changaule
JF-Expert Member
- Jan 10, 2020
- 6,039
- 10,151
Awali napongeza uongozi kwa kuweza kukamilisha usajili wa wachezaji, japo sijajua kama usajili umekamilika au bado kuna wachezaji wengine watakaosajiliwa.
Kwa uzoefu wa mpira ni kwamba usajili unaweza kulipa au usilipe ni sawa na kamari kuna kufanikiwa na kutofanikiwa hivyo sio jambo la kutamba au kuwa mnyonge kwa kusikia tu majina ya wachezaji waliosajiliwa msimu huu hadi pale msimu utakapoanza na tukashuhudia watakachotupa.
Niende kwenye swala la msingi;. Msimu uliopita viongozi mlitukosea sana kwa kutokuwa na malengo na mikakati ya timu kufanya vizuri klabu bingwa jambo ambalo limetufanya tusifike mbali.
Tulifanya makosa kadhaa ikiwemo ufinyu wa maandalizi ya timu (kutopata muda wa kuandaa timu na pia kutopata michezo ya kirafiki ya kimataifa walau tatu za kujipima nguvu) kutokamilisha kwa wasaa ITC za wachezaji wapya waliosajiliwa.
Hivyo naushauri uongozi kuwa wachezaji wapya waliosajiliwa watafutiwe ITC zao mapema ili waitumikie timu katika michuano ya klabu bingwa hatua ya awali. Pili ni kuhakikisha timu inaandaliwa mapema na pia kupata mechi kadhaa za kuwafanya wawe na match fitness.
Kwa uzoefu wa mpira ni kwamba usajili unaweza kulipa au usilipe ni sawa na kamari kuna kufanikiwa na kutofanikiwa hivyo sio jambo la kutamba au kuwa mnyonge kwa kusikia tu majina ya wachezaji waliosajiliwa msimu huu hadi pale msimu utakapoanza na tukashuhudia watakachotupa.
Niende kwenye swala la msingi;. Msimu uliopita viongozi mlitukosea sana kwa kutokuwa na malengo na mikakati ya timu kufanya vizuri klabu bingwa jambo ambalo limetufanya tusifike mbali.
Tulifanya makosa kadhaa ikiwemo ufinyu wa maandalizi ya timu (kutopata muda wa kuandaa timu na pia kutopata michezo ya kirafiki ya kimataifa walau tatu za kujipima nguvu) kutokamilisha kwa wasaa ITC za wachezaji wapya waliosajiliwa.
Hivyo naushauri uongozi kuwa wachezaji wapya waliosajiliwa watafutiwe ITC zao mapema ili waitumikie timu katika michuano ya klabu bingwa hatua ya awali. Pili ni kuhakikisha timu inaandaliwa mapema na pia kupata mechi kadhaa za kuwafanya wawe na match fitness.