Ungekuwa wewe ungefanyaje?

Under-cover

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2023
Posts
1,834
Reaction score
3,042
Wakuu habari,
Em fikiria mko katika shule fulani ivi mkiwa mnajiandaa na mtihani kama testi kesho asubuhi saa 12 asubuhi, wewe na rafiki zako wa wili jumla mko watatu usiku mkapanga kutoroka kwenda disco ila mkakubaliana kuwa alfajiri mapema mtawahi kurudi.

Kweli usiku ukafika mkaruka ukuta hao kwenda disco, mkacheza wee mpaka alfajiri kukaribia kukucha, ndio mkajikusanya kurudi shule, ile mnapanda ukuta na kuruka ndani mara paa
walinzi hao wana waona kisha wanawakamata.

Then wanasubiri pakuche walimu waje wawakabidhi, walimu wanafika, walinzi kama kawaida wanapepeta mdomo pale nyie hoi, mwalimu fulani mwenye somo lake kwaajili ya test anawakataa msiingie makusudi, huku akisema jiandaeni kwa test nyingne wiki inayofuata huku huo msala ukafika kwa mkuu wa shule.

Basi baadae kidgo mkaitwa na mkuu wa shule na kuwauliza, mlikwenda wapi , mmoja wenu akajibu tulikuwa msibani,ndio nanyinyi mkadakia kweli tulikuwa msibani.

Basi mkaachwa , ikafika hio wiki ya mtihani, na mkatenganishwa madarasa, na kupewa tahadhari kuwa hakikisheni majibu yanakuwa sawa, mkitofautiaana basi shule ndio hamna tena, mkashituka, mkapewa mtihani/test

1. Nani aliyefariki?
2. Msiba upo wapi?
3. Na atazikwa lini na wapi?

NB hapa mkiwa madarasa tofauti...

Pia soma:My true story; Jinsi uongozi wangu shuleni ulivyonifanya niishi maisha ya upweke
 
Hakuna Cha kufanya
Kwenye maisha Kuna kanuni Moja ya uongo nayo ni hii
"Unaposema uongo Sasa hivi jua baadae utasema uongo tena ili kuulinda huu uongo uliosema na hali hiyo itaendelea hadi pale utakapojulikana kuwa wewe ni muongo"
Sema kweli Kisha acha mtu aamue
 
Back
Top Bottom