Undava wa Nyosso: Haji Manara naye alalamika kusukumwa bila sababu baada mpira kumalizika

Undava wa Nyosso: Haji Manara naye alalamika kusukumwa bila sababu baada mpira kumalizika

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
f8dba4cf22af4bc3d4456e102334347e.jpg
Mkuu wa habari wa Simba Sports Club, Haji Manara, naye amelalamika kufanyiwa undava kwa kusukumwa na mchezaji wa Kagera Sugar Juma Nyosso bila sababu.

Manara kupitia ukurasa wake wa Instagram ameeleza kuwa;

"Lau ningekuwa mjinga ningeanza kugombana mimi na huyu mchezaji asiyejitambua, kanisukuma bila sababu baada ya game ila nikaona nikichachamaa washabiki wetu wangeweza kumdhuru..uzuri wake nilimwambia Kocha wake Mecky Maxime na nahodha Juma Kaseja kabla ya kwenda kumdhuru huyo mshabiki..Nyosso mimi sijatoka Buhelelo..Waangaishe maforeigners mjini.. huo undava na uselamavi mimi nishavuka huko", aliandika Haji Manara.
 
Hivi huyu Nyosso si ndio kipindi fulani alipata kumchomeka vidole mchezaji mwenzie uwanjani? Anavuta mabangi au?

Au ni Nyosso mwingine?

Kwanini asifungiwe kabisa maisha yake yote?
 
Huyu jamaa akili yake siyo nzuri. Nadhani mpira si sehemu yake
 
Hivi huyu Nyosso si ndio kipindi fulani alipata kumchomeka vidole mchezaji mwenzie uwanjani? Anavuta mabangi au?

Au ni Nyosso mwingine?

Kwanini asifungiwe kabisa maisha yake yote?
Ndo yeye. bila shaka kifungo cha maisha cha soka kinamhusu
 
Huyo mshabiki alifuata nini kwa kiwanja? Sheria inamruhusu kuingia kwa kiwanja? Mshabiki kataka mwenyewe kuzimia
 
Huyu Nyoso ameshindwa kujua kuwa hawa wote akiwepo na Manara walikuwa wakimtafuta kitambo sana kwa kitendo cha kumdhalilisha nahodha wao? Manara alimchokoza Nyoso kwa vimaneno vya kejeli basi yeye badala ya kunyamaza akaingia mkenge na kuiruhusu bangi ifanye kazi badala ya akili, sasa yatakayomkuta itakuwa majuto makubwa kwake akiwaacha walimkejeli wakimcheka na asijue cha kuwafanya.
 
Daah huyu nyoso huyu.
Kama vipi stengeneze brand kama ya 900 itapendeza maana matukio yake si ya mchezo[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Manara alimchokoza Nyoso kwa vimaneno vya kejeli basi yeye badala ya kunyamaza akaingia mkenge na kuiruhusu bangi ifanye kazi badala ya akili, sasa yatakayomkuta itakuwa majuto makubwa kwake akiwaacha walimkejeli wakimcheka na asijue cha kuwafanya.

Kwa hivyo ulikuwa ni mtego ambao Nyosso hakung'amua chochote, basi akili yake imefichwa mbali sana
 
Namhurumia nyoso

I naweza kuwa amezungukwa na watu wabaya ndo maana

Nyoso ubabe hauna mana km unataka mafanikio
 
f8dba4cf22af4bc3d4456e102334347e.jpg
Mkuu wa habari wa Simba Sports Club, Haji Manara, naye amelalamika kufanyiwa undava kwa kusukumwa na mchezaji wa Kagera Sugar Juma Nyosso bila sababu.

Manara kupitia ukurasa wake wa Instagram ameeleza;

"Lau ningekuwa mjinga ningeanza kugombana mimi na huyu mchezaji asiyejitambua, kanisukuma bila sababu baada ya game ila nikaona nikichachamaa washabiki wetu wangeweza kumdhuru.. Uzuri wake nilimwambia Kocha wake Mecky Maxime na nahodha Juma Kaseja kabla ya kwenda kumdhuru huyo mshabiki. Nyosso mimi sijatoka Buhelelo.. Waangaishe maforeigners mjini.. huo undava na uselamavi mimi nishavuka huko", aliandika Haji Manara.

Sikujua kama kumbe Afisa Habari wa Taasisi au Klabu Kubwa kama ya Simba anaweza akaongea na hadi kuyaandika hayo maneno ya Kihuni na ' hovyo hovyo '. Taasisi ya Simba inaharibiwa na huu Uhuni wa Msemaji wake Haji Manara na nadhani ifike muda sasa Simba nao wafanye maamuzi magumu kama ya Yanga kwa kumtafuta Afisa Habari / Msemaji mwenye nidhamu na kujitambua. Anachokifanya Haji Manara ni kinyume kabisa na Taaluma nzima ya Public Relations na anaiabisha pia.
 
Mimi nampa pole uyo shabiki aliyrzimia ..ila kiukweli Juma Nyoso yuko vizur kiafya nakimwil..Yaani uyo shabiki kapigwa ngumi moja imemfanya kuzimia ...Mimi nawaomba watu msio na lishe muahache kujichanganya na watu walioshiba kama Nyoso..
Shabiki amekura mshahara wake..nafikil akizinduka ataacha uwo ujinga wakuzarau watu waliomtangulia mjini..haaaaaaaaa [HASHTAG]#NyosoWewe[/HASHTAG].
 
Jamaa anastress za maisha, nafikir ubondia unamfaa ila pia nidham inahitajika yasijemkuta km tyson ubondia hadi nje ya ulingo
 
Duh! Buselela ni wapi na huo Uselamavi Manara ashapitia kumbe. [emoji35]
 
Huyo mshabiki alifuata nini kwa kiwanja? Sheria inamruhusu kuingia kwa kiwanja? Mshabiki kataka mwenyewe kuzimia
Mpira ulishakwisha, sil wakati wa mpira, na ni pembeni mwa uwanja.
 
Haji nae kafikishwa Mafinga Mufindi na Nyosso analeta fasihi zake istagram
 
Hivi huyu Nyosso si ndio kipindi fulani alipata kumchomeka vidole mchezaji mwenzie uwanjani? Anavuta mabangi au?

Au ni Nyosso mwingine?

Kwanini asifungiwe kabisa maisha yake yote?
Umeuliza tatizo ni nini au unatokwa povu tu,,Nyoso si chizi ampige mtu bila sababu
 
Back
Top Bottom