Unyang'anyi wa ardhi tishio kwa wakulima wadogo wadogo Tanzania

Unyang'anyi wa ardhi tishio kwa wakulima wadogo wadogo Tanzania

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
IMG_20210331_124443_895.jpg

Takriban asilimia 80 ya ardhi inayotumiwa kwa kilimo Tanzania inatumiwa na wakulima wadogo wadogo wanaolima kwa ajili ya chakula.

Wakulima katika maeneo mengi ya Tanzania wanakumbana na changamoto kubwa ya unyang'anyi wa ardhi kwa ajili ya uwekezaji hasa wa watu binafsi hali inayowalazimu kukosa maeneo ya kutosha kuendesha shughuli zao ili kumudu gharama za maisha.

Aidha changamoto nyingine zinazowakabili ni ukosefu wa pembejeo pamoja na kukosa taarifa muhimu kuhusu kilimo hasa mabadiliko ya tabia ya nchi.

Jamii za Wamasai ndizo hukumbwa na unyang'anyi wa ardhi sana Tanzania. Wengi wao huishi maeneo ya hifadhi hivyo hunyang'anywa ardhi kwa ajili ya kupanua maeneo hayo ili Serikali iingize kipato zaidi kupitia utalii.

Mwaka 2017 Wamasai walifukuzwa kwenye hifadhi ya Serengeti hali iliyopelekea kukosa makazi pamoja na malisho ya mifugo yao.
 
Upvote 0
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom