Uongozi wa AL AHLY SC na YANGA SC waanzisha ushirikiano rasmi. Eng. Hersi na uongozi wa yanga watembezwa kwenye makao makuu ya AL AHLY

Madumbikaya

JF-Expert Member
Joined
Jun 6, 2018
Posts
639
Reaction score
1,919
Uongozi wa AL Ahly SC umewakaribisha Young Africans SC katika makao yao makuu na imeamriwa watafanya ushirikiano katika kukuza uwekezaji

Eng Hersi amesisitiza mbele ya uongozi wa al ahly kuwa mabadiliko ya kwanza walienda kujifunza FC Barcelona na kuanzisha ushirikiano ambao unawasaidia kupata mbinu na njia za kuendesha timu

Na sasa wamefurahia mbinu na mikakati waliyopatiwa toka Al ahly kwa kuweza kuwa club bora ya karne

Aidha Uongozi wa juu na maafisa waandamizi wa Young Africans wameonyeshwa mbinu na mikakati iliyowezesha al ahly kufikia pale walipo

Eneo la Ahly ni kubwa sana na limebeba kila kitu kuna masoko makubwa,masoko ya rejareja ,Viwanja vya mazoezi vya Football, basketball na Volleyball .Maeneo ya kuhifadhia makombe na sehemu za utalii na mahotel

Viongozi wa Young Africans wakiongozwa na Eng Hersi wamefanya vikao na mijadala kwa masaa zaidi ya kumi na Management ya Al Ahly

Wanaoruhusiwa kuingia kwenye compound ya al Ahly ni wale waliolipa life membership au uwanachama wa kudumu unaofikia dollar 40,000 au TZs milioni 100 ,Anayelipa life membership ndie ana enjoy facilities zote zilizopo Al Ahly compound

Management ya Al ahly wamekiri kuwa mpira unaochezwa na Young Africans ni wa kisasa sana hivyo nao wanahitaji kujifunza aina ya mpira wa kasi na wa kuvutiwa unaochezwa na Young Africans

Rais wa Al Ahly na Rais wa Young Africans wamekubaliana pia katika maeneo ya uwekazaji na Al ahly wamekubali kutuma watu wao kwa ajili ya kuisadia Young Africans kwenye mageuzi yake ya uongozi,miundombinu na mbinu za usajili
 
"Rais wa Al Ahly baada ya kuonyeshwa eneo la Jangwani ambalo Yanga Afrika inaenda kujenga uwanja wake, alishindwa kujizuia hadi akaangua kicheko"
Hahaaa sema wewe jamaa ni mpuuzi..ila Kuna mimbumbumbu mienzio sasa hivi inatukuna sana matusi tofauti na wewe unazungumza mpira.
 
"Rais wa Al Ahly baada ya kuonyeshwa eneo la Jangwani ambalo Yanga Afrika inaenda kujenga uwanja wake, alishindwa kujizuia hadi akaangua kicheko"
Mkuu wewe umetoka sayari gani, watu wansogeza bahari wanajenga airport itakua uwanja wa mpira
 
Mkuu wewe umetoka sayari gani, watu wansogeza bahari wanajenga airport itakua uwanja wa mpira
Wanaofanya hivyo hawana ardhi ya kutosha ndiyo maana wako radhi kuingia gharama za ziada kufanya hivyo.

Ngojeni hao maafisa waandamizi wenu wakirudi utasikia wanasema "kutokana na tulichokiona kule Misri, tumesitisha zoezi la ujenzi pale Jangwani"
 
Waboreshe kwanza lile gofu lao pale matopeni
 
Kote huko ilikuwa kuwabembeleza wasifungwe goli nyingi ndio maana wakawapangia mabenchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…