Unanua Gari Unakosa Parking unaamua Kulilaza Sheli

UMUGHAKA

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2021
Posts
2,753
Reaction score
12,932
Nsikuchoshe na Usinchoshe,tusichoshane!.

Umetafuta vipesa vyako kwa kudunduliza hatimaye ukanunua ki Spacio chako au Ki - Ist halafu mwisho wa siku unaamua kwenda kukilaza Sheli!.

Hakuna mtu mwenye wivu na kagari kako lakini nakutahadharisha ya kwamba Sheli si sehemu salama!.

Ni vema ukatafuta Maegesho mahali pengine ambapo ni salama lakini si Sheli kwasababu tunafahamu wote lile ni eneo maalumu kwa ajili ya vimiminika vinavyolipuka.

Kama wewe ni mwenzangu na mie ambaye hako ka gari kako kakiungua unabaki kubung'aa bung'aa tena ni vema ukajihadhari mapema;

Lakini kama wewe ni sawa na kina Bakhresa sina ushauri na wewe kwasababu hata ka-gari kako kakiungua utanunua kengine.

Ni hayo tu.
 

Mwenye pesa kama za Bakhresa halazi gari sheli..
 
Mi kagari kangu kukapaki hata chini ya Mti tu naogopa,sembuse kupaki petrol station,si ntakua naota kila usiku kagari kangu kanauungua,mwisho nitakua nalala usingizi wa mangamumangamu!!
 
Naongezea,watu wanapaki ccm,misikitini, nk

Ova
Tatizo makazi mengi ya uswahilini swala la parking au upitaji wa magari hadi mjengoni hilo hawakulizingatia, alafu kuna swala la ulinzi pia wa chombo chako!!
 
Mbona wenzako wananunua ndege na wanailaza uwanja wa ndege, cha ajabu kipi! Usijifanye wewe tajiri sana, wapo matajiri wananunua gari za bei kali kwa anili ya shambaboi wake.
 
Mbona wenzako wananunua ndege na wanailaza uwanja wa ndege, cha ajabu kipi! Usijifanye wewe tajiri sana, wapo matajiri wananunua gari za bei kali kwa anili ya shambaboi wake.
Hivi umekielewa nilichokiandika au umeandika ukiwa umelewa?
 
Kwa hiyo wanalaza gari kwenye kituo cha Mafuta (sio Shell - Kampuni ya Shell haiko Tanzania siku hizi) ili lisiibiwe; na wao wanatembea kwa Miguu kwenda Nyumbani?? Wakikabwa je??
 
Hivi umekielewa nilichokiandika au umeandika ukiwa umelewa?
Wewe umewabeza wanaonunua gari huku wanaishi kwenye vijumba visivyo na nafasi ya kutosha, acha hizo siku hizi gari si dili kwani hata wezi wanazo za kuiba.
 
Wewe umewabeza wanaonunua gari huku wanaishi kwenye vijumba visivyo na nafasi ya kutosha, acha hizo siku hizi gari si dili kwani hata wezi wanazo za kuiba.
Rudi Darasani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…