Unyonyaji wa serikali kwa watumishi wa umma ulianza hapa .

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Habari!
Unyonyaji unaanzia kwenye tangazo la kazi
Ukisoma tangazo lolote la kazi za serikali hasa ajira za kudumu utaona sehemu moja wameiandika kiwango cha mshahara kimafumbo, wenyewe wanaita kimuundo.
Mfano,: TGS D, TGOS A, TPAS D, TANAPA 4, TGTS C n.k, n.k.
Kama nia ni kuficha kiwango cha mshahara kwanini wataje na muundo ?
Kama unataja muundo pasipo ku attach summary ya muundo wote ili mtu aangalie kiwango halisi sio utahira huo?
Ni wazi serikali inawanyonya watumishi wake(baadhi).

Serikali unaogopa unaweza ukawa mhasibu unalipwa 790, 000 uko kazini miaka 3 na una degree kisha ukaona tangazo la ajira serikalini ofisi tofauti na unayofanyia kazi mshahara ni mara 2 na zaidi ya mshahara wako na sifa ni zilezile lazima uzalendo utakuisha. Utaamua uibe au upambane uhamie huko wanakolipwa mara mbili ya mshahara wako na posho juu.
 
Tatizo linaanzia pale ccm ilipoanzishwa mwaka 1977!

Tatzo litaendelea tena 2025 wakurugenzi na marpc wakiwa na washawasha, ya machozi na marungu wakiwa wanatangaza waliyoandikiwa na neccm kwa uhariri na kuchapwa na tccm.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…