DOKEZO Unguja: Wagonjwa tunakosa Haki ya Faragha wakati wa kuonana na Daktari katika Hospitali ya Wilaya ya Magharibi, tunawekwa chumba kimoja

DOKEZO Unguja: Wagonjwa tunakosa Haki ya Faragha wakati wa kuonana na Daktari katika Hospitali ya Wilaya ya Magharibi, tunawekwa chumba kimoja

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Mimi ni Mwananchi ambaye nimekuwa nikipata huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Magharibi, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja (Hospitali ya Ijitimai) kuna kero ambayo imekuwa ikinisumbua muda mrefu na ninaamini inasumbua watu wengi pia.

Nimekuwa nikifika kituoni hapo kupata huduma ya Ugonjwa wa Sukari (Diabetes), changamoto iliyopo hospitalini hap oni kuwa hakuna usiri kwa Wagonjwa, unakuna muda mwingi tunawekwa katika chumba kimoja hadi wagonjwa Watano.

Unakuta wote watano au zaidi ya mmoja mpo kwa Daktari mkitakiwa kueleza shida ya kila mtu binafsi, sasa haki ya faragha iko wapi hapo?

Kinachotokea unakuta wengi wetu tunabakaki na dukuduku, tunashindwa kuwa na uhuru wa kuzungumza, hilo jambo siyo zuri kabisa.

Tunaomba kama Madaktari hawawezi kutuweka katika vyumba tofauti au kutusikiliza mmoja mmoja basi itafutwe njia nyingine mbadala badala ya hiki kinachoendelea ambacho kinatuumiza wengi.
 
Mimi ni Mwananchi ambaye nimekuwa nikipata huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Magharibi, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja (Hospitali ya Ijitimai) kuna kero ambayo imekuwa ikinisumbua muda mrefu na ninaamini inasumbua watu wengi pia.

Nimekuwa nikifika kituoni hapo kupata huduma ya Ugonjwa wa Sukari (Diabetes), changamoto iliyopo hospitalini hap oni kuwa hakuna usiri kwa Wagonjwa, unakuna muda mwingi tunawekwa katika chumba kimoja hadi wagonjwa Watano.

Unakuta wote watano au zaidi ya mmoja mpo kwa Daktari mkitakiwa kueleza shida ya kila mtu binafsi, sasa haki ya faragha iko wapi hapo?

Kinachotokea unakuta wengi wetu tunabakaki na dukuduku, tunashindwa kuwa na uhuru wa kuzungumza, hilo jambo siyo zuri kabisa.

Tunaomba kama Madaktari hawawezi kutuweka katika vyumba tofauti au kutusikiliza mmoja mmoja basi itafutwe njia nyingine mbadala badala ya hiki kinachoendelea ambacho kinatuumiza wengi.
Sasa mkuu kuelezea ugonjwa wa diabetes unahitaji faragha gani kweli? Ingekua diagonasis ya kwanza ya kuelezea dalili za huo ugonjwa hapa faragha inahitajika, kumbuka kuna uhaba wa madakitari na vyumba nyie mna bahati mna pata dakitari kuna watu mikoani hata huyu dakitari kumuona ni shida.
 
Pole sana mkuu, hospital zetu nyingi kwenye swala la huduma bado kuna kusua sua. Jaribu kuongea na daktari pembeni umueleze pengine ataangalia namna ya ku deal na tatizo lako
 
inamana hiyo hosptal haina sehemu ya kupumzika mbele ya chumba cha daktari ukiwa unasubiri mwito wa next?
 
Sasa mkuu kuelezea ugonjwa wa diabetes unahitaji faragha gani kweli? Ingekua diagonasis ya kwanza ya kuelezea dalili za huo ugonjwa hapa faragha inahitajika, kumbuka kuna uhaba wa madakitari na vyumba nyie mna bahati mna pata dakitari kuna watu mikoani hata huyu dakitari kumuona ni shida.
Anashindwa kusema kuw hata game siku hizi hapigi fresh mkuu. kisukari ina mambo mengi kama inawezekana wawape tu faragha maana amgonjwa huambatana na mengi ambayo kimsingi unaweza uone jau kuyasema mbele ya kadamnasi.
 
Anashindwa kusema kuw hata game siku hizi hapigi fresh mkuu. kisukari ina mambo mengi kama inawezekana wawape tu faragha maana amgonjwa huambatana na mengi ambayo kimsingi unaweza uone jau kuyasema mbele ya kadamnasi.
Yote haya yanajulikana na huo ugonjwa wa kisukàli na dakitari hana jinsi zaidi ya kumpa dawa apone kwanza game atapiga tu badaye kupewa huruma na dakitari haisaidii kabisa huruma sia tiba.
 
Sasa mkuu kuelezea ugonjwa wa diabetes unahitaji faragha gani kweli? Ingekua diagonasis ya kwanza ya kuelezea dalili za huo ugonjwa hapa faragha inahitajika, kumbuka kuna uhaba wa madakitari na vyumba nyie mna bahati mna pata dakitari kuna watu mikoani hata huyu dakitari kumuona ni shida.
Mkuu
Proffesionalism and ethics inasema hivyo unavyowaza?

Wekeni utaratibu vizuri. Sio sawa.
 
Mimi ni Mwananchi ambaye nimekuwa nikipata huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Magharibi, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja (Hospitali ya Ijitimai) kuna kero ambayo imekuwa ikinisumbua muda mrefu na ninaamini inasumbua watu wengi pia.

Nimekuwa nikifika kituoni hapo kupata huduma ya Ugonjwa wa Sukari (Diabetes), changamoto iliyopo hospitalini hap oni kuwa hakuna usiri kwa Wagonjwa, unakuna muda mwingi tunawekwa katika chumba kimoja hadi wagonjwa Watano.

Unakuta wote watano au zaidi ya mmoja mpo kwa Daktari mkitakiwa kueleza shida ya kila mtu binafsi, sasa haki ya faragha iko wapi hapo?

Kinachotokea unakuta wengi wetu tunabakaki na dukuduku, tunashindwa kuwa na uhuru wa kuzungumza, hilo jambo siyo zuri kabisa.

Tunaomba kama Madaktari hawawezi kutuweka katika vyumba tofauti au kutusikiliza mmoja mmoja basi itafutwe njia nyingine mbadala badala ya hiki kinachoendelea ambacho kinatuumiza wengi.
Yaani unataka kuniambia uongozi wa hospitali unashindwa kuwapanga wagonjwa foleni akawa anaingia mmoja baada ya mwingine? Samia mitano tena!
 
Hiyo ni mbaya sana.Hapo huwezi kuelezea Kwa uhuru maana wenzako wanakuwa wanakusikiliza mazungumzo Yako.Hiyo hospitali hajitambui na haisimamii miongozo ya kazi yao
 
Yote haya yanajulikana na huo ugonjwa wa kisukàli na dakitari hana jinsi zaidi ya kumpa dawa apone kwanza game atapiga tu badaye kupewa huruma na dakitari haisaidii kabisa huruma sia tiba.
Tiba inaanzia kuchwani mkuu... Ndiyo maana mgonjwa akimwona daktari kuna wakati anajihisi ahueni. Inapaswa mgonjwa awe na imani na hiyo tiba na yule anayemtibu pia. Ndiyo maana viongozi wetu mara nyingi hawatibiwi hospitali zetu kwa sababu hawana imani na wanaotibu na tiba zilizo hapo, sema wao wana uwezo wa kugharamiwa kutibiwa kwingine.
Anyway bado miundombinu hairuhusu jamaa avumilie tu mpaka 2050.
 
Mkuu
Proffesionalism and ethics inasema hivyo unavyowaza?

Wekeni utaratibu vizuri. Sio sawa.
Mkuu necessity au emergence does not respect ethics and professionalism ndo mama mjamzito anaweza kajifungulia kwenye corridor ya hospitali na dakitari akamsaidia hapo hapo bila kuzingatia ethics na professionalism za kazi hiyo
 
inamana hiyo hosptal haina sehemu ya kupumzika mbele ya chumba cha daktari ukiwa unasubiri mwito wa next?
Inaonekana wagonjwa au wazanzibar hawawaamini madakitari maana ukimuacha dakitari mwanaume amuudumie mgonjwa mwanamke wakiwa faragha wanapelekeana moto! Wazanzibari bwaanah😛😍😍
 
Tiba inaanzia kuchwani mkuu... Ndiyo maana mgonjwa akimwona daktari kuna wakati anajihisi ahueni. Inapaswa mgonjwa awe na imani na hiyo tiba na yule anayemtibu pia. Ndiyo maana viongozi wetu mara nyingi hawatibiwi hospitali zetu kwa sababu hawana imani na wanaotibu na tiba zilizo hapo, sema wao wana uwezo wa kugharamiwa kutibiwa kwingine.
Anyway bado miundombinu hairuhusu jamaa avumilie tu mpaka 2050.
Ni kweli Imani katika kutibiwa ni Tiba pia, ndo maana mpaka leo walokole wanatibu wagonjwa wa diabetes na saratani na wagonjwa wanatowa ushuhuda kwamba wamepona, kumbe wamepata afueni tu physically ugonjwa uko pale pale.
 
Mkuu necessity au emergence does not respect ethics and professionalism ndo mama mjamzito anaweza kajifungulia kwenye corridor ya hospitali na dakitari akamsaidia hapo hapo bila kuzingatia ethics na professionalism za kazi hiyo
Sasa hiyo ni emergence au uvivu na kutojali kwa madaktari wa hicho kituo??
Hiyo sio sawa, watu wazima wake kwa waume wasikilizane maswaibu yao, wengine wataona hata kuyasema badala yake wataficha ficha wapewe dawa sizo. Sio wote wana ujasiri wa kueleza shida mbele za watu.
 
Mkuu necessity au emergence does not respect ethics and professionalism ndo mama mjamzito anaweza kajifungulia kwenye corridor ya hospitali na dakitari akamsaidia hapo hapo bila kuzingatia ethics na professionalism za kazi hiyo
Sawa nakubali ila wawawekee utaratibu vizuri isibaki ndo mazoea .....hata kama vyumba vichache basi Hata kutenganisha na mapazia ya kijani sidhani kama inashindikana kabisa mkuu......

hata nikiwa Mimi,Nina kaugonjwa kengine kangozi mfano nashindwa kumuonesha Daktar kutokana na watu wananiangalia .......

Privacy inabaki kua ni muhimu mno ....naamini bado Kuna kitu wanaweza fanya ikiwemo hata walau hiyo ya mapazia .
 
Back
Top Bottom