Upelelezi wa kesi ya kuchana noti zenye thamani ya Bilioni 4.6 iliyoanza mwaka 2020, bado unaendelea

Upelelezi wa kesi ya kuchana noti zenye thamani ya Bilioni 4.6 iliyoanza mwaka 2020, bado unaendelea

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Upelelezi wa kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili watu 13, wakihusishwa na uharibifu wa noti zenye thamani ya Sh4.6 bilioni, bado unaendelea.

Kesi hiyo, ambayo imekuwa ikifuatiliwa kwa muda mrefu, ilitajwa leo Alhamisi, Februari 20, 2025, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Kwa mujibu wa mashtaka, kundi hilo linakabiliwa na makosa matano, mojawapo likiwa ni kuharibu noti hizo na kusababisha Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kupata hasara kubwa.

Wakili wa Serikali, Winiwa Kasala, ameeleza kuwa upelelezi upo katika hatua za mwisho, lakini shauri limeahirishwa hadi Machi 20, 2025, kwa sababu Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Anna Magutu, yupo likizo.

jengo la bot.png


Miongoni mwa washtakiwa ni wafanyakazi wa BoT waliotajwa kuwa Mariagoreth Kunzugala (maarufu kama Bonge), Henry Mbowe (Mzee wa Vichwa), Asha Sekiboko, Cecilia Mpande, Agripina Komba, Zubeda Mjewa, Khadija Kassunsumo, na Mwanaheri Omary—wote wakiwa wakazi wa Dar es Salaam.

Washtakiwa wengine, ambao si watumishi wa BoT, ni Alistides Genand, Musa Chengula, Zaituni Chihipo, na Respicius Rutabilwa.

Hati ya mashtaka inaeleza kuwa kati ya Januari 2017 na Septemba 30, 2019, baadhi ya watuhumiwa, wakitumia nyadhifa zao ndani ya BoT, walivunja majukumu yao ya kazi na kuruhusu kutokea kwa kosa la kuongoza genge la kihalifu. Pia, Genand, Chengula, Chihipo, na wenzao wanadaiwa kushirikiana na watumishi hao wa BoT kurahisisha njama hizo.

Kosa lingine linalowakabili ni kuharibu noti 460,000 za Sh10,000 kila moja, zenye thamani ya Sh4.6 bilioni, kwa kuzikatakata. Pia, wanadaiwa kufaidika na Sh1.5 bilioni kutoka BoT baada ya kuwasilisha noti hizo benki hiyo.

Awali, walikuwa na mashitaka sita, lakini Juni 18, 2021, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) aliondoa shtaka la utakatishaji fedha, na kuwaacha na makosa matano yanayoendelea kushughulikiwa mahakamani.

Source: Mwananchi
 
Kwanini kipindi hiki!!?

Nani anatafutwa!!?lazima ushahidi utawakumba baadhi ya wazito waliopo mzigoni!

Lazima Kuna watu wataliwa vichwa au kupotezewa uhalali wa kuwa kwenye vitengo vyao!!
 
Wakuu,

Upelelezi wa kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili watu 13, wakihusishwa na uharibifu wa noti zenye thamani ya Sh4.6 bilioni, bado unaendelea.

Kesi hiyo, ambayo imekuwa ikifuatiliwa kwa muda mrefu, ilitajwa leo Alhamisi, Februari 20, 2025, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Kwa mujibu wa mashtaka, kundi hilo linakabiliwa na makosa matano, mojawapo likiwa ni kuharibu noti hizo na kusababisha Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kupata hasara kubwa.

Wakili wa Serikali, Winiwa Kasala, ameeleza kuwa upelelezi upo katika hatua za mwisho, lakini shauri limeahirishwa hadi Machi 20, 2025, kwa sababu Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Anna Magutu, yupo likizo.

View attachment 3243950

Miongoni mwa washtakiwa ni wafanyakazi wa BoT waliotajwa kuwa Mariagoreth Kunzugala (maarufu kama Bonge), Henry Mbowe (Mzee wa Vichwa), Asha Sekiboko, Cecilia Mpande, Agripina Komba, Zubeda Mjewa, Khadija Kassunsumo, na Mwanaheri Omary—wote wakiwa wakazi wa Dar es Salaam.

Washtakiwa wengine, ambao si watumishi wa BoT, ni Alistides Genand, Musa Chengula, Zaituni Chihipo, na Respicius Rutabilwa.

Hati ya mashtaka inaeleza kuwa kati ya Januari 2017 na Septemba 30, 2019, baadhi ya watuhumiwa, wakitumia nyadhifa zao ndani ya BoT, walivunja majukumu yao ya kazi na kuruhusu kutokea kwa kosa la kuongoza genge la kihalifu. Pia, Genand, Chengula, Chihipo, na wenzao wanadaiwa kushirikiana na watumishi hao wa BoT kurahisisha njama hizo.

Kosa lingine linalowakabili ni kuharibu noti 460,000 za Sh10,000 kila moja, zenye thamani ya Sh4.6 bilioni, kwa kuzikatakata. Pia, wanadaiwa kufaidika na Sh1.5 bilioni kutoka BoT baada ya kuwasilisha noti hizo benki hiyo.

Awali, walikuwa na mashitaka sita, lakini Juni 18, 2021, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) aliondoa shtaka la utakatishaji fedha, na kuwaacha na makosa matano yanayoendelea kushughulikiwa mahakamani.

Source: Mwananchi
Kwa utawala huu na rushwa ilivyotamalaki kwenye vyombo vya sheria, hakuna atakayefungwa wala kuwajibishwa hapo.
 
Wakaharibu bil 4 ili kupata bil 1.5 watu 13

1,500,000,000÷13=115,384,233
 
Inasogeasogea ili msahau, mkisahau inapigwa dismiss jamaa wanakuja kuvimba kitaa.
 
Wakuu,

Upelelezi wa kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili watu 13, wakihusishwa na uharibifu wa noti zenye thamani ya Sh4.6 bilioni, bado unaendelea.

Kesi hiyo, ambayo imekuwa ikifuatiliwa kwa muda mrefu, ilitajwa leo Alhamisi, Februari 20, 2025, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Kwa mujibu wa mashtaka, kundi hilo linakabiliwa na makosa matano, mojawapo likiwa ni kuharibu noti hizo na kusababisha Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kupata hasara kubwa.

Wakili wa Serikali, Winiwa Kasala, ameeleza kuwa upelelezi upo katika hatua za mwisho, lakini shauri limeahirishwa hadi Machi 20, 2025, kwa sababu Hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Anna Magutu, yupo likizo.

View attachment 3243950

Miongoni mwa washtakiwa ni wafanyakazi wa BoT waliotajwa kuwa Mariagoreth Kunzugala (maarufu kama Bonge), Henry Mbowe (Mzee wa Vichwa), Asha Sekiboko, Cecilia Mpande, Agripina Komba, Zubeda Mjewa, Khadija Kassunsumo, na Mwanaheri Omary—wote wakiwa wakazi wa Dar es Salaam.

Washtakiwa wengine, ambao si watumishi wa BoT, ni Alistides Genand, Musa Chengula, Zaituni Chihipo, na Respicius Rutabilwa.

Hati ya mashtaka inaeleza kuwa kati ya Januari 2017 na Septemba 30, 2019, baadhi ya watuhumiwa, wakitumia nyadhifa zao ndani ya BoT, walivunja majukumu yao ya kazi na kuruhusu kutokea kwa kosa la kuongoza genge la kihalifu. Pia, Genand, Chengula, Chihipo, na wenzao wanadaiwa kushirikiana na watumishi hao wa BoT kurahisisha njama hizo.

Kosa lingine linalowakabili ni kuharibu noti 460,000 za Sh10,000 kila moja, zenye thamani ya Sh4.6 bilioni, kwa kuzikatakata. Pia, wanadaiwa kufaidika na Sh1.5 bilioni kutoka BoT baada ya kuwasilisha noti hizo benki hiyo.

Awali, walikuwa na mashitaka sita, lakini Juni 18, 2021, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) aliondoa shtaka la utakatishaji fedha, na kuwaacha na makosa matano yanayoendelea kushughulikiwa mahakamani.

Source: Mwananchi
Huo upelelezi tu kwa miaka yote inaonyesha ni sheria inaenda kuchezewa wala hakuna haki itafanyika kwenye hii kesi.
 
Miongoni mwa washtakiwa ni wafanyakazi wa BoT waliotajwa kuwa Mariagoreth Kunzugala (maarufu kama Bonge), Henry Mbowe (Mzee wa Vichwa), Asha Sekiboko, Cecilia Mpande, Agripina Komba, Zubeda Mjewa, Khadija Kassunsumo, na Mwanaheri Omary—wote wakiwa wakazi wa Dar es Salaam.
90% wanawake nini kilitokea? Mapepo!!
 
Kesi itafutwa na wao watarudishwa kazini + kuhamishwa vituo vya kazi, mpk sasa wanapokea mishahara kama kawa
 
Kosa lingine linalowakabili ni kuharibu noti 460,000 za Sh10,000 kila moja, zenye thamani ya Sh4.6 bilioni, kwa kuzikatakata. Pia, wanadaiwa kufaidika na Sh1.5 bilioni kutoka BoT baada ya kuwasilisha noti hizo benki hiyo.
Wahuni sana hawa jamaa.
 
Back
Top Bottom