Unapokuwa kwenye situation ya namna hii... unafanyaje?

Unapokuwa kwenye situation ya namna hii... unafanyaje?

MwanajamiiOne

Platinum Member
Joined
Jul 24, 2008
Posts
10,470
Reaction score
6,580
Maisha ya ndoa na mahusiano ni kama kuna maboksi ambayo tunatamani kuwa nayo na kuyabeba maisha yetu yote. Wengi wetu hupata bahati ya kupata mabox mema na wengine huambulia mengine ambayo tungejua tungefikiria kwanza kabla ya kuamua kuyabeba!

Wengi wetu tumejikuta tumebeba maboksi ambayo tunadhani ni yetu na kwa furaha kubwa huwa tunawaringishia wengine hasa kutokana uzuri wa boksi kwa nje tukitegemea na ndani litakuwa na kitu kizuri.
Hata hivyo tukifika majumbani tunashangaa huku vitu vilivyomo ndani ya boksi ni kinyume chake. Mara nyingi tunaambulia maboksi ambayo ndani yake yamejaa viboksi vingine vingi kama vile hasira, ukali, au manyanyaso ya kila aina, maneno magumu na mazito ambayo hukuumiza zaidi ya kupigwa ngumi na mateke.

Mbaya zaidi pale pale box lenyewe likijua kwamba wewe ni mbebaji mzuri basi utachakaa kwa kubeba hili boksi.

Hali hii huitwa “Narcissism” hili ni neno la kigiriki lenye maana ya mtu kuipenda zaidi nafsi yake kuliko kawaida (extreme self-loving). Tatizo ambalo huanzia utotoni baada ya mtu kukosa upendo so anapokuwa mtu mzima anakuwa hajui maana ya kupenda na kupendwa.

Utafiti unaonesha ni asilimia 75 wana kaasili ka narcissists na kinara wao akiwa Adolph Hitler. Wengi wetu tunao akina Hitler kwenye mahusiano yetu ya kimapenzi. Pale ambapo mpenzi wako anachofanya ni kukubebesha kiboksi cha wewe Kujiona una hatia, anakupa hofu, woga, mashaka, anakufanya usijiamini ili akupelekesha anavyotaka yeye. Wakati mwingine anaweza kudhalilisha kimwili, kimapenzi, kihisia na pia anaweza kuzira kuongea (silence) na anachofanya ni kuku-control wewe idara zote za maisha yako unakuwa kama mfungwa fulani kwa kuwa umeingia kwenye anga zake.

Wapenzi wa namna hii wanaume au wanawake hufurahia sana kutesa wake zao au waume zao, hawana huruma wala haya.

Source:The Hill Of Wealth


Je unapojikuta unaye mtu wa hivi na wewe umeolewa/ oa kanisani ndoa ya kikristo. Unafanyaje?
 
Maisha ya ndoa na mahusiano ni kama kuna maboksi ambayo tunatamani kuwa nayo na kuyabeba maisha yetu yote. Wengi wetu hupata bahati ya kupata mabox mema na wengine huambulia mengine ambayo tungejua tungefikiria kwanza kabla ya kuamua kuyabeba!

Wengi wetu tumejikuta tumebeba maboksi ambayo tunadhani ni yetu na kwa furaha kubwa huwa tunawaringishia wengine hasa kutokana uzuri wa boksi kwa nje tukitegemea na ndani litakuwa na kitu kizuri.
Hata hivyo tukifika majumbani tunashangaa huku vitu vilivyomo ndani ya boksi ni kinyume chake. Mara nyingi tunaambulia maboksi ambayo ndani yake yamejaa viboksi vingine vingi kama vile hasira, ukali, au manyanyaso ya kila aina, maneno magumu na mazito ambayo hukuumiza zaidi ya kupigwa ngumi na mateke.

Mbaya zaidi pale pale box lenyewe likijua kwamba wewe ni mbebaji mzuri basi utachakaa kwa kubeba hili boksi.

Hali hii huitwa “Narcissism” hili ni neno la kigiriki lenye maana ya mtu kuipenda zaidi nafsi yake kuliko kawaida (extreme self-loving). Tatizo ambalo huanzia utotoni baada ya mtu kukosa upendo so anapokuwa mtu mzima anakuwa hajui maana ya kupenda na kupendwa.

Utafiti unaonesha ni asilimia 75 wana kaasili ka narcissists na kinara wao akiwa Adolph Hitler. Wengi wetu tunao akina Hitler kwenye mahusiano yetu ya kimapenzi. Pale ambapo mpenzi wako anachofanya ni kukubebesha kiboksi cha wewe Kujiona una hatia, anakupa hofu, woga, mashaka, anakufanya usijiamini ili akupelekesha anavyotaka yeye. Wakati mwingine anaweza kudhalilisha kimwili, kimapenzi, kihisia na pia anaweza kuzira kuongea (silence) na anachofanya ni kuku-control wewe idara zote za maisha yako unakuwa kama mfungwa fulani kwa kuwa umeingia kwenye anga zake.

Wapenzi wa namna hii wanaume au wanawake hufurahia sana kutesa wake zao au waume zao, hawana huruma wala haya.

Source:The Hill Of Wealth


Je unapojikuta unaye mtu wa hivi na wewe umeolewa/ oa kanisani ndoa ya kikristo. Unafanyaje?

Mj1,
Napenda sana unavyoleta mada za kweli zenye kulenga maisha yetu ya kila siku ya vitendo na siyo nadharia tu.
Mpendwa, bahati mbaya sana watu tunaingia kwenye vifungo/ndoa/pingu bila kujitambua "siye ni nani" na "hao wenzetu ni nani".This should have been the starting point.
1.Kujijua wewe ni nani ( SW(OT)- utaelewa strengths, weakness na hivyo basi utajaribu kumuelewa huyo uliyempata na kuamua je uko tayari kumbeba na mapungufu yake? je anayo strength ya kuweza kukuvumilia mapungufu yako?
2. Tunapaswa/tungepaswa pia kujua zaidi kuhusu mizizi yetu na ile ya wenzetu na kuona kama kuna vitu/tabia ambazo zinaweza/zingeweza kuwa zimewaathiri na hivyo kujakuwa donda kwenye mahusiano yetu.Unajua enzi za mababu na hata mpaka sasa kuna familia utasikia zikisema hatuoi ukoo fulani..etc kulikuwa na maana kubwa maana walishajua kabisa kuwa hizo tabia zinaweza kurithiwa na kuja kuwa balaa.Hii ni over and above magonjwa ya kuambukiza etc.Tuna bahati mbaya sana kuwa kwa maisha ya sasa hivi ni vigumu kufuata hii misingi maana watu wanaoana kutoka makabila mbalimbali au pia wameishi mijini sana hata mila na desturi hatufuati tena.

Ila kwa kujaribu kujibu suali lako, ukishajikuta uko kwenye ndoa na hali ndiyo hiyo, kwanza mtu unapaswa kukubali kuwa ulifanya makosa toka unajiandaa kuoana na huyo mtu.Halafu unatakiwa ujaribu kufanya ufahamu huo hapo juu na kuona ni vipi sasa mtavumiliana.
Nitaendelea kuchangia tena baadae maana ninayo mengi ya kusema.
 
uvumilivu ni kitu muhimu sana ndani, bila hiyo hamtasonga, kipindi cha uchumba mtu unaona kwamba huyu kweli ndio mume aliestahili kuwa wangu, but mkishaingia ndani unaweza kujuta/kuona haku deserve but too late, na ndoa ze2 za kikristo ndo hizo za mpaka kifo ki2tenganishe, kwangu mie nitatenganishwa na pale ninapoona mambo kila kukicha yanazidi unga, misuko suko/malumbano na yote ya kero ni ya kawaida na yawe na kipimo chake.
 
Maisha ya ndoa na mahusiano ni kama kuna maboksi ambayo tunatamani kuwa nayo na kuyabeba maisha yetu yote. Wengi wetu hupata bahati ya kupata mabox mema na wengine huambulia mengine ambayo tungejua tungefikiria kwanza kabla ya kuamua kuyabeba!

Wengi wetu tumejikuta tumebeba maboksi ambayo tunadhani ni yetu na kwa furaha kubwa huwa tunawaringishia wengine hasa kutokana uzuri wa boksi kwa nje tukitegemea na ndani litakuwa na kitu kizuri.
Hata hivyo tukifika majumbani tunashangaa huku vitu vilivyomo ndani ya boksi ni kinyume chake. Mara nyingi tunaambulia maboksi ambayo ndani yake yamejaa viboksi vingine vingi kama vile hasira, ukali, au manyanyaso ya kila aina, maneno magumu na mazito ambayo hukuumiza zaidi ya kupigwa ngumi na mateke.

Mbaya zaidi pale pale box lenyewe likijua kwamba wewe ni mbebaji mzuri basi utachakaa kwa kubeba hili boksi.

Hali hii huitwa “Narcissism” hili ni neno la kigiriki lenye maana ya mtu kuipenda zaidi nafsi yake kuliko kawaida (extreme self-loving). Tatizo ambalo huanzia utotoni baada ya mtu kukosa upendo so anapokuwa mtu mzima anakuwa hajui maana ya kupenda na kupendwa.

Utafiti unaonesha ni asilimia 75 wana kaasili ka narcissists na kinara wao akiwa Adolph Hitler. Wengi wetu tunao akina Hitler kwenye mahusiano yetu ya kimapenzi. Pale ambapo mpenzi wako anachofanya ni kukubebesha kiboksi cha wewe Kujiona una hatia, anakupa hofu, woga, mashaka, anakufanya usijiamini ili akupelekesha anavyotaka yeye. Wakati mwingine anaweza kudhalilisha kimwili, kimapenzi, kihisia na pia anaweza kuzira kuongea (silence) na anachofanya ni kuku-control wewe idara zote za maisha yako unakuwa kama mfungwa fulani kwa kuwa umeingia kwenye anga zake.

Wapenzi wa namna hii wanaume au wanawake hufurahia sana kutesa wake zao au waume zao, hawana huruma wala haya.

Source:The Hill Of Wealth


Je unapojikuta unaye mtu wa hivi na wewe umeolewa/ oa kanisani ndoa ya kikristo. Unafanyaje?
Nakushauri fanya yafuatayo:
1.Tafuta mtu unayemwamini na ZUNGUMZA YOTE YANAYOKUKERA.Nafikiri hii thread ni mwendelezo wa zile nyingine ulizoweka hapa.Ni wazi unalotatizo limekuzonga, unahitaji msaada.

2.Kama una mtoto au watoto hamisha mapenzi kwao, usifikiri chochote zaidi yao.

3.Kama huna, weka mapenzi yako kwenye kazi unayofanya.Amka asubuhi ukifikiria kazi tu,fanya kazi mpaka late hours, then rudi nyumbani.

Unakumbuka zile stages nilizokueleza? elewa upo stage gani na songa mbele.
 
Mj1,
Napenda sana unavyoleta mada za kweli zenye kulenga maisha yetu ya kila siku ya vitendo na siyo nadharia tu.
Mpendwa, bahati mbaya sana watu tunaingia kwenye vifungo/ndoa/pingu bila kujitambua "siye ni nani" na "hao wenzetu ni nani".This should have been the starting point.
1.Kujijua wewe ni nani ( SW(OT)- utaelewa strengths, weakness na hivyo basi utajaribu kumuelewa huyo uliyempata na kuamua je uko tayari kumbeba na mapungufu yake? je anayo strength ya kuweza kukuvumilia mapungufu yako?

Aksante WoS. Haya yote ni maisha yanayotutokea sisi binadamu kama si kwangu basi yupo ambaye yuko katika hali hizi tunazozizungumzia hapa JF kwa namna moja au nyingine.

Nakubaliana kabisa na wewe WoS dada yangu na nadhani hiki ni kitu kikubwa zaidi cha kujifahamu wewe kwanza ili uweze kudetermine the kind of a person unayetaka kuishi naye. Bahati mbaya sana kwa watu wengine inatuwia vigumu kuweza kujitambua (sijaelewa ni kwa nini). Wengi wetu huwa tunazibwa mioyo na maneno matamu, muonekano wa mtu na hata hali yake (kifedha) bila kusahau laghai mbalimbali tunazokutana nazo. Matokeo yake tunakuja kushtuka when it is too late.

2. Tunapaswa/tungepaswa pia kujua zaidi kuhusu mizizi yetu na ile ya wenzetu na kuona kama kuna vitu/tabia ambazo zinaweza/zingeweza kuwa zimewaathiri na hivyo kujakuwa donda kwenye mahusiano yetu.Unajua enzi za mababu na hata mpaka sasa kuna familia utasikia zikisema hatuoi ukoo fulani..etc kulikuwa na maana kubwa maana walishajua kabisa kuwa hizo tabia zinaweza kurithiwa na kuja kuwa balaa.Hii ni over and above magonjwa ya kuambukiza etc.Tuna bahati mbaya sana kuwa kwa maisha ya sasa hivi ni vigumu kufuata hii misingi maana watu wanaoana kutoka makabila mbalimbali au pia wameishi mijini sana hata mila na desturi hatufuati tena.

ni kweli kabisa wazee wetu walikuwa na hayo na yalitusaidia sana katika kuminimize matatizo kama haya. Na ni kweli kabisa kuwa vizazi vya leo ambavyo saa nyingine tunakutanishwa na technologia, intertribal marriages na hata inter-racial inakuwa vigumu kufuatilia mizizi hiyo.

Ila kwa kujaribu kujibu suali lako, ukishajikuta uko kwenye ndoa na hali ndiyo hiyo, kwanza mtu unapaswa kukubali kuwa ulifanya makosa toka unajiandaa kuoana na huyo mtu.Halafu unatakiwa ujaribu kufanya ufahamu huo hapo juu na kuona ni vipi sasa mtavumiliana.
Nitaendelea kuchangia tena baadae maana ninayo mengi ya kusema.


Ni sawa kabisa swala la uvumilivu ni muhimu unapokuwa katika situation kama hii. Lakini ni kweli hakuna kitu kingine cha kufanya zaidi ya kuvumilia?. How can you handle mtu ambaye ni selfish kupita kiasi mtu ambaye anaweza hata kukubali wewe uumiekutokana na maneno yake ya kashfa na maumivu? Naombeni mbinu
 
You resort to nyumba ndogo mdau, coz kudivorce sio ishu na kumepitwa na wakati na ukizingatia hujui huyo utakayemparamia tena! So better get involved to nyumba ndogo kwa sababu ya flexibility, yani ukigundua ni mzigo unmbwaga leo na kesho you look fo new adventures!
 
Mj1,
Napenda sana unavyoleta mada za kweli zenye kulenga maisha yetu ya kila siku ya vitendo na siyo nadharia tu.
Mpendwa, bahati mbaya sana watu tunaingia kwenye vifungo/ndoa/pingu bila kujitambua "siye ni nani" na "hao wenzetu ni nani".This should have been the starting point.
1.Kujijua wewe ni nani ( SW(OT)- utaelewa strengths, weakness na hivyo basi utajaribu kumuelewa huyo uliyempata na kuamua je uko tayari kumbeba na mapungufu yake? je anayo strength ya kuweza kukuvumilia mapungufu yako?
2. Tunapaswa/tungepaswa pia kujua zaidi kuhusu mizizi yetu na ile ya wenzetu na kuona kama kuna vitu/tabia ambazo zinaweza/zingeweza kuwa zimewaathiri na hivyo kujakuwa donda kwenye mahusiano yetu.Unajua enzi za mababu na hata mpaka sasa kuna familia utasikia zikisema hatuoi ukoo fulani..etc kulikuwa na maana kubwa maana walishajua kabisa kuwa hizo tabia zinaweza kurithiwa na kuja kuwa balaa.Hii ni over and above magonjwa ya kuambukiza etc.Tuna bahati mbaya sana kuwa kwa maisha ya sasa hivi ni vigumu kufuata hii misingi maana watu wanaoana kutoka makabila mbalimbali au pia wameishi mijini sana hata mila na desturi hatufuati tena.

Ila kwa kujaribu kujibu suali lako, ukishajikuta uko kwenye ndoa na hali ndiyo hiyo, kwanza mtu unapaswa kukubali kuwa ulifanya makosa toka unajiandaa kuoana na huyo mtu.Halafu unatakiwa ujaribu kufanya ufahamu huo hapo juu na kuona ni vipi sasa mtavumiliana.
Nitaendelea kuchangia tena baadae maana ninayo mengi ya kusema.

Avatar yako ya awali ilikuwa nzuri zaidi
 
Nakushauri fanya yafuatayo:
1.Tafuta mtu unayemwamini na ZUNGUMZA YOTE YANAYOKUKERA.Nafikiri hii thread ni mwendelezo wa zile nyingine ulizoweka hapa.Ni wazi unalotatizo limekuzonga, unahitaji msaada.

2.Kama una mtoto au watoto hamisha mapenzi kwao, usifikiri chochote zaidi yao.

3.Kama huna, weka mapenzi yako kwenye kazi unayofanya.Amka asubuhi ukifikiria kazi tu,fanya kazi mpaka late hours, then rudi nyumbani.

Unakumbuka zile stages nilizokueleza? elewa upo stage gani na songa mbele.

Bonnie not necessarily yanikute mimi haya yote ni maisha yanayotutokea sisi binadamu kama si kwangu basi yupo ambaye yuko katika hali hizi tunazozizungumzia hapa JF kwa namna moja au nyingine

Mh unazungumzia kuhamisha mapenzi kwa mtoto ndo kufanyaje? Can you stop loving the man/woman of your heart ukahamishia kwa mtoto?. Is it possible kuwa na amani kwa kufanya hivyo tu?
 
Aksante WoS. Haya yote ni maisha yanayotutokea sisi binadamu kama si kwangu basi yupo ambaye yuko katika hali hizi tunazozizungumzia hapa JF kwa namna moja au nyingine.

Nakubaliana kabisa na wewe WoS dada yangu na nadhani hiki ni kitu kikubwa zaidi cha kujifahamu wewe kwanza ili uweze kudetermine the kind of a person unayetaka kuishi naye. Bahati mbaya sana kwa watu wengine inatuwia vigumu kuweza kujitambua (sijaelewa ni kwa nini). Wengi wetu huwa tunazibwa mioyo na maneno matamu, muonekano wa mtu na hata hali yake (kifedha) bila kusahau laghai mbalimbali tunazokutana nazo. Matokeo yake tunakuja kushtuka when it is too late.



ni kweli kabisa wazee wetu walikuwa na hayo na yalitusaidia sana katika kuminimize matatizo kama haya. Na ni kweli kabisa kuwa vizazi vya leo ambavyo saa nyingine tunakutanishwa na technologia, intertribal marriages na hata inter-racial inakuwa vigumu kufuatilia mizizi hiyo.




Ni sawa kabisa swala la uvumilivu ni muhimu unapokuwa katika situation kama hii. Lakini ni kweli hakuna kitu kingine cha kufanya zaidi ya kuvumilia?. How can you handle mtu ambaye ni selfish kupita kiasi mtu ambaye anaweza hata kukubali wewe uumiekutokana na maneno yake ya kashfa na maumivu? Naombeni mbinu
Mj1,
Zipo namna mbalimbali na mimi binafsi naamini zaidi katika zile zenye kujikita katika imani zetu za dini .. ila sidhani ni vema kuziweka hapa maana JF ni ya watu wenye imani tofauti tofauti.

Asikudanganye mtu , usipoweza kutibu kuanzia chanzo cha tabia ( ambazo zaweza kurithiwa hadi vizazi vinne) no matter what step you take haitaleta suluhisho - utaenda kwenye counselling, utaenda kwa wazazi..mtaka vikao visivyoisha, mtashtaki kwa wasimamizi wa ndoa... na kote huko ni kama kujitibia na panadol upunguze maumivu lakini si kutibu ugonjwa.Kama ni malaria itahitaji ALU au sijui metakelfin ( orijino) na si vinginevyo.

Watu wengine wanachukua njia za mkato - talaka/kutengana kila mtu aishi mwenyewe, wengine huishi kibabe humohumo ndani kila mtu akiingia na kutoka kwa wakati wake kama wapangaji, wengine huamua kuvumilia na kuishi kwa mateso - yote kutegemeana na ugumu wa roho ya mhusika au faida anazozipata kwa kuchukua uamuzi huo.
 
You resort to nyumba ndogo mdau, coz kudivorce sio ishu na kumepitwa na wakati na ukizingatia hujui huyo utakayemparamia tena! So better get involved to nyumba ndogo kwa sababu ya flexibility, yani ukigundua ni mzigo unmbwaga leo na kesho you look fo new adventures!

Duh this......... I didnt see it coming!

matters of the heart.
 
You resort to nyumba ndogo mdau, coz kudivorce sio ishu na kumepitwa na wakati na ukizingatia hujui huyo utakayemparamia tena! So better get involved to nyumba ndogo kwa sababu ya flexibility, yani ukigundua ni mzigo unmbwaga leo na kesho you look fo new adventures!

Mkuu!
Inaweza ikakugharibu vikubwa zaidi..na ukitaka kuibwaga haibwagiki
( un-bwagable!)
 
In reality
Ni katika stage hii ndipo watu huanza kuingia kwenye masuala ya Extramarital affairs(NYUMBA NDOGO),kama hutokuwa mwangalifu.

Suala moja la msingi ni JE,WHAT IF THAT NYUMBA NDOGO ITAKUWA UN-BWAGABLE? KAULIZA VIZURI HUYU WOS.
 
In reality
Ni katika stage hii ndipo watu huanza kuingia kwenye masuala ya Extramarital affairs(NYUMBA NDOGO),kama hutokuwa mwangalifu.

Suala moja la msingi ni JE,WHAT IF THAT NYUMBA NDOGO ITAKUWA UN-BWAGABLE? KAULIZA VIZURI HUYU WOS.
 
Ni sawa kabisa swala la uvumilivu ni muhimu unapokuwa katika situation kama hii. Lakini ni kweli hakuna kitu kingine cha kufanya zaidi ya kuvumilia?. How can you handle mtu ambaye ni selfish kupita kiasi mtu ambaye anaweza hata kukubali wewe uumiekutokana na maneno yake ya kashfa na maumivu? Naombeni mbinu[/QUOTE]

Pole sana ndugu, watu wa namna hiyo wewe kaa kimya kwa kumdharau tuu kimoyo moyo ila usimuonyeshe...jaribu kuwa busy sana na kazi zako, usimuonyeshe mapenzi then kuwa na furaha kila wakati hata kama yeye kanuna. Yani muone kama sisimizi mbele yako but usimuonyeshe. Sijui umenielewa.
 
Ni sawa kabisa swala la uvumilivu ni muhimu unapokuwa katika situation kama hii. Lakini ni kweli hakuna kitu kingine cha kufanya zaidi ya kuvumilia?. How can you handle mtu ambaye ni selfish kupita kiasi mtu ambaye anaweza hata kukubali wewe uumiekutokana na maneno yake ya kashfa na maumivu? Naombeni mbinu

Pole sana ndugu, watu wa namna hiyo wewe kaa kimya kwa kumdharau tuu kimoyo moyo ila usimuonyeshe...jaribu kuwa busy sana na kazi zako, usimuonyeshe mapenzi then kuwa na furaha kila wakati hata kama yeye kanuna. Yani muone kama sisimizi mbele yako but usimuonyeshe. Sijui umenielewa.[/QUOTE]

Penny unaeleweka vizuri but mh ni kazi maana soon unapoanza kumdharau kimoyomoyo sidhani kama utakuwa unamfeel hata katika tendo! Utatamani uhame nyumba.

How can you not onyesha mapenzi kwa mtu wako? Maana huyu wa hivi si kwamba mnakasirikiana mfululizo hapana kuna wakati mnacheka but hammalizi wiki mshagombana tena yeye ndo anayekuudhi.
 
Mi iwa nawaambia maisha ya uhawala ni maisha mazuri sana kuliko ndoa zenu hizi mnazo ng'ang'ania mliopo kwenye ndoa mtupe raha ya ndoa na karaha zake lakini nafikiri karaha ndo nyingi sana.
 
In reality
Ni katika stage hii ndipo watu huanza kuingia kwenye masuala ya Extramarital affairs(NYUMBA NDOGO),kama hutokuwa mwangalifu.

Suala moja la msingi ni JE,WHAT IF THAT NYUMBA NDOGO ITAKUWA UN-BWAGABLE? KAULIZA VIZURI HUYU WOS.

. Ni kweli mtu unawezapata mawazo ya kujaribu bahati yako ya kupendwa kwenye nyumba ndogo but is that a solution? Maana unawezajikuta umeruka majivu ukakanyaga moto.

Nimeileta hii situation hapa (kama inavyoonekkana nilikoitoa) kwa sababu mimi nimesoma kisha nikawaza kama najikuta katika situation kama hii nafanyaje harakaharaka nikapata jibu la kumwaga (divorce) but nikajiuliza tena what if mmefunga ndoa ya kanisa ya kikristo ambayo huwa hakuna kuachana unless kifo kiingilie kati, nikakosa jibu ndo mana nikaileta hapa.

Bonnie ya kwangu yapo ila hayajafikia huku (kumbuka kama sitabadili mwelekeo ndoa yangu itafungwa November (ya July 2009 nimeiahirisha kwanza)
 
...kwa kujaribu kujibu suali lako, ukishajikuta uko kwenye ndoa na hali ndiyo hiyo, kwanza mtu unapaswa kukubali kuwa ulifanya makosa toka unajiandaa kuoana na huyo mtu.Halafu unatakiwa ujaribu kufanya ufahamu huo hapo juu na kuona ni vipi sasa mtavumiliana.Nitaendelea kuchangia tena baadae maana ninayo mengi ya kusema.

uvumilivu ni kitu muhimu sana ndani, bila hiyo hamtasonga, kipindi cha uchumba mtu unaona kwamba huyu kweli ndio mume aliestahili kuwa wangu, but mkishaingia ndani unaweza kujuta/kuona haku deserve but too late, na ndoa ze2 za kikristo ndo hizo za mpaka kifo ki2tenganishe, kwangu mie nitatenganishwa na pale ninapoona mambo kila kukicha yanazidi unga, misuko suko/malumbano na yote ya kero ni ya kawaida na yawe na kipimo chake.

Mj1,
Zipo namna mbalimbali na mimi binafsi naamini zaidi katika zile zenye kujikita katika imani zetu za dini .. ila sidhani ni vema kuziweka hapa maana JF ni ya watu wenye imani tofauti tofauti.

Asikudanganye mtu , usipoweza kutibu kuanzia chanzo cha tabia ( ambazo zaweza kurithiwa hadi vizazi vinne) no matter what step you take haitaleta suluhisho - utaenda kwenye counselling, utaenda kwa wazazi..mtaka vikao visivyoisha, mtashtaki kwa wasimamizi wa ndoa... na kote huko ni kama kujitibia na panadol upunguze maumivu lakini si kutibu ugonjwa.Kama ni malaria itahitaji ALU au sijui metakelfin ( orijino) na si vinginevyo.

Watu wengine wanachukua njia za mkato - talaka/kutengana kila mtu aishi mwenyewe, wengine huishi kibabe humohumo ndani kila mtu akiingia na kutoka kwa wakati wake kama wapangaji, wengine huamua kuvumilia na kuishi kwa mateso - yote kutegemeana na ugumu wa roho ya mhusika au faida anazozipata kwa kuchukua uamuzi huo.

...Penny unaeleweka vizuri but mh ni kazi maana soon unapoanza kumdharau kimoyomoyo sidhani kama utakuwa unamfeel hata katika tendo! Utatamani uhame nyumba.

How can you not onyesha mapenzi kwa mtu wako? Maana huyu wa hivi si kwamba mnakasirikiana mfululizo hapana kuna wakati mnacheka but hammalizi wiki mshagombana tena yeye ndo anayekuudhi.

...kina mama, 😀 michango yenu imejaa busara, nimetulia tuli nikijifunza mengi! endeleeni 'kutufunda!'
 
Inahitaji neema ya Mungu kuujua undani wa mtu - moyo wa mwanadamu unaficha siri nyingi sana - tabia mbaya etc. na mara nyingi watu wako kwenye ndoa bila kujua kilichoko ndani na hii inatokana na KUZITEGEMEA AKILI ZETU bila KUMHUSISHA MUNGU KIKAMILIFU KATIKA KILA JAMBO - ili kukiwa na TATIZO uweze kumhusisha MUNGU uliyemhusisha toka mwanzo -

Kuvumilia mateso muda mrefu - na haswa usiseme kitu - unaumia ndani kwa ndani inasababisha magonjwa kama CANCER, VIDONDA VYA TUMBO, WOGA, WASIWASI na KUFUPISHA MAISHA YA MTU -
WANAUME na WANAWAKE WOTE TUJIREKEBISHE - MWONE MWENZAKO ANA THAMANI KULIKO WEWE, JENGA KUMHESHIMU MWENZAKO na kufanya hayo hutaweza kumtukana, kumpa maneno makali etc. TUACHE TAMAA YA MACHO - VITU HAVILETI RAHA YA KWELI BALI AMANI NDIO INALETA RAHA -

WATU WENGINE wanaingia kwenye NDOA bila kujipanga - wanafanya kama fasheni - mradi kuna kuoa/kuolewa - namimi nifanye hivyo - UNAPOTAKA KUJENGA NYUMBA INABIDI UHESABU GHARAMA YA UJENZI - LA SIVYO UTAISHIA KATIKATI

Mungu ana uwezo wa kuubadilisha moyo wa mtu - hivyo mwombee mwenzi wako unapoona udhaifu wowote kabla hujaanza kulalamika kwa marafiki, ndugu etc. ambao wengi wao wanatumika kuwa maadui wakubwa wa ndoa -

SHETANI ni mvurugaji mkubwa wa NDOA - alianza tangu enzi za Bustani ya EDENi - Adamu na Hawa - walidanganyana wakamkosea Mungu - na hadi leo SHETANI YUPO - UKIMGUNDUA NA KUMPINGA - MAFANIKIO KWENYE NDOA YAPO

NAWASILISHA
 
Back
Top Bottom