Updates za Beijing Auto Show 2024 (25 April - 4 May)

Mercedes Benz MG GT 63 S E Performance
Hii niliitaja tu nilivokua naongelea G Wagen ya umeme. Ila Mercedes Benz wamezindua hii performance car ambayo ni Hybrid.

Hizi Falcon wings πŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™Œ

Okay, ni performance hybrid car, ina 4.0L bi-turbo V8 engine, so she is quick! Ina jumla ya 805 hp na ina acceleration kali ya 0-100kph ndani ya 2.7 sec.

Wazee wa manual mtatusamehe.
 
H

Hivi haya magari ya umeme unachaji popote hata nyumbani kwako au sehemu maalum?
Ata nyumbani, ila speed itategemea na umeme ulioletwa kwenu. Ila umeme wa nyumbani Tegemea kuchaji slow kama ni ule wa kawaida.

Hiko hivi, wameweka charging levels mbalimbali kutegemea na umeme unaokuja kwako. Home nyingi ni Level 1 na Level 2, ambao ni AC current na wakati ule ambao wanaita Public (mfano unakuta mtu anaweka station ya kuchajia pale Mlimani city) inakuaga DC fast charging, Level 3.

Level 1 inatumia 120 Volt outlet (AC current), inatoa 1 -2 kW ya power, na mara nyingi ukichaji kwa saa 1 inakupa kama kilometa 6-8 hivi za range.
Hii inaweza kuchukua masaa 24 hadi 40 kujaza full charge battery (factors zipo nyingi za kutofautiana muda).

Level 2 inatumia 240 Volt (AC current) hii inatoa 19 kW ya power na kwa saa 1 inaweza kukupa kilometa 15 hadi 30 hivi. Hizi pia zinaweza kupatikana nyumbani, makazini na public charging stations.


Level 3 ndio inaitwaga DC fast charging. Hii yenyewe inatumia DC currentna inaweza kuongeza kilometa 5 hadi 30 kwa dakika utakayo charge, kwasababu inatoa power rate kubwa ya 25 hadi 350 kW.

Wanashauri uwe unapendelea kuchaji na Level 1 au 2 mara nyingi kuliko Fast Charging.

Na pia hakikisha chuma inakua na charge 30% hadi 85% ili battery idumu sanaaaa.
 
Li Mega from Li Auto
Li Auto tuliwaongelea jana kaa kuzindua Li Auto L6 (kama hatukutaja nitacheki). Ila kama haitochi, wezindua MPV kubwaaa linaitwa Li Mega.

Hii MPV aka minivan ina battery lenye 102 kWh na ina support 5C ultra fast charging.


Kama sio waongo, hii gari inafika 100km/h ndani ya sekunde 5.5 tu.




Mchina hana masihara. Ndani mbele kuna massive screen, na nyuma kuna screen ya abiria wa nyuma ambayo una control kwa gesture. Haina haja kuigusa.

Baadhi ya info hawajatoa bado
 
Kwa maelezo haya tupambane na hybrid.
Mkuu pia nilitaka kupata ufahamu kuhusu PHEV na Hybrid. Nimetafuta mitandaoni nipate uelewa kwa lugha rahisi lakini sijatosheka.
Kama mdau wa magari na kwa kuzingatia mazingira yetu ya kibongo na huu umeme wetu mwingi usio na ubora unashauri gari aina gani haitasumbua kati ya PHEV na Hybrid.
 
Chery ni balaa hii kampuni Wana ndinga zinatisha
Massive Government subsidies , makampuni ya China ni ngumu kushindana nao maana hata wakiuza kwa hasara ,CCP government inawapa subsidies kufidia hasara .
Unfair competition
Huwezi shindana na makampuni ya China Kwa mwendo huu
Imefikia kipindi BYD na wengine wanafanya kuua soko kwa kuuza kwa dumping price isiyoendana na uhalisia
 
Kuna gari BYD inaitwa seagul , imezinduliwa hivi karibuni , inauzwa kwa 9700usd
Its ridiculous .

Imagine
Ukija kupiga cost za uzalishaji wa Tesla model yenye specifications kama hizo , bei lazima iwe juu .
Na hapo hujaweka cheap labours na low industrial regulations za China
Mchina lazima a win

Ndio maana hata Elon Musk anatoa kilio huko na nguvu anahamishiwa kwenye Ventures nyingine kama kuzalisha robots , tunnel boring machines , starlink ,space X nk
 
Na si Mmarekani tu anaye suffer na competition ya makampuni ya China amvayo yanapewa boost kubwa ya kifedha na serikali ya China ,
Germany , the industrial power house ya uzalishaji wa magari na mitambo pale ulaya wanakiona cha moto .
Wote kampuni zao zinashindwa kucompete na makampuni ya China Kwa sasa .
Kampuni la Porsche ,BMW , Volkswagen , Audi zinapumulia mirija .
Production costs zao zipo juu pia ,so mwisho wa siku ,customers wanakimbilia Kitonga
 
Ukiangalia hata sekta ya uzalishaji wa mitambo ya kufua Renewable energy ,kama solar na wind .
Mchina kampuni zake zinapata mtonyo mrefu toka kwa serikali ,so zinauza products Kwa dumping fee , mfano solar panels na wind turbines
Kampuni kongwe kama Siemens wanakutana na ushindani mkali kwenye soko pia
 
Mchina ni hatari sana
 
Hakuna unachokijua wewe.

Tafuta pesa kijana, utakufa masikini.

Simu za Apple ambazo ni iPhone zinatengenezwa Shenzhen, ama ili ufahamu?
 
Nilimsikia mwigulu akisema electric car wataondoa Kodi, SS sijajua kama anatania ama Kweli
 
Ndio maana CCP nawakubali Sana.Safiiii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…