Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,336
- 4,731
Salaam wana jukwaa,
Kumekuwa na tabia ambayo kwa sasa imekuwa sugu sana kwa hizi kampuni za mawasiliano kuamua kupanga bei za vifurushi na kuvibadilisha wanavyoona wao bila hata kuangalia mlaji au mteja wao wanampa usumbufu wa kiasi gani.
Kero hiyo haiishii tu kwenye kubadilisha bei za vifurushi bali hata unaweza nunua data mara unakutana na ujumbe hongera kwa kununua kifushi cha data za WatsApp au Youtube tu nk hali lengo lako lilikuwa ni upate data ambazo zitakuwa huru kutumika kwa matumizi yote ya kimtandao bila kubagua upande wowote.
Wakati mwingine unajiunga bandle linaisha ndani ya muda mfupi tena kwa matumizi yaleyale ya kila siku ambayo kimsingi huwa unatumia kwa muda mrefu, au unajiunga mtandao unakata huwezi tumia na muda ukifika wa kufikia mwisho wa matumizi linaisha bila kujali kuwa chanzo cha kutotumia ni wao kusumbua mtandao.
Nachojiuliza mamlaka ya kumlinda mlaji hawaoni jinsi mlaji wa hivi vifurushi vya data ambavyo anatendewa ndivyosivyo? wao wako wapi mbona hatuoni wakitututea ili tupate kile ambacho tunakusudia?
Kumekuwa na tabia ambayo kwa sasa imekuwa sugu sana kwa hizi kampuni za mawasiliano kuamua kupanga bei za vifurushi na kuvibadilisha wanavyoona wao bila hata kuangalia mlaji au mteja wao wanampa usumbufu wa kiasi gani.
Kero hiyo haiishii tu kwenye kubadilisha bei za vifurushi bali hata unaweza nunua data mara unakutana na ujumbe hongera kwa kununua kifushi cha data za WatsApp au Youtube tu nk hali lengo lako lilikuwa ni upate data ambazo zitakuwa huru kutumika kwa matumizi yote ya kimtandao bila kubagua upande wowote.
Wakati mwingine unajiunga bandle linaisha ndani ya muda mfupi tena kwa matumizi yaleyale ya kila siku ambayo kimsingi huwa unatumia kwa muda mrefu, au unajiunga mtandao unakata huwezi tumia na muda ukifika wa kufikia mwisho wa matumizi linaisha bila kujali kuwa chanzo cha kutotumia ni wao kusumbua mtandao.
Nachojiuliza mamlaka ya kumlinda mlaji hawaoni jinsi mlaji wa hivi vifurushi vya data ambavyo anatendewa ndivyosivyo? wao wako wapi mbona hatuoni wakitututea ili tupate kile ambacho tunakusudia?