Troupe, Shirika la Reli, Shirika la Wakala za Meli (Nasaco) na vingine kabla mwaka 1983 kwenda nchini Uingereza kwa maonyesho kadhaa ya sanaa.

Alifariki dunia Juni 8, 2014, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili amabapo alikuwa anapatiwa matibabu baada ya kuugua kiharusi kwa miaka miwili.

Mzee Small.jpg

PIA SOMA:
- TANZIA - Said Ngamba alias 'Mzee Small wa Ngamba' afariki dunia
 
Hivi kumbe ile hamsini hamsini mia ilikuwa yake, nilidhani ya mzee Majuto... namkumbuka alikuwa na mke wa sanaa bi. Chau...
 
Nakumbka lile tangazo lake la mafuta............. alikua kitchen akafuta jiko na 🤢🤢🤮kohozi,,, uuuuuuuiiiiiiiiiiii
 
Walikuwa wanapendezana sana wakiwa na Bi chau, naona yupo ITV bado maneno yale yale anachamba huyo sijui mtu wa wapi yule mama🤣
 
Ninachokumbuka Dunia imemeza vikubwa kuliko vilivyopo. Fikiria STEVE NYERERE ANADUNDA
 
Back
Top Bottom