NALIA NGWENA
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 10,587
- 13,425
Makamu wa Rais wa klabu ya Young Africans Arafat Haji, amewaondoa wasiwasi Mashabiki na Wanachama wa Klabu hiyo kuhusu mustakabali wa Mshambuliaji kutoka DR Congo Fiston Kalala Mayele, ambaye anadaiwa kuwindwa na baadhi ya Klabu za BArani Afrika.
Kufanya vizuri kwa Mayele akiwa na Young Africans kwenye Michuano ya Kimataifa kumezitamanisha klabu kadhaa kuhitaji huduma ya Mshambuliaji huyo ambaye amekuwa msaada mkubwa kwa Wananchi.
Baadhi ya klabu zinazotajwa kuwania saini ya Mshambuliaji huyo kinara wa mabao katika Kombe la Shirikisho Barani Afrika msimu huu akifunga saba ni Kaizer Chiefs, Orlando Pirates za Afrika Kusini, US Berkane na Raja Casablanca za Morocco.
Kufanya vizuri kwa Mayele akiwa na Young Africans kwenye Michuano ya Kimataifa kumezitamanisha klabu kadhaa kuhitaji huduma ya Mshambuliaji huyo ambaye amekuwa msaada mkubwa kwa Wananchi.
Baadhi ya klabu zinazotajwa kuwania saini ya Mshambuliaji huyo kinara wa mabao katika Kombe la Shirikisho Barani Afrika msimu huu akifunga saba ni Kaizer Chiefs, Orlando Pirates za Afrika Kusini, US Berkane na Raja Casablanca za Morocco.