ginyisi
JF-Expert Member
- Apr 6, 2023
- 287
- 465
Habari wakuu
Niende moja kwa moja kwenye mada...nimekutana na kijana mmoja akawa ananisimulia kuhusu unyanyasaji anaopitia mwanamke hyu kutoka familia za kijijini ukweli inasikitisha sana, kisa hichi kimenifanya niamini kuwa huko vijijini kuna wanawake wanaopitia mateso na manyanyaso kama haya...ni hivi.......
Mzee ni mtata kweli kweli yaani hazuiliki kwa yeyote katika maamuzi yake hali ambayo humfanya awe huru kumpiga mke wake atakavyo na hakuna wa kuingilia hata mamake mzazi hamsikilizi...ilifikia wakati huyu mama alitakaga kujinyonga lakini hakufanikiwa ndipo ndugu zake wakaingilia kati na kwenda kumshitaki serikali ya mtaa....
Alivoitwa yule mzee alikuwa mpole na kuomba radhi ili mambo yasiwe mengi....wakakubaliana aandike barua ya kukiri kutompiga tena na akirudia watamchukulia hatua kali zaidi.....basi wakatoa nakala moja ikaenda upande wa ndugu mwanamke na nyingine ikabaki serikali ya mtaa na nyingine wakabaki nayo....lengo ni kutafuta amani....
Lakini haikufanikiwa kwani baada ya mda mzee hyu alianza kumshinikiza mwanamke bila kuzileta barua hizo zote hakutakuwa na amani kwenye nyumba ile.... na kweli mwanamke akakubali kwenda kuchukua nakala zote na kumkabidhi mzee yule akiwa na imani ndio njia sahihi ya kuileta amani lakini hii ndo ilikuwa sawa na kujichumia fimbo.....
Mzee alipambana kurudisha uhuru wake na akafanikiwa na akaendelea kumpiga kila kosa ni mkanda mashine unatembea/kumpiga mbele ya watoto mpaka anajisaidia mbele ya watoto mzee hakuwa na huruma ata kidogo kumpiga kumchania nguo kumburuza yaani ni vitu vya ajabu Mara vitisho vya kumuua na kumwambia ikiwa utanishtaki popote basi nitakimbia na kukuachia watoto peke yake na ataenda kumloga awe chizi.
Huyu mama alishawahi kuondoka lakini alirudi kwa ajili ya watoto na mwanamke hawezi tena kuondoka kwa sababu anawapenda sana watoto wake anasema bora afe katikat ya watoto wake....huyu mama amekuwa ni mtu wa kulia kila kukicha kutokana na anachofanyiwa na mume wake.......
Ushauri wako utasaidia sana kumuokoa mwanamke huyu kwenye manyanyaso haya...ahsanten.
Niende moja kwa moja kwenye mada...nimekutana na kijana mmoja akawa ananisimulia kuhusu unyanyasaji anaopitia mwanamke hyu kutoka familia za kijijini ukweli inasikitisha sana, kisa hichi kimenifanya niamini kuwa huko vijijini kuna wanawake wanaopitia mateso na manyanyaso kama haya...ni hivi.......
Mzee ni mtata kweli kweli yaani hazuiliki kwa yeyote katika maamuzi yake hali ambayo humfanya awe huru kumpiga mke wake atakavyo na hakuna wa kuingilia hata mamake mzazi hamsikilizi...ilifikia wakati huyu mama alitakaga kujinyonga lakini hakufanikiwa ndipo ndugu zake wakaingilia kati na kwenda kumshitaki serikali ya mtaa....
Alivoitwa yule mzee alikuwa mpole na kuomba radhi ili mambo yasiwe mengi....wakakubaliana aandike barua ya kukiri kutompiga tena na akirudia watamchukulia hatua kali zaidi.....basi wakatoa nakala moja ikaenda upande wa ndugu mwanamke na nyingine ikabaki serikali ya mtaa na nyingine wakabaki nayo....lengo ni kutafuta amani....
Lakini haikufanikiwa kwani baada ya mda mzee hyu alianza kumshinikiza mwanamke bila kuzileta barua hizo zote hakutakuwa na amani kwenye nyumba ile.... na kweli mwanamke akakubali kwenda kuchukua nakala zote na kumkabidhi mzee yule akiwa na imani ndio njia sahihi ya kuileta amani lakini hii ndo ilikuwa sawa na kujichumia fimbo.....
Mzee alipambana kurudisha uhuru wake na akafanikiwa na akaendelea kumpiga kila kosa ni mkanda mashine unatembea/kumpiga mbele ya watoto mpaka anajisaidia mbele ya watoto mzee hakuwa na huruma ata kidogo kumpiga kumchania nguo kumburuza yaani ni vitu vya ajabu Mara vitisho vya kumuua na kumwambia ikiwa utanishtaki popote basi nitakimbia na kukuachia watoto peke yake na ataenda kumloga awe chizi.
Huyu mama alishawahi kuondoka lakini alirudi kwa ajili ya watoto na mwanamke hawezi tena kuondoka kwa sababu anawapenda sana watoto wake anasema bora afe katikat ya watoto wake....huyu mama amekuwa ni mtu wa kulia kila kukicha kutokana na anachofanyiwa na mume wake.......
Ushauri wako utasaidia sana kumuokoa mwanamke huyu kwenye manyanyaso haya...ahsanten.