Unawafahamu watu waliofanikiwa kwa kuwatoa kafara watu wao wa karibu?

Hamna kitu kama hicho. Ni fikra potofu.
 
Lisemwalo lipo! Hayo mambo yapo katika ulimwengu wa Giza!
Nadhani wenye taarifa kuhusu mambo hayo ni Mafundi yaani Waganga wa kienyeji.
 
I
Illusion
 
Eleza jinsi Kazi ya kuchekesha inavyowezesha kupata utajiri wa Kujenga ghorofa. Otherwise ni kuwekwa loop ya kutafutwa kwa siri (?) Kuelekea kwenye utapeli?,
 
Ndio maana watu wengi waliofanikiwa wapenda kuwa na mitaa yao kuishi kiutulivu peke yao, hiyo mitaa hauwezi kukuta uswahili swahili wa kijinga.

Mbona wengi wanamuomba na wanafanya kazi kwa bidii na uaminifu sana ila bado wanakufa wakiwa masikini??
Kuna ulazima gani haswa hadi Watu wote tuwe matajiri?

Ubinadamu ni kazi The humanity is work.
 
Thibitisha neno utajiri lipo kwa nyanja gani na kwanini tusimuamini huyo uliyemnukuu ila tukuamini wewe.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is work.
 
Utamu wa pesa uusotee si kupata pesa kirahisi rahisi tu, pia si wote tunaopenda maisha marahisi marahisi tu bila ya kuvuja jasho na damu.

Ubinadamu ni kazi/The humanity is work.
 
Thibitisha neno utajiri lipo kwa nyanja gani
Moja nyanja ya kuweza kumudu basic needs siku zote na wakati wote pasipo kuhitaji msaada.

Mbili, kuweza kumudu gharama za kupata social services siku zote na wakati wote pasipo kuhitaji msaada.

Sasa waafrika wengi hata kujigharamia tu basic needs zao za kila siku ni shida. Sababu ya umaskini wao.
na kwanini tusimuamini huyo uliyemnukuu
Kwa sababu hayupo na hajawahi kuwepo.
ila tukuamini wewe.
Sihitaji uniamini mimi.

Hakuna sehemu nimetaja, mtu aniamini.
Ubinadamu ni kazi/The humanity is work.
 
Ni story za watu wajinga na kama unavyojua watanganyika wengi bado akili zao zipo zama za ujima. Unakuta mtu na ndevu zake anaamini kuna watu wanapaa kwa ungo. Mtu kama huyo ni kumuacha tu maana bado yupo zama za ujima.

Mtu maskini ambae hajui jioni anakula wapi hawezi shindwa kumtoa ndugu yake kafara ili apate mali kama kweli kungekua na utajiri wa kafara.
 
Huo msimu huyo chatu alipokuja haukuwa msimu wa neema kwa wakulima wengi? Kuna miaka Tanzania wakulima nchi nzima au baadhi ya maeneo wengi wao wanazalisha sana na miaka mazao yanakuwa haba, inawezekana ujio wa chatu uligogana na msimu wa neema kwa wakulima wengi nyie mkafiriki chatu ndiye anasababisha mzalishe sana mazao na mifugo.

Swala la madini mtu akiwa anatumia vifaa vya teknolojia ya juu anajua hapa kuna madini kiasi fulani na hapa hakuna, mchawi hawezi kuweka madini sehemu yasiyokuwepo kama ambavyo hawezi kukuongezea pesa benki kwenye akaunti yako, inawezekana wachimbaji wadogo kwa sababu wanachimba madini kwa kubahatisha yalipo waganga wanapitia humo kucheza na psychology za bahati.

Pia wanyama au viumbe wengine huwa wana tabia ya kurudi na kudumu sehemu wanajihisi salama, hao chatu walikuwa wanakuja wanaona hakuna uadui wowote na binadamu ndio maana wakawa wanaendelea kurudi kila mara, hizi ni tabia za wanyama ndio maana huko nje watu wengi tu wanafuga nyoka wakiwemo chatu kama pets.
 
kwahiyo mama angekubali tusingekuwa na ephen_
 
hebu share usije ukavuka nalo, huyo namuona ona tu, ndio aliyekutoa kafara?
Hahaaaa hapana huyu mkuu jina lake nimelipenda, nataka niishi kwenye jina lake ...lol...mkuu tusiende mbali mimi kuweka reality yangu humu sitakaa kufanya hivyo, wanaonijua watakua wanajua naongelea masahibu gani...wasionijua basi bwana...
 
Hahaaaa hapana huyu mkuu jina lake nimelipenda, nataka niishi kwenye jina lake ...lol...mkuu tusiende mbali mimi kuweka reality yangu humu sitakaa kufanya hivyo, wanaonijua watakua wanajua naongelea masahibu gani...wasionijua basi bwana...
wengine hatukujui, hivyo hatutajua chochote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…