Raymanu KE
JF-Expert Member
- Jan 20, 2022
- 8,611
- 16,118
Nakumbuka kipindi nikiwa mdogo nilikuwa msumbufu Sana na mama yangu alikuwa mnoko Tena mkali ajabu.Kipindi hicho wiki isingeweza kuisha kabla sijachezea mabakora ya mama kutokana na ununda wangu.
Nakumbuka visasa kadha wa kadha ambavyo vilinisababishia adhabu Kali Sana kutoka kwa mama.Kuna siku nilijumuika na rafiki zangu kuwapeleka ng'ombe machungani.Tulikuwa takribani watoto Saba tukawakusanya ng'ombe wetu kwenye uwanja mmoja huku tunacheza mpira mixer kuwapiganisha ng'ombe ndume.Ng'ombe wangu mmoja aligongwa vibaya Sana kwa kudungwa dungwa mapembe na ng'ombe mwingine Hadi akafumuliwa kipande Cha ngozi.
Nilirudi nyumbani natetemeka Sana maana nilijua naenda kuchezea kichapo sio Cha sayari hii wakuu.Nyumbani palichimbika kinyama Yaani nilipigwa mafimbo mengi Sana nikalia Hadi nikazimia.Yaani unapigwa unalia Kisha unapigwa Tena ili unyamaze [emoji23].Ukishapigwa unaambiwa uchukue maji ya baridi uoge Kisha uende chumbani ukalale, chakula unanyimwa[emoji25]
Kisa Cha pili ile umerudi shuleni jioni kabsa kisha mama anakuamuru uchukue mtungi uwahi mtoni ukateke maji ya kunywa.Jamaa nazuga kuwa nimeenda mtoni kumbe nimepitia kwa rafiki yangu kucheza kibe.Giza kinaingia mtoni sijaenda na nyumbani wamesubiri maji.Nikaamua kuchota maji ya kisima na kurudi nyumbani.Kwa ujinga wangu kamwe sikuwahi jua kwamba ladha ya maji ya kisima Ni tofauti Sana na ladha ya maji ya mtoni.Mama akayaonja maji akakuta Ni ya kisimani kudadeki!!
Nilipigwa, nikachunwa,nikatukanwa mixer kunyimwa chakula.Usiku wa manane njaa imekuchachamaa unaanza kulia mama anaamka anawasha taa anakuja ananichapa Tena ili ninyamaze kulia.
Kipindi Cha utoto wangu nilipitia Mikasa mingi Sana ambayo siwezi kuielezea yote lakini ilinisababishia adhabu Kali Sana kutoka kwa mama.Lakini namshukuru Sana mama yangu coz adhabu zake zilininyoosha na kunifanya niwe na nidhamu ya Hali ya juu.Mungu ambariki mama yangu[emoji120][emoji120]
Nakumbuka visasa kadha wa kadha ambavyo vilinisababishia adhabu Kali Sana kutoka kwa mama.Kuna siku nilijumuika na rafiki zangu kuwapeleka ng'ombe machungani.Tulikuwa takribani watoto Saba tukawakusanya ng'ombe wetu kwenye uwanja mmoja huku tunacheza mpira mixer kuwapiganisha ng'ombe ndume.Ng'ombe wangu mmoja aligongwa vibaya Sana kwa kudungwa dungwa mapembe na ng'ombe mwingine Hadi akafumuliwa kipande Cha ngozi.
Nilirudi nyumbani natetemeka Sana maana nilijua naenda kuchezea kichapo sio Cha sayari hii wakuu.Nyumbani palichimbika kinyama Yaani nilipigwa mafimbo mengi Sana nikalia Hadi nikazimia.Yaani unapigwa unalia Kisha unapigwa Tena ili unyamaze [emoji23].Ukishapigwa unaambiwa uchukue maji ya baridi uoge Kisha uende chumbani ukalale, chakula unanyimwa[emoji25]
Kisa Cha pili ile umerudi shuleni jioni kabsa kisha mama anakuamuru uchukue mtungi uwahi mtoni ukateke maji ya kunywa.Jamaa nazuga kuwa nimeenda mtoni kumbe nimepitia kwa rafiki yangu kucheza kibe.Giza kinaingia mtoni sijaenda na nyumbani wamesubiri maji.Nikaamua kuchota maji ya kisima na kurudi nyumbani.Kwa ujinga wangu kamwe sikuwahi jua kwamba ladha ya maji ya kisima Ni tofauti Sana na ladha ya maji ya mtoni.Mama akayaonja maji akakuta Ni ya kisimani kudadeki!!
Nilipigwa, nikachunwa,nikatukanwa mixer kunyimwa chakula.Usiku wa manane njaa imekuchachamaa unaanza kulia mama anaamka anawasha taa anakuja ananichapa Tena ili ninyamaze kulia.
Kipindi Cha utoto wangu nilipitia Mikasa mingi Sana ambayo siwezi kuielezea yote lakini ilinisababishia adhabu Kali Sana kutoka kwa mama.Lakini namshukuru Sana mama yangu coz adhabu zake zilininyoosha na kunifanya niwe na nidhamu ya Hali ya juu.Mungu ambariki mama yangu[emoji120][emoji120]