GuDume
JF-Expert Member
- Jan 18, 2015
- 6,651
- 14,337
Tamer El-Noury ni jina lake kamili akiwa ni FBI muislamu ambaye alipewa jukumu la kuingia ndani ya makundi ya kigaidi yenye msimamo mkali na kushirikiana nao katika kupanga mashambulizi dhidi ya Marekani. Huyu alihusika kwa kiasi kikubwa kabisa katika kupanga mashambulizi huko new York ambako walitakiwa kuiondoa train kwenye reli ili isababishe uharibifu na vifo vingi miaka minne iliyopita.
Aliamua kuandika kitabu akitaka waamerika wafahamu kazi yake akiitumikia nchi yake kama Muislamu ndani ya FBI. Anaelezea magaidi ni watu wa namna gani katika mahojiano yake na BBC.
“Kiukweli magaidi ni watu ambao katika maisha wanakuwa wameshakata tamaa. Ni watuwasio jielewa wasioelewa wataishi vipi. Hawa huchukuliwa na kufundishwa chuki, hupandikizwa chuki ambao inahusishwa na dini , Imani. Hapa kwa kupandikiziwa haya huwafanya wajione sasa wamepata tumaini,wamepata uelekeo”
Anaendelea kusema “mimi ni Muislamu na pia ni Mwamerika na nina fadhaishwa na haya yanayofanywa na hawa wanyama kwa nchi yangu na kuidhalilisha pia dini yangu”
FBI waliona wana upungufu kiasi flan cha watu wanaoweza kuzungumza kiarabu. Kwa namna utendaji kazi wa FBI ulivyo una departments nyingi na kila aina ya watu. Kuna walimu,kuna madaktari,kuna wanasheria,kuna wanajeshi,kuna polisi,kuna kila kada ambayo inahitajika hapa duniani ambayo wanajua wanaweza hitaji mtu wa namna hiyo katika operations zao mbalimbali hapa duniani. Hivyo hata wale ambao kuna wakati inabidi wajifanye vichaa, ombaomba, wapiga debe n.k kila sehemu kila aina ya mtu. Huko kote watu huwa wamejifunza lugha husika kwa kiwango cha juu sana. Hulelewa katika kujifunza kazi za FBI wengine toka wakiwa wadogo. Hivyo kila mara hujiangalia wanahitaji kuboresha kada gani katika vitengo vyao mbalimbali. Kumbuka walipoenda kumpeleleza Osama kuna walioenda kipindi cha upelelezi huko Pakistani kama madaktari wa chanjo wakizungumza kiarabu kizuri kabisa.
Bwana EL- Noury ni motto wa Mhamiaji wa Kiarabu kutoka Misri. Ambaye alijiunga na jeshi la polisi huko New Jersey. Ambako alikuwa akifanya kazi kubwa ya kuyavunja makundi yanayojihusisha na madawa ya kulevya. Kipindi chote hicho FBI walikuwa wakimsoma,wakimfuatilia kwa ukaribu na mwishowe waliamua ku mchukua baada ya kugundua wamepungukiwa na wafanyakazi wanaozungumza kiarabu.
Katika shughuli zake hizo akiwa kama undercover alikuwa amepewa jukumu la kuua watu wengi kadri awezavyo katika jaribio flan la kigaidi ambalo lilihusisha kuiangusha train ya umeme kutoka New York kwenda Toronto. Na hii ni kwa vile magaidi wenyewe walikuwa wakiamini kuwa huyu jamaa ni mtu wao mmoja ya watu wenye chuki na USA. Alijiunga kupitia urafiki wake wa karibu na Raia wa Tunisia Chiheb Esseghaier ambaye alikuwa mmoja ya wahusika wakuu katika jaribio hilo la Kigaidi. unaweza soma zaidi habari zake na namna ambavyo alikamatwa kutokana na intelejensia iliyofanyika ikisaidiwa na El-Noury kwa kiwango kikubwa.
Kutokana na urafiki ambao alikuwa amejitengenezea na Esseghaier basi naye akawekwa kuwa mmoja ya wahusika wa jaribio hilo la hatari. Yeye alikuwa akionekana kama ni Ni Mmarekani mwenye asili ya kiarabu tajiri. Ambaye alikuwa na chuki kubwa sana kwa Wamarekani. Na hii ndiyo ilikuwa gear yake ya kuingilia katika hilo kundi la kigaidi. Anasema alikuwa na wakati mgumu . maana alitakiwa hasa ajengeke kuwa ni mtu wa namna hiyo kwa kipindi chote yupo na lile kundi. Alijitahidi sana kuendana na ukweli wa kile ambacho alikuwa amewaambia.
Hivyo hadith zake zote, kila ambacho alisema kilipaswa kiwe kina uhalisia kulingana na aliyokuwa kiwaambia. Anasema “unaposafiri dunia nzima na kundi la magaidi wenye msimamo mkali ukimaliza siku,wiki na miezi pamoja nao inabidi uwe kama wao. Ama sivyo uhalisia wako utaonekana maana upo chini ya ngozi yao.hivyo inabidi u copy na maisha yao na kile unachokisema”
Unapaswa kuwafanya wakuamini, waone wewe ni mwenzao maana kinyume na hapo ni kuhatarisha maisha yako .lilikuwa ni suala la kufumba na kufumbua wao wakijua kuwa si mwenzao unauawa kwa mateso makali sana. Hivyo ni kama umeiweka roho yako rehani.
"Kazi yangu ilikuwa ni kuwa karibu sana na wale watu wabaya.wale watu makatili wenye kupanga na kutenda mambo ya kinyama. Nilipaswa kuwasikiliza na pia kuwafuatilia kwa ukaribu sana jinsi wanavyozungumzia familia zao, mama zao, ndugu zao n.k"
Wakiwa katika safari ya kwenda New York Esseghaier alianza kupanga nao mipango ya shambulio lijalo eneo la Times Square huko New York wakati wa sherehe za Krismas na mwaka mpya. Wakiwa katika safari hiyo hiyo wakatembelea Twin Tower ilipotokea shambulio la 9/11. Anasema wakiwa katika eneo hilo Esseghaier alisema” Marekani inahitaji September 11 nyingine tena” kauli hii ilimshtua sana El- Noury na anasema ilikuwa kidogo ajiumbue kutokana na ule mshtuko na mchango wake katika matamshi hayo.
Anasema bahati nzuri mipangao hiyo haikufanikiwa sababu Esseghaier na Raed Jaser na mpalestina mmoja aliyekuwa akiishi Canada walikamatwa mwaka 2013 na kuhukumiwa kifungo cha maisha mwaka 2015 kupitia upelelezi uliofanywa na El-Noury.
Mahojiano yaliyofanyika kuhusiana na story hii ya El-Noury yalitoa mwangaza mkubwa sana kuhusiana na nini kina fanyika katika ulimwengu wa giza wa kikaidi akiwa kama undercover.FBI walisisitiza kuwa mahojiano hayo yafanyike kwa njia ya simu huku wakifuatilia kwa ukaribu ili kuhakikisha kuwa wanaendelea kumlinda mtu wao.
Kwa mengi ambayo aliyaelezea ni bora ukisoma kitabu cha Ameican Radical Inside the world of an Undecover Muslim FBI Agent.
WITO WANGU : "TUILINDE NCHI YETU DHIDI YA WATU WOTE WENYE NIA MBAYA NAYO"
Aliamua kuandika kitabu akitaka waamerika wafahamu kazi yake akiitumikia nchi yake kama Muislamu ndani ya FBI. Anaelezea magaidi ni watu wa namna gani katika mahojiano yake na BBC.
“Kiukweli magaidi ni watu ambao katika maisha wanakuwa wameshakata tamaa. Ni watuwasio jielewa wasioelewa wataishi vipi. Hawa huchukuliwa na kufundishwa chuki, hupandikizwa chuki ambao inahusishwa na dini , Imani. Hapa kwa kupandikiziwa haya huwafanya wajione sasa wamepata tumaini,wamepata uelekeo”
Anaendelea kusema “mimi ni Muislamu na pia ni Mwamerika na nina fadhaishwa na haya yanayofanywa na hawa wanyama kwa nchi yangu na kuidhalilisha pia dini yangu”
FBI waliona wana upungufu kiasi flan cha watu wanaoweza kuzungumza kiarabu. Kwa namna utendaji kazi wa FBI ulivyo una departments nyingi na kila aina ya watu. Kuna walimu,kuna madaktari,kuna wanasheria,kuna wanajeshi,kuna polisi,kuna kila kada ambayo inahitajika hapa duniani ambayo wanajua wanaweza hitaji mtu wa namna hiyo katika operations zao mbalimbali hapa duniani. Hivyo hata wale ambao kuna wakati inabidi wajifanye vichaa, ombaomba, wapiga debe n.k kila sehemu kila aina ya mtu. Huko kote watu huwa wamejifunza lugha husika kwa kiwango cha juu sana. Hulelewa katika kujifunza kazi za FBI wengine toka wakiwa wadogo. Hivyo kila mara hujiangalia wanahitaji kuboresha kada gani katika vitengo vyao mbalimbali. Kumbuka walipoenda kumpeleleza Osama kuna walioenda kipindi cha upelelezi huko Pakistani kama madaktari wa chanjo wakizungumza kiarabu kizuri kabisa.
Bwana EL- Noury ni motto wa Mhamiaji wa Kiarabu kutoka Misri. Ambaye alijiunga na jeshi la polisi huko New Jersey. Ambako alikuwa akifanya kazi kubwa ya kuyavunja makundi yanayojihusisha na madawa ya kulevya. Kipindi chote hicho FBI walikuwa wakimsoma,wakimfuatilia kwa ukaribu na mwishowe waliamua ku mchukua baada ya kugundua wamepungukiwa na wafanyakazi wanaozungumza kiarabu.
Katika shughuli zake hizo akiwa kama undercover alikuwa amepewa jukumu la kuua watu wengi kadri awezavyo katika jaribio flan la kigaidi ambalo lilihusisha kuiangusha train ya umeme kutoka New York kwenda Toronto. Na hii ni kwa vile magaidi wenyewe walikuwa wakiamini kuwa huyu jamaa ni mtu wao mmoja ya watu wenye chuki na USA. Alijiunga kupitia urafiki wake wa karibu na Raia wa Tunisia Chiheb Esseghaier ambaye alikuwa mmoja ya wahusika wakuu katika jaribio hilo la Kigaidi. unaweza soma zaidi habari zake na namna ambavyo alikamatwa kutokana na intelejensia iliyofanyika ikisaidiwa na El-Noury kwa kiwango kikubwa.
Kutokana na urafiki ambao alikuwa amejitengenezea na Esseghaier basi naye akawekwa kuwa mmoja ya wahusika wa jaribio hilo la hatari. Yeye alikuwa akionekana kama ni Ni Mmarekani mwenye asili ya kiarabu tajiri. Ambaye alikuwa na chuki kubwa sana kwa Wamarekani. Na hii ndiyo ilikuwa gear yake ya kuingilia katika hilo kundi la kigaidi. Anasema alikuwa na wakati mgumu . maana alitakiwa hasa ajengeke kuwa ni mtu wa namna hiyo kwa kipindi chote yupo na lile kundi. Alijitahidi sana kuendana na ukweli wa kile ambacho alikuwa amewaambia.
Hivyo hadith zake zote, kila ambacho alisema kilipaswa kiwe kina uhalisia kulingana na aliyokuwa kiwaambia. Anasema “unaposafiri dunia nzima na kundi la magaidi wenye msimamo mkali ukimaliza siku,wiki na miezi pamoja nao inabidi uwe kama wao. Ama sivyo uhalisia wako utaonekana maana upo chini ya ngozi yao.hivyo inabidi u copy na maisha yao na kile unachokisema”
Unapaswa kuwafanya wakuamini, waone wewe ni mwenzao maana kinyume na hapo ni kuhatarisha maisha yako .lilikuwa ni suala la kufumba na kufumbua wao wakijua kuwa si mwenzao unauawa kwa mateso makali sana. Hivyo ni kama umeiweka roho yako rehani.
"Kazi yangu ilikuwa ni kuwa karibu sana na wale watu wabaya.wale watu makatili wenye kupanga na kutenda mambo ya kinyama. Nilipaswa kuwasikiliza na pia kuwafuatilia kwa ukaribu sana jinsi wanavyozungumzia familia zao, mama zao, ndugu zao n.k"
Wakiwa katika safari ya kwenda New York Esseghaier alianza kupanga nao mipango ya shambulio lijalo eneo la Times Square huko New York wakati wa sherehe za Krismas na mwaka mpya. Wakiwa katika safari hiyo hiyo wakatembelea Twin Tower ilipotokea shambulio la 9/11. Anasema wakiwa katika eneo hilo Esseghaier alisema” Marekani inahitaji September 11 nyingine tena” kauli hii ilimshtua sana El- Noury na anasema ilikuwa kidogo ajiumbue kutokana na ule mshtuko na mchango wake katika matamshi hayo.
Anasema bahati nzuri mipangao hiyo haikufanikiwa sababu Esseghaier na Raed Jaser na mpalestina mmoja aliyekuwa akiishi Canada walikamatwa mwaka 2013 na kuhukumiwa kifungo cha maisha mwaka 2015 kupitia upelelezi uliofanywa na El-Noury.
Mahojiano yaliyofanyika kuhusiana na story hii ya El-Noury yalitoa mwangaza mkubwa sana kuhusiana na nini kina fanyika katika ulimwengu wa giza wa kikaidi akiwa kama undercover.FBI walisisitiza kuwa mahojiano hayo yafanyike kwa njia ya simu huku wakifuatilia kwa ukaribu ili kuhakikisha kuwa wanaendelea kumlinda mtu wao.
Kwa mengi ambayo aliyaelezea ni bora ukisoma kitabu cha Ameican Radical Inside the world of an Undecover Muslim FBI Agent.
WITO WANGU : "TUILINDE NCHI YETU DHIDI YA WATU WOTE WENYE NIA MBAYA NAYO"