Unavaa saa mkono gani?

Mimi huwa huwa navaa mkono wa kulia,maana mkono wa kushotovndio huwa nautumia kuandikia na kazi za mikono pia.
 
Japo umeweka angalizo kuwa sio lazima, lakini huu ndio ukweli wenyewe

Sent from my SM-J730F using JamiiForums mobile app
 
Mkono gani kuvaa saa inategemea na aina ya mkono mtu autumiao na wala si maamuz binafsi, japo wachache huamua tu wao binafsi. binafsi am left handed so navaa saa mkono wa kulia, na naona wengi wanaovaa sa kushoto ni wale ambao ni right handed!! ni hivyo tu yaani
 
Nimependa huu ifafanuzi,lakini ngoja nichangie.

Kuna ambao huvaa saa za chuma na kulegeza mkanda yaani saa inapwerepweta anaigeuza atakavyo(binafsi sipendi)haitulii pahala pamoja

Na mara nyingi hizi ni saa za chuma.
Watu wa aina hii kuepuka usumbufu wavae mkono ambao hauna harakati nyingi.

Kuna ambao huvaa saa hizo hizo za chuma au zingine za mipira, lakini mikanda yake mipana mno kiasi kwamba hata kuandika haandiki vizuri.

Mtu kama ana harakati nyingi za kuandika andika basi kuepusha usumbufu pia bora avae katika mkono ambao hatumii kufanyia shughuli zake.

Alafu kuna ambao huvaa saa za chuma lakini zimekamata vizuri mkononi kiasi kwamba hata ufanye harakati za kunyanyua mkono bado saa iko pale pale hawa wanaweza kuvaa katika mkono wao wa kulia kwa sababu saa haimsumbui wala kumtia uzito.


Lakini zipo saa za aina nyingi sana ambazo kwa watu wanaopenda kuvaa mkono wa kulia zipo saa nyingi tu ambazo haziwezi kuwasumbua endapo watavaa kwa mkono huo.

Saa mikanda membamba,nyepesi,inakaa vizuri mkononi,imebana vizuri japo sio sana,hizi saa zipo nyingi sana.

Lakini pia kuangalia kazi ya mtu ni muhimu sana.

Mfano kuna watu wao kazi yao kubwa ni kuandika ofisini labda wanatumia mkono wa kulia,mtu huyu pengine akaacha kuvaa mkono wa kulia kwa kudhani harakati nyingi zitaharibu saa yake,huyu anajinyima tu kwa sababu neno harakati linamtisha wakati hakuna harakati hiyo ya kutisha.

Neno harakati liangaliwe tena kwamba ni harakati zipi.

Kuandika ni harakati,kuuza bidhaa ni harakati,kubeba zege harakati,ukonda harakati n.k

Binafsi kitu kingine huwa ninachotizama ni urahisi wangu wa kuangalia saa naupata ukiwa mkono gani.

Mkono wa kulia nimezowea kuvaa saa na kufanyia vitu vingi hivyo hata nikivaa saa ni rahisi kwangu kuangalia saa luliko mkono wa kushoto.
 

hii ndio kanuni sahihi ya uvaaji saa na kwa kuongozea tu,saa zinatengenezwa kutokana na mkono unaoivaa.saa ya kuvaliwa na mtu wa mashoto(lefty) ambae ataivaa mkono wa kulia,ile knob yake ya kubadili majira huwa inawekwa tofauti na saa ya kuvaa mtu wa right.
 
Ila Sasa kuzipata hizi za sisi mashoto ndo ubahatishe
 
Umejibu kitaaluma kabsa. Asante.
 
Ila Sasa kuzipata hizi za sisi mashoto ndo ubahatishe

Kwa Tanzania itakuwa ni ngumu tu kuzipata sababu hata uelewa wa sababu ya mkono wa kuzivalia watu hawana.kama una mtu yuko nje ya Tanzania muagizie zipo nyingi tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…