Unaniudhi wewe...

md4doctor2000

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2012
Posts
736
Reaction score
315
Unaniudhi wewe.....Wewe usiojua vema matumizi sahihi ya herufi...

Utakuta mtu hajui atumie wapi 'l' na wapi atumie 'r', anabaki kuchanganya na kuleta maneno au sentensi isiyoeleweka vizuri. Mfano, badala ya kuandika/kutamka 'Iringa' anatamka 'Ilinga'; badala ya 'Arusha' atasema 'Alusha'; badala ya 'rais' anatamka au ataandika 'lais'. Akitaka kusema 'ilani' yeye atasema 'irani'.

Kuna mwingine naye anaudhi sana tu, yeye hajui atumie wapi 'dhi' na wapi atumie 'zi'! Utakuta anataka usema 'maudhui' atakachosema ni 'mauzui' au anataka kusema 'maradhi' atasema 'marazi'.

Jirekebishe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…