Even MOre
JF-Expert Member
- May 6, 2023
- 204
- 298
Nimekuwa nikifatilia muda mrefu sana toka Serikali imebadili baadhi ya maombi ya ajira kuwa yanaombwa kwa njia ya mtandao (Online Application) nina kama miaka 4 sasa nafanya kazi hii ya kusaidia watu kutuma maombi kwa njia ya mtandao (Internet services) pia huduma ya mifumo ya Kiserikali.
Hoja iko hivi kwa hii miaka kadhaa kumekuwa na shida kubwa pale tu ambapo Taasisi flani ya Serikali ikitangaza nafasi za kazi ziwe za muda au za kudumu basi kutatokea shida ya mfumo husika wa maombi ya kazi kushindwa kufanya kazi hadi zitakapobaki siku kadhaa kufikia mwisho wa maombi (Deadline) kama siku 1&2 ndipo mfumo hurejea na kuweza kufunguka kwa urahisi kabisa.
Nimeshuhudia haya mfano kipindi cha maombi ya kazi za Ualimu, Kada ya Afya, Maombi ya Sensa, nk mpaka maombi yanayoendelea ya kujiunga na Jeshi la Polisi ambayo deadline ni kesho, toka watangaze mpaka leo mfumo haufunguki licha ya shida internet nchini lakini mifumo mingine ya Serikali inafunguka na kutumika bila shida kabisa.
Maswali yangu ni haya:-
1. Ikiwa kuna shida ya mfumo kuwa na watumiaji wengi (Traffic jam) kwanini mifumo haiboreshwi kwa miaka yote hii ambapo wanajua kila wakati wanapotoa matangazo watu waombe kwa njia ya mfumo wanaona mfumo unalemewa na watumiaji?
Kama ni mfumo kuzidiwa na watumiaji, kwanini wasiongeze Servers zenye uwezo mkubwa wa kufanya kazi kwa kasi zaidi ili kuendana na muda wa maombi uliopangwa?
2. Ikiwa hakuna wataamu waajiliwa wa Serikali wanaoweza kutatua changamoto hii ambayo imekuwa inajirudia mara zote, kwanini Serikali wasiingie ubia na makampuni ya Teknolojia yenye Wataalamu wabobezi (Ukweli Serikalini hakuna wataalamu walio bora wengi kanjanja).
3. Ikiwa kunakuwa na shida ya mfumo inakuwaje baadhi ya watu wanaweza kufanya maombi? (Hapa inaingia dhana kuwa kuna namna inafanyika)
4. Ikiwa tunataka kuendana na kasi ya mabadiliko ya Teknolojia Dunia lakini hatutaki kuboresha mifumo yetu na kutaweka watu wenye ujuzi na waliobobea bila kujali Elimu zao, kwanini tusibaki kwenye utaratibu wa zamani wa maombi kutumwa kwa njia ya mkono?
Nawasilisha
Hoja iko hivi kwa hii miaka kadhaa kumekuwa na shida kubwa pale tu ambapo Taasisi flani ya Serikali ikitangaza nafasi za kazi ziwe za muda au za kudumu basi kutatokea shida ya mfumo husika wa maombi ya kazi kushindwa kufanya kazi hadi zitakapobaki siku kadhaa kufikia mwisho wa maombi (Deadline) kama siku 1&2 ndipo mfumo hurejea na kuweza kufunguka kwa urahisi kabisa.
Nimeshuhudia haya mfano kipindi cha maombi ya kazi za Ualimu, Kada ya Afya, Maombi ya Sensa, nk mpaka maombi yanayoendelea ya kujiunga na Jeshi la Polisi ambayo deadline ni kesho, toka watangaze mpaka leo mfumo haufunguki licha ya shida internet nchini lakini mifumo mingine ya Serikali inafunguka na kutumika bila shida kabisa.
Maswali yangu ni haya:-
1. Ikiwa kuna shida ya mfumo kuwa na watumiaji wengi (Traffic jam) kwanini mifumo haiboreshwi kwa miaka yote hii ambapo wanajua kila wakati wanapotoa matangazo watu waombe kwa njia ya mfumo wanaona mfumo unalemewa na watumiaji?
Kama ni mfumo kuzidiwa na watumiaji, kwanini wasiongeze Servers zenye uwezo mkubwa wa kufanya kazi kwa kasi zaidi ili kuendana na muda wa maombi uliopangwa?
2. Ikiwa hakuna wataamu waajiliwa wa Serikali wanaoweza kutatua changamoto hii ambayo imekuwa inajirudia mara zote, kwanini Serikali wasiingie ubia na makampuni ya Teknolojia yenye Wataalamu wabobezi (Ukweli Serikalini hakuna wataalamu walio bora wengi kanjanja).
3. Ikiwa kunakuwa na shida ya mfumo inakuwaje baadhi ya watu wanaweza kufanya maombi? (Hapa inaingia dhana kuwa kuna namna inafanyika)
4. Ikiwa tunataka kuendana na kasi ya mabadiliko ya Teknolojia Dunia lakini hatutaki kuboresha mifumo yetu na kutaweka watu wenye ujuzi na waliobobea bila kujali Elimu zao, kwanini tusibaki kwenye utaratibu wa zamani wa maombi kutumwa kwa njia ya mkono?
Nawasilisha
Upvote
2