Uchaguzi 2020 Uongozi wa CHADEMA ulikuwa sahihi "kuwatimua" TBC katika uzinduzi wa kampeni zake

Kati ya taasisi za kipuuzi kabisa kwa sasa, mojawapo ni TBC.

Rais Magufuli amekuwa anatukana watu hadharani, na TBC wakiwa mubashara. Lakini wapinzani hawajawahi kutoa tusi lolote. Wakiusema tu ukweli dhidi ya Magufuli, wanasema ni matusi!

Hivi mtu akisema kuwa Rais amejenga uwanja mkubwa wa ndege Chato wakati hakuna hata manispaa moja yenye uwanja mkubwa kama wa Chato, hilo ni tusi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walienda kwa maagizo, toka lini wakafanya kazi bila maagizo
 
Mystery usichokijua tu ni kwamba hata hao TBC walihisi na walifanya 'Kusudi' ili 'muwatimue' na wapate sababu. Kiufupi Wao ndiyo Washindi hapa.
Nakubaliana na wewe kabisa. Hao jamaa walikuwa wanatafuta sababu tu ya beef na CDM liwe rasmi. Hiyo TV huwa inachefua sana na sidhani kama inatazamwa na watu wawanaojielewa
 
Mnawaonea Watangazaji bur, wao huwa hawajui ukifanya nini unakosea....anayejua yupo huko juu hivyo wanachofanya wao ni kubahatisha tu kwamba hili ni kosa na hili ndio sahihi.
 
Hakuna mtego hapo, kwanza tbccm haiangaliwi na watu wengi sana kama huna habari.
Wapuuzi sana, kodi zetu zitawatokea puani.
 
Mystery usichokijua tu ni kwamba hata hao TBC walihisi na walifanya 'Kusudi' ili 'muwatimue' na wapate sababu. Kiufupi Wao ndiyo Washindi hapa.
Nami niliwaza hivyo ila nkasema ngoja muda utaamua
Kwa hyo hapo chadema mikutano yao ya kampeni haitawekwa live kwa sababu kuwa hawataki chombo cha habari cha taifa lakini wanahubiri "uhuru wa vyombo vya habari"?


Sent from my SM-J701F using JamiiForums mobile app
 
Tutaona leo kama watakuwa wanakata matangazo ili kukidhi matakwa ya sheria ya maudhui

HAWATAKATA KWA KUWA WATAFUATA MAUDHUI YA UTANGAZAJI. FULL STOP.

MBONA JANA CDM HAWAJAPATA HATA REDIO STATION MBALI YA TV, KWA KUWA WENYE TV WALITOA MASHARTI YA KAMA WATAFUATA MAUDHUI YA UTANGAZAJI , WATAENDA, LKN HAWAKUONESHA KAMA KWELI WATAFUATA MASHARTI NDIO MAANA TV ZOTE ZILIJITOA. HATA TV YA UPANDE WA KWAO JANA ILIWATOLEA NJE. HAJUNA JANJA JANJA MWAKA HUU.
 
Watu mkitaka kila kitu muongee kishabiki ni kwamba ccm wataisapoti Tbc na wapinzani wataunga mkono ufukuzwaji wa watangazaji pale uwanjani...kwa sisi ambao hatuna vyama tunaona wote wamekosea pale na hakuna aliyefanya kitendo kizuri, TBC kukatakata matangazo hata mimi iliniuma sana, nilikuwa nasikiliza TbcTaifa mbowe alivyoanza kuongea uhuni wa kuenguliwa wabunge wa upinzani nikasikia mtangazaji anasema tusikilize kidogo wimbo wa uchaguzi, nikajikuta namtukana tu...then mbowe nae anakuja kusema Tbc watoke kisa wanakatakata matangazo.

Mambo ya Tbc mbowe angeyaacha tu yajiendeshe yenyewe kama watakavyo TBC wenyewe, hasira hizo hazina maana yoyote. Kwani kukatakata kwa matangazo ya Tbc kuna hasara gani kwa mkutano ule? Vyombo kibao vilikuwepo kuurusha live mkutano kwa hiyo Tbc ilivyokuwa inazingua watu tulihamia kwingine. Kuifukuza TBC uwanjani sio kitendo kizuri mngewaacha tu wafanye maovu yao na aibu ingewapata hata bila kuwafukuza.
 
Hakuna mtego hapo,kwanza tbccm haiangaliwi na watu wengi sana kama huna habari.

Wapuuzi sana, kodi zetu zitawatokea puani
Hivi hawa TBC watajisikiaje hapo Oktoba 28, watakapoona Mheshimiwa Tundu Lissu ndiye katangazwa mshindi katika uchaguzi mkuu?

Hivi hawataona aibu na watapiga U-Turn na kuanza kumtangaza kwa kuwa tayari keshakuwa Rais?
 
Mimi nimeshangaa kwamba kumbe TBC inafuatiliwa Sana kiasi kwamba wana CDM walilalamikia kwamba matangazo yalikua yanakatakata.
Nikawaza Kama yanakatakata TBC si nikuangalia kupitia njia nyingine na kuwaacha TBC ili kila mmoja atumie uhuru wake.

Wanaosema huwa hawaangalii TBC unawakuta ndio wnaolalamika ilikua inakatakata.

Makosa ya TBC hayakusahihishwa kwa hekima na kutumiwa vyema na CDM zaidi waliharibu zaidi na kiki ikahamia kwa TBC sio kwa uzinduzi wa kampeni.

Sent from my Infinix X603 using JamiiForums mobile app
 
Suala ni kuwa hiko chombo cha habari cha TBC kinaendeshwa kwa kodi zetu sote wana-ccm na wana Chadema, sasa swali la kujiuliza ni kwa vipi wao wajifanye kama chombo cha habari cha chama kimoja tu cha CCM?
 
TBC ni hovyo kabisa na inaudhi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…