Unawakumbuka nguli hawa wa soka?

hapa ndio ukisikia no comment ndio hiyo zetu azam tu siunajua tena wazaliwa wasiku hizi sijui kina kayuni sijui huyu nani huyu mwameja wala sina time nao sie zetu ngassa na kina bocco ndio baadae watakuwa kina Pazi, Mkwasa..
 


Kaka kwa kweli upo juu kuna huyo kwenye red jamaa alikuwa noumer...nadhani pia alikuwepo Juma Amir kama sikosei...David Mwakalebela hakuwa kwenye hicho kikosi kabla ya kwenda yanga? Kipa wao alikuwa anaitwa nani?
 
Nimemkumbuka Nteze John Lungu naye alikuwa kwenye hiki kikosi
 
Jamaa lichana nyavu mara kibao sijui nyavu zenyewe zilikuwa za kuunga unga au kweli kick ilikuwa kali mpaka ikachana
Gaga asingeedekeza pombe na msuba angelifika mbali.
 
kulikua na nyanda mmoja toka kanda ya ziwa KICHOCHI LEMBA[biashara shinyanga] duh alikua na mbwembwe sana langoni,kweli kila zama na enzi zake.
 
kulikua na nyanda mmoja toka kanda ya ziwa KICHOCHI LEMBA[biashara shinyanga] duh alikua na mbwembwe sana langoni,kweli kila zama na enzi zake.

Alikuwa RTC Kagera, akipiga kapelo kama alivyokuwa Manyika Petre wa Yanga.
 
Mavumbi Omari
Rafael Paul
İtutu Kigi
Abubakar Salum
 

Tunakumbuka ila ilikuwa 1979, baada ya vita ya Uganda. Simba ilikuwa; Mahadhi, Kajole, Daudi Salum, Filbert Rubibira, Husein Tindwa, Nico Njohole, George(Best) Kulagwa, Abass Kuka, Thuwein Ally, somebody Mabaso, labda na Kikwa sikumbuki. Mwaka ule pia Pan Africa walicheza kombe la washindi na AS Vita ya Zaire sasa DRC. Kassim Manara akafunga magoli mawili ya hali ya juu. Vita walifunga moja kupitia kwa LOFOMBO. Kwenda Zaire AS Vita wakafunga goli la utata wakapata faida ya goli la ugenini tulilalamika AFC na kudai mkanda uonyeshwe sijui nini tulishindwa. Pan ilikuwa Pondamali, Jaffar Abdurahman, Mohamed Mkweche, Leodgard Tenga, Jela Mtagwa, Mohamed Rishard(Adolph), Godian Mapango, Muhaji Muki, Kitwana Manara, Sunday Manara, Kassim Manara. Nafikiri hii ilikuwa rekodi ya wanafamilia watatu kucheza mechi moja ya kimataifa, Sunday akitokea USA kupitia KIA na kuingia uwanjani baada ya timu kukaguliwa. Hata hivyo, kitwana aliharibu akarudisha mpira uliokuwa unaenda wavuni kwa tick tak ya Kassim Manara vinginevyo Kassim angepiga hat trick. Mwaka uliofuata 1980 ndiyo tulifuzu fainali za afrika kupitia goli la Peter Tino.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…