Uongozi wa SIMBA uwe na utaratibu wa kuaaga wachezaji wake kwa kuwapa zawadi

mpimamstaafu

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
4,445
Reaction score
4,707
Hakika nimeshtushwa sana kusikia kuna wachezaji wa Mabingwa wa Soka Simba wameachwa kwenye Usajili na wengine wamesajiliwa na Vilabu vya ndani na nje ya Nchi.

Ni vema Klabu ya Simba ikawa na Utaratibu wa kuwaaga wachezaji wake kwani Walitoa michango yao kwenye Klabu ikibidi ikawaandalia Mechi na kuwaaga mbele ya mashabiki na wanachama wao.

Utaratibu huu ni kuonyesha uungwana kwa hao wachezaji kwani ndio walioifikisha Simba Robo fainal na kutwaa Ubingwa wa 2019/2020.
 
Mastermind hayupo waliopo ni watu wa mafao Haji rudi tafadhali
 
Mkuu huu utaratibu umeutolea wapi, wachezaji wanaoagwa ni mara nyingi wanaostaafu sio kuachwa ama kuhama, ronaldo kwenda madrid ilichezwa mechi gani kumuaga!? Cr7 kawapa madrid uefa 4 ilichezwa mechi gani kuaga, hazard je katoka kuwapa chelsea europa mechi ya kumuoga umeiona, vipi th 14, thierry henry kichogo, aliagwa na arsenal!!??

Hizi ni siasa na porojo, ulitaka ichezwe mechi ya kumuaga kotei na wenzake!? Liver ya comeback ndani ya Istanbul miracle msimu uliofata kama sikosei kina smicer waliachwa hakuna cja mechi ya kuaga wala nini..

Mechi za kuagana ni mtu anapostaafu.
 
Mkuu kwani Simba Day ipo kwa vilabu vyote Duniani? Ni utaratibu ambao Klabu ya Simba imejiwekea,kuwaaga wachezaji nao ni utaratibu wa kuwashukuru kwa michango yao na mafanikio waliyoipatia klabu.
 
Mkuu kwani Simba Day ipo kwa vilabu vyote Duniani? Ni utaratibu ambao Klabu ya Simba imejiwekea,kuwaaga wachezaji nao ni utaratibu wa kuwashukuru kwa michango yao na mafanikio waliyoipatia klabu.
Basi mkuu Simba ndio hawana huo utaratibu wa kuaga wachezaji wanaowaacha.
 
Basi mkuu Simba ndio hawana huo utaratibu wa kuaga wachezaji wanaowaacha.
Viongozi wa Simba ni Wasikivu ndio maana tunawashauri mkuu ni utaratibu wa kiungwana kwa wachezaji walioisaidia klabu kutwaa ubingwa kuwashukuru na pia kuwaaga pindi wanapoachana na klabu
 
Viongozi wa Simba ni Wasikivu ndio maana tunawashauri mkuu ni utaratibu wa kiungwana kwa wachezaji walioisaidia klabu kutwaa ubingwa kuwashukuru na pia kuwaaga pindi wanapoachana na klabu
Umeona kimya maana yake huo utaratibu haupo na hawana, utaratibu uliopo nadhani ni kama kwa wengine, aliagwa mgosi kwenye kustaafu, nasisitiza utaratibu huo haupo na hautakuwepo, aliyeachwa kaachwa, aliyeuzwa kauzwa, tunashukuru kwa mawazo na mtazamo wenu.
 
Yaani kama vile yondani alipotoka simba kwenda yanga ulitaka aagwe kwa sherehe sio? Ndo akili zako zilivyokutuma sio?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…