beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,880
- 6,368
KWANINI "KASONGO" ILITUNGWA.
Jina lake halisi aliitwa Kasongo wa Kanema, aliyekuwa Mwanamuziki Mkongwe wa Congo ambaye alihamia Nairobi na kufariki huko miaka minne iliyopita (Aprili 15, 2020) na kuzikwa kwenye makaburi ya Lang'ata.
Alikuwa sehemu ya kikundi cha wanamuziki wa Congo waliohamia Kenya mwanzoni mwa miaka ya 1970, chini ya ulezi wa nguli, Baba Ilunga wa Ilunga, kutafuta maisha mazuri wakati Kinshasa haikuwa matumaini mazuri kwa bendi nyingi.
Kasongo anakumbukwa zaidi kwa sauti yake kuu katika wimbo wa evergreen wa Kakolele Viva Christmas.
Wimbo wa "Kasongo" umekuwa ikivuma sana kwa siku za hivi Karibuni lakini ni wachache wanaofahamu hadithi ya wimbo huo.
"Kasongo" ilifanywa na bendi Kongwe ya Super Mazembe, bendi ya Kongo iliyohamia Kenya mwaka wa 1974 ambapo Kasongo amewahi kuiongoza bendi hiyo.
Waimbaji hao walikuwa wamekwenda kumtembelea rafiki yao Kasongo huko Eastleigh, Nairobi. Walipofika nyumbani kwake, walikutana na mke wa Kasongo na wakamuuliza kama alikuwa nyumbani. Mke wa Kasongo aliwakaribisha na kuwaambia kuwa hajaonana na Kasongo siku nyingi.
Wakati huo, hakukuwa na internet na ilikuwa nadra kupata mtu anayemiliki simu. Hivyo, waliamua kumtumia ujumbe kwa njia ya muziki, wakitumaini kwamba ungemfikia.
Wanamuziki hao wa Super Mazembe walianza kumtengenezea Kasongo wimbo sebuleni kwake wakimwambia arudi nyumbani kwa sababu mkewe anahangaika anamtafuta lakini hampati. Waliendelea kurekodi wimbo na, kama wanavyosema, iliyobaki ni historia.
MAANA YA WIMBO WA KASONGO
[Chorus]
Kasongo ye yeee, mobali na ngai,[Kasongo mume wangu]
Kasongo nga nawe oo,
[Kasongo nina kufa]
Zonga libala ee
[Rudi kwenye ndoa] x2
Kasongo yo yo, mobali na ngai [Kasongo mume wangu]
Kasongo nga nawe oo
[Kasongo nina kufa]
Zonga libala ee
[Rudi kwenye ndoa]
[Chorus]
Nga na ndako Kasongo
[Nikiwa nyumbani, Kasongo]
Miso na nzela
[Kutwa kukodoa macho barabarani]
Soki okozonga dia ee
[Ikiwa utarudi]
Yebisa nga ye ee
[Nitaarifu Mpendwa]
Jina lake halisi aliitwa Kasongo wa Kanema, aliyekuwa Mwanamuziki Mkongwe wa Congo ambaye alihamia Nairobi na kufariki huko miaka minne iliyopita (Aprili 15, 2020) na kuzikwa kwenye makaburi ya Lang'ata.
Alikuwa sehemu ya kikundi cha wanamuziki wa Congo waliohamia Kenya mwanzoni mwa miaka ya 1970, chini ya ulezi wa nguli, Baba Ilunga wa Ilunga, kutafuta maisha mazuri wakati Kinshasa haikuwa matumaini mazuri kwa bendi nyingi.
Kasongo anakumbukwa zaidi kwa sauti yake kuu katika wimbo wa evergreen wa Kakolele Viva Christmas.
Wimbo wa "Kasongo" umekuwa ikivuma sana kwa siku za hivi Karibuni lakini ni wachache wanaofahamu hadithi ya wimbo huo.
"Kasongo" ilifanywa na bendi Kongwe ya Super Mazembe, bendi ya Kongo iliyohamia Kenya mwaka wa 1974 ambapo Kasongo amewahi kuiongoza bendi hiyo.
Waimbaji hao walikuwa wamekwenda kumtembelea rafiki yao Kasongo huko Eastleigh, Nairobi. Walipofika nyumbani kwake, walikutana na mke wa Kasongo na wakamuuliza kama alikuwa nyumbani. Mke wa Kasongo aliwakaribisha na kuwaambia kuwa hajaonana na Kasongo siku nyingi.
Wakati huo, hakukuwa na internet na ilikuwa nadra kupata mtu anayemiliki simu. Hivyo, waliamua kumtumia ujumbe kwa njia ya muziki, wakitumaini kwamba ungemfikia.
Wanamuziki hao wa Super Mazembe walianza kumtengenezea Kasongo wimbo sebuleni kwake wakimwambia arudi nyumbani kwa sababu mkewe anahangaika anamtafuta lakini hampati. Waliendelea kurekodi wimbo na, kama wanavyosema, iliyobaki ni historia.
MAANA YA WIMBO WA KASONGO
[Chorus]
Kasongo ye yeee, mobali na ngai,[Kasongo mume wangu]
Kasongo nga nawe oo,
[Kasongo nina kufa]
Zonga libala ee
[Rudi kwenye ndoa] x2
Kasongo yo yo, mobali na ngai [Kasongo mume wangu]
Kasongo nga nawe oo
[Kasongo nina kufa]
Zonga libala ee
[Rudi kwenye ndoa]
[Chorus]
Nga na ndako Kasongo
[Nikiwa nyumbani, Kasongo]
Miso na nzela
[Kutwa kukodoa macho barabarani]
Soki okozonga dia ee
[Ikiwa utarudi]
Yebisa nga ye ee
[Nitaarifu Mpendwa]