Unawakumbuka hawa wachezaji?

Kamgomoli

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2018
Posts
1,896
Reaction score
4,058
Sikumbuki vzr kama hawa wachezaji walikuwa ni wa Malindi au Mlandege ya Zanzibar, ila nakumbuka miaka ya 90s nikiwa mdogo nilikua nikisia balaa lao.

1. Victor Bambo (Shujaa)
2. Hassan Wembe
3. Amri Aziz
4. Muhidini Cheupe

Yaani japo ilikua ni Redioni ila walikua ni shida!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cheupe alikuwa Ndovu ya Arusha,Amri Aziz na Hasani Wembe Walikuwa Malindi..Bambo Mlandege...
 
Juma Bakari Kidishi, Innocent Haule,
Sent using Jamii Forums mobile app
 
V
Sesten Zakazaka njoo utupe ABC mana natumai unawajua hawa wachezaji.
Victor Bambo, Hassan Wembe na Amri Azizi ni Wazanzibari wakichezea vilabu vya Malindi na Miembeni vya kule Unguja. Walikua ni wachezaji wa wa kiwango cha kuridhisha

Muhidin Cheupe alichezea AFC ya Arusha wakati huo na yeye alikua vizuri pia Shadeeya
 
Ila wee jamaa Mungu akubariki sana.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Victor Bambo alicheza hata Yanga vizuri tu. Mmewasahau kina Rifat Said mlinda mlango nadhani alikipiga sana Malindi kama sikosei baadae Yanga, pia kuna Ali Bushiri huyu alikuwa mlinda mlango wa mlandege kama sikosei. Wapi Abert Sengo? Alikipiga hadi ujerumani sijui ligi daraja la pili au tatu vile?!
 
Ni kweli Rifat Said alichezea Yanga akiwa golikipa wa kutegemewa. Alikuja kupata mtihani wa ugonjwa wa macho na kupofuka kabisa. Hakuwahi kuona tena hadi mauti yalipomkuta. Mungu Amrehemu na amfanyie wepesi hesabu yake
 
Amour Azizi siyo Amri Azizi . Huyu alikuwa Malindi
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu vpi kuhusu Twaha Amidu alichezea vilabu gani? Nae nilikua namsikia sn enzi hizo
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…