Upendo wa Mbarawa Unazidi Viwango Vyote

Upendo wa Mbarawa Unazidi Viwango Vyote

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Wanaotufundisha umuhimu wa upendo, kadiri ya maagizo ya kitabu Kitakatifu cha Biblia, wanatuambia kuwa, Umpende mwenzako kama unavyojipenda mwenyewe. Sijawahi kuona wala kusikia kuwa kuna mahali imenenwa umpende mwenzako zaidi ya unavyojipenda mwenyewe. Na Mungu pekee yake ndiye aliupenda sana ulimwengu hata akamtoa mwanae wa pekee ili ulimwengu upone. Kwa mwanadamu, ni vigumu sana.

Napenda niamini maneno ya Mbarawa na wale wote wanaomwunga mkono kuwa mkataba wa bandari kati ya Serikali ya Tanzania na kampuni ya DP World ya Dubai, ndio mkataba mzuri kuliko yote ambayo tunayo, na kwamba DP ikishachukua bandari zote za Tanganyila:

1) Itakuwa mwisho wa tatizo la ajira kwa vijana wa Tanzania

2) Zaidi ya 60% ya bajeti itachangiwa na mapato ya bandari pekee. Na hivyo kwa sababu bajeti yetu 40% huwa inajazilizwa na misaada na mikopo. Kodi zetu zote toka viwandani, kwa wafanyakazi, wafanyabiashara, tozo, migodi, utalii, adhabu za barabarani, ushuru wa mazao na misitu huwa zinachangia 60%. Hii ina maana kutokana na ujio wa DP, bwana Mbarawa anataka kusema sasa tunaweza kufuta kodi, tozo na ushuru wote, na pengo likazibwa na DP pekee yake, halafu 40% iliyosalia tukaendelea kujazilizia kwa mikopo na misaada. Watanganyika wataishi bila ya bugdha ya kodi, tozo wala ushuru. Tanganyika itaingia kwenye orodha ya zile nchi chache sana Duniani ambazo wananchi wake hawalipi kodi yoyote! Neema kubwa hii toka DP iliyosababishwa na upendo wa pekee wa bwana Mbarawa na katibu wake Aisha Amour, wote wazanzibari.

Mahali panaposhangaza zaidi, Mbarawa na Amour, wote wazanzibari, nyumbani kwao kwa asili ambako wapo wazazi wao, wajomba zao, mabibi zao, mabinamu zao, shemeji zao, wapwaa zao, ni Zanzibar. Wakati wakionesha upendo wa pekee ambao haujawahi kutokea Duniani, kwa watanganyika, wamekosa kabisa upendo kwa ndugu zao wa damu waliopo Zanzibar. Wakaamua ndugu zao wa damu kule Zanzibar, wasinufaike kabisa na hizo neema za pekee wanazotuambia zinaambatana na ujio wa DP. Wakaamua kuziweka bandari zote za Zanzibar, nje ya mkataba. Watu hawa wana chuki kubwa sana kwa ndugu zao wa damu!!

Hawa waheshimiwa, baada ya kuhudumu kwenye serikali ya JMT, watarudi nyumbani kwao, kwa ndugu zao wa damu, waliowatenga na neema za DP!! Maana yake wameamua kuwapenda watanganyika kuliko wanavyojipenda wenyewe? Jamani ni upendo ulioje huu? Ndiyo maana wengine wamesema kuwa watu hawa wapambwe kwa maua ya dhahabu.

Jibu lisipokuwa la ndiyo, basi itamaanisha watu hawa wanawachukia mno Watanganyika, kiasi cha kuamua kuwaletea watanganyi chatu awameze, wakati kwa upendo mkubwa na wa upendeleo, wakiwalinda jamaa zao wa damu kwa kuwaweka mbali na chatu, ili hata siku wakirudi nyumbani, wawaambie ndugu zao, "angalieni ndugu zetu tulivyowalinda, hata tukawaweka mbali na gharika ili msiangamie. Tumewaokoa, tumedhihirisha ni namna gani chura ana uwezo wa kumwua tembo. Tuwadogo, tuwachache, lakini tumemwangamiza mkubwa, tumewatia utumwani walio wengi"

Kwa wasiojua ni kwa namna gani chura humwua tembo: Chura hukaa kwenye maji, hasa madimbwi na mabwawa. Tembo kwa sababu mkonga wake ni mkubwa, anapoenda kunywa maji huvuta vitu vyote vidogo vidogo vilivyopo karibu na pale anapokunywa maji, chura ni miongoni mwa viumbe ambao huvutwa. Akiingia kwenye mkonga wa tembo hujibanza ukutani, na hivyo haendi pamoja na maji kwenye tumbo la tembo. Chura asili yake ni kupiga kelele. Baada ya muda chura huanza kupiga kelele akiwa ndani ya mkonga wa tembo. Tembo kwa hasira, huanza kubamiza mkonga wake kwenye miti na mawe kwa lengo la kumwua chura, lakini kinachochakaa ni mkonga wake ambao ndiyo mkono wake unaompa maisha. Mwishowe tembo hupoteza maisha.

Ukubwa wa nchi siyo hoja, itategemea huyo mdogo umemweka wapi. Kama umemweka kwenye moyo, hata uwe mkubwa namna gani, atakuangamiza.
 
Wanaotufundisha umuhimu wa upendo, kadiri ya maagizo ya kitabu Kitakatifu cha Biblia, wanatuambia kuwa, Umpende mwenzako kama unavyojipenda mwenyewe. Sijawahi kuona wala kusikia kuwa kuna mahali imenenwa umpende mwenzako zaidi ya unavyojipenda mwenyewe. Na Mungu pekee yake ndiye aliupenda sana ulimwengu hata akamtoa m
Na wale wezi wa mabilioni aliyoyataja mkaguzi mkuu wa serikali nao wataiba zaidi bila kubugudhiwa, mama asifiwe amen.
 
60% ya mapato ya bajeti itachangiwa na bandari?!

Mbarawa ameamua kwa lazima kutugeuza watumwa ndani ya nchi yetu.

Inawezekana vipi mwarabu aliyekuja kufanya biashara kwetu profit apeleke kwao, atupe sisi asilimia 60 kwa ajili ya bajeti yetu?

Kwamba Mbarawa anathibitisha kiuhalisia kwa hiyo kauli yake kwamba, tumempa mwarabu mamlaka kamili ya nchi, yeye ndie mtawala wetu sasa.
 
Kwanza ukisoma tu hizo figure zao unaona kuwa ni uongo, kama hao DP World watailipa Serikali fedha zote hizo wao faida yao wataipataje? Tunaambiwa wanawekeza, je hiyo fedha watairudishaje na lini au baada ya muda gani hadi waanze kutulipa sisi kiasi chote hicho au Falme za Kiarabu wameamua kutupa fedha bure? Isitoshe ingekuwa ni rahisi hivyo nchi zote zenye Bandari Duniani wangefunga safari kwenda Dubai ili DP World wawaletee utajiri wa bure, huu ni uongo na umafia wanaotufanyia.
 
Hawa waheshimiwa, baada ya kuhudumu kwenye serikali ya JMT, watarudi nyumbani kwao, kwa ndugu zao wa damu, waliowatenga na neema za DP!! Maana yake wameamua kuwapenda watanganyika kuliko wanavyojipenda wenyewe? Jamani ni upendo ulioje huu? Ndiyo maana wengine wamesema kuwa watu hawa wapambwe kwa maua ya dhahabu.
Watakwenda kula nao 10% waliyovuna kwa kuiuza Tanganyika kwa watawala wao wa zamani
 
Mheshimiwa apite kwenye njia iliyopambwa maua.
20230621_032407.jpg
 
Ccm wanajua kuongea lugha laini na kupika data ila utekelezaji ndio hafifu. We miaka zaidi ya 60, taifa hatujafanikiwa ata kwenye sekta moja ambayo kila taifa lingetutazama sie wa mfano.

Ata usafi,
 
Wanaotufundisha umuhimu wa upendo, kadiri ya maagizo ya kitabu Kitakatifu cha Biblia, wanatuambia kuwa, Umpende mwenzako kama unavyojipenda mwenyewe. Sijawahi kuona wala kusikia kuwa kuna mahali imenenwa umpende mwenzako zaidi ya unavyojipenda mwenyewe. Na Mungu pekee yake ndiye aliupenda sana ulimwengu hata akamtoa mwanae wa pekee ili ulimwengu upone. Kwa mwanadamu, ni vigumu sana.

Napenda niamini maneno ya Mbarawa na wale wote wanaomwunga mkono kuwa mkataba wa bandari kati ya Serikali ya Tanzania na kampuni ya DP World ya Dubai, ndio mkataba mzuri kuliko yote ambayo tunayo, na kwamba DP ikishachukua bandari zote za Tanganyila:

1) Itakuwa mwisho wa tatizo la ajira kwa vijana wa Tanzania

2) Zaidi ya 60% ya bajeti itachangiwa na mapato ya bandari pekee. Na hivyo kwa sababu bajeti yetu 40% huwa inajazilizwa na misaada na mikopo. Kodi zetu zote toka viwandani, kwa wafanyakazi, wafanyabiashara, tozo, migodi, utalii, adhabu za barabarani, ushuru wa mazao na misitu huwa zinachangia 60%. Hii ina maana kutokana na ujio wa DP, bwana Mbarawa anataka kusema sasa tunaweza kufuta kodi, tozo na ushuru wote, na pengo likazibwa na DP pekee yake, halafu 40% iliyosalia tukaendelea kujazilizia kwa mikopo na misaada. Watanganyika wataishi bila ya bugdha ya kodi, tozo wala ushuru. Tanganyika itaingia kwenye orodha ya zile nchi chache sana Duniani ambazo wananchi wake hawalipi kodi yoyote! Neema kubwa hii toka DP iliyosababishwa na upendo wa pekee wa bwana Mbarawa na katibu wake Aisha Amour, wote wazanzibari.

Mahali panaposhangaza zaidi, Mbarawa na Amour, wote wazanzibari, nyumbani kwao kwa asili ambako wapo wazazi wao, wajomba zao, mabibi zao, mabinamu zao, shemeji zao, wapwaa zao, ni Zanzibar. Wakati wakionesha upendo wa pekee ambao haujawahi kutokea Duniani, kwa watanganyika, wamekosa kabisa upendo kwa ndugu zao wa damu waliopo Zanzibar. Wakaamua ndugu zao wa damu kule Zanzibar, wasinufaike kabisa na hizo neema za pekee wanazotuambia zinaambatana na ujio wa DP. Wakaamua kuziweka bandari zote za Zanzibar, nje ya mkataba. Watu hawa wana chuki kubwa sana kwa ndugu zao wa damu!!

Hawa waheshimiwa, baada ya kuhudumu kwenye serikali ya JMT, watarudi nyumbani kwao, kwa ndugu zao wa damu, waliowatenga na neema za DP!! Maana yake wameamua kuwapenda watanganyika kuliko wanavyojipenda wenyewe? Jamani ni upendo ulioje huu? Ndiyo maana wengine wamesema kuwa watu hawa wapambwe kwa maua ya dhahabu.

Jibu lisipokuwa la ndiyo, basi itamaanisha watu hawa wanawachukia mno Watanganyika, kiasi cha kuamua kuwaletea watanganyi chatu awameze, wakati kwa upendo mkubwa na wa upendeleo, wakiwalinda jamaa zao wa damu kwa kuwaweka mbali na chatu, ili hata siku wakirudi nyumbani, wawaambie ndugu zao, "angalieni ndugu zetu tulivyowalinda, hata tukawaweka mbali na gharika ili msiangamie. Tumewaokoa, tumedhihirisha ni namna gani chura ana uwezo wa kumwua tembo. Tuwadogo, tuwachache, lakini tumemwangamiza mkubwa, tumewatia utumwani walio wengi"

Kwa wasiojua ni kwa namna gani chura humwua tembo: Chura hukaa kwenye maji, hasa madimbwi na mabwawa. Tembo kwa sababu mkonga wake ni mkubwa, anapoenda kunywa maji huvuta vitu vyote vidogo vidogo vilivyopo karibu na pale anapokunywa maji, chura ni miongoni mwa viumbe ambao huvutwa. Akiingia kwenye mkonga wa tembo hujibanza ukutani, na hivyo haendi pamoja na maji kwenye tumbo la tembo. Chura asili yake ni kupiga kelele. Baada ya muda chura huanza kupiga kelele akiwa ndani ya mkonga wa tembo. Tembo kwa hasira, huanza kubamiza mkonga wake kwenye miti na mawe kwa lengo la kumwua chura, lakini kinachochakaa ni mkonga wake ambao ndiyo mkono wake unaompa maisha. Mwishowe tembo hupoteza maisha.

Ukubwa wa nchi siyo hoja, itategemea huyo mdogo umemweka wapi. Kama umemweka kwenye moyo, hata uwe mkubwa namna gani, atakuangamiza.
DP kuchangia 60% ya bajeti yetu ni 30 years kutoka sasa. Wakati huo mengi yatakuwa yamebadilika na hatutamwitaji DP.
 
Wanaotufundisha umuhimu wa upendo, kadiri ya maagizo ya kitabu Kitakatifu cha Biblia, wanatuambia kuwa, Umpende mwenzako kama unavyojipenda mwenyewe. Sijawahi kuona wala kusikia kuwa kuna mahali imenenwa umpende mwenzako zaidi ya unavyojipenda mwenyewe. Na Mungu pekee yake ndiye aliupenda sana ulimwengu hata akamtoa mwanae wa pekee ili ulimwengu upone. Kwa mwanadamu, ni vigumu sana.

Napenda niamini maneno ya Mbarawa na wale wote wanaomwunga mkono kuwa mkataba wa bandari kati ya Serikali ya Tanzania na kampuni ya DP World ya Dubai, ndio mkataba mzuri kuliko yote ambayo tunayo, na kwamba DP ikishachukua bandari zote za Tanganyila:

1) Itakuwa mwisho wa tatizo la ajira kwa vijana wa Tanzania

2) Zaidi ya 60% ya bajeti itachangiwa na mapato ya bandari pekee. Na hivyo kwa sababu bajeti yetu 40% huwa inajazilizwa na misaada na mikopo. Kodi zetu zote toka viwandani, kwa wafanyakazi, wafanyabiashara, tozo, migodi, utalii, adhabu za barabarani, ushuru wa mazao na misitu huwa zinachangia 60%. Hii ina maana kutokana na ujio wa DP, bwana Mbarawa anataka kusema sasa tunaweza kufuta kodi, tozo na ushuru wote, na pengo likazibwa na DP pekee yake, halafu 40% iliyosalia tukaendelea kujazilizia kwa mikopo na misaada. Watanganyika wataishi bila ya bugdha ya kodi, tozo wala ushuru. Tanganyika itaingia kwenye orodha ya zile nchi chache sana Duniani ambazo wananchi wake hawalipi kodi yoyote! Neema kubwa hii toka DP iliyosababishwa na upendo wa pekee wa bwana Mbarawa na katibu wake Aisha Amour, wote wazanzibari.

Mahali panaposhangaza zaidi, Mbarawa na Amour, wote wazanzibari, nyumbani kwao kwa asili ambako wapo wazazi wao, wajomba zao, mabibi zao, mabinamu zao, shemeji zao, wapwaa zao, ni Zanzibar. Wakati wakionesha upendo wa pekee ambao haujawahi kutokea Duniani, kwa watanganyika, wamekosa kabisa upendo kwa ndugu zao wa damu waliopo Zanzibar. Wakaamua ndugu zao wa damu kule Zanzibar, wasinufaike kabisa na hizo neema za pekee wanazotuambia zinaambatana na ujio wa DP. Wakaamua kuziweka bandari zote za Zanzibar, nje ya mkataba. Watu hawa wana chuki kubwa sana kwa ndugu zao wa damu!!

Hawa waheshimiwa, baada ya kuhudumu kwenye serikali ya JMT, watarudi nyumbani kwao, kwa ndugu zao wa damu, waliowatenga na neema za DP!! Maana yake wameamua kuwapenda watanganyika kuliko wanavyojipenda wenyewe? Jamani ni upendo ulioje huu? Ndiyo maana wengine wamesema kuwa watu hawa wapambwe kwa maua ya dhahabu.

Jibu lisipokuwa la ndiyo, basi itamaanisha watu hawa wanawachukia mno Watanganyika, kiasi cha kuamua kuwaletea watanganyi chatu awameze, wakati kwa upendo mkubwa na wa upendeleo, wakiwalinda jamaa zao wa damu kwa kuwaweka mbali na chatu, ili hata siku wakirudi nyumbani, wawaambie ndugu zao, "angalieni ndugu zetu tulivyowalinda, hata tukawaweka mbali na gharika ili msiangamie. Tumewaokoa, tumedhihirisha ni namna gani chura ana uwezo wa kumwua tembo. Tuwadogo, tuwachache, lakini tumemwangamiza mkubwa, tumewatia utumwani walio wengi"

Kwa wasiojua ni kwa namna gani chura humwua tembo: Chura hukaa kwenye maji, hasa madimbwi na mabwawa. Tembo kwa sababu mkonga wake ni mkubwa, anapoenda kunywa maji huvuta vitu vyote vidogo vidogo vilivyopo karibu na pale anapokunywa maji, chura ni miongoni mwa viumbe ambao huvutwa. Akiingia kwenye mkonga wa tembo hujibanza ukutani, na hivyo haendi pamoja na maji kwenye tumbo la tembo. Chura asili yake ni kupiga kelele. Baada ya muda chura huanza kupiga kelele akiwa ndani ya mkonga wa tembo. Tembo kwa hasira, huanza kubamiza mkonga wake kwenye miti na mawe kwa lengo la kumwua chura, lakini kinachochakaa ni mkonga wake ambao ndiyo mkono wake unaompa maisha. Mwishowe tembo hupoteza maisha.

Ukubwa wa nchi siyo hoja, itategemea huyo mdogo umemweka wapi. Kama umemweka kwenye moyo, hata uwe mkubwa namna gani, atakuangamiza.
Sasa wewe logic yako hapo Mzanzibar au Mpemba akitaka kujenga Tanzania nzuri lazima kwanza ajenge Pemba au Zanzibar? Nyerere hakujenga Musoma, alijenga Zaidi sehemu zenye economic priority, hakupenda Musoma?.

Halafu hizi name calling ati Mzanzibar au Mpemba zinatoka wapi, ok, hata akiwa Mpemba au Mzanzibar hawezi kufanya kosa?. Kwa nini usiende mbali useme madhara ya DPW kupewa hiyo bandari labda ni rushwa au ya Mbarawa kuwa unreasonable kwa thinking yake na siyo Upemba?

Ukiona unaanza kuweka wegde kwa kugawa watu ujue umekuwa mufilisi! Mbarawa Ntanzania kama wewe.

Mie napenda sana DPW waje kwa sababu hiyo bandari imekaa miaka yote kuwa ni chimbuko la rushwa tu.
Ila sipendi kwa kuwa sovereign kama inapotea vile, lakini ndiyo hivyo uwezohatuna, hii ni kweli .

CCM hakuna kitu wanachoweza ndiyo maana tupo hapa leo, na huyu mtawala wa sasa ni kusikiliza kila kitu, YULE mwamba kwa mambo kama haya nilikuwa namuamini alikuwa hatanii. Ingawa-----
 
Sasa wewe logic yako hapo Mzanzibar au Mpemba akitaka kujenga Tanzania nzuri lazima kwanza ajenge Pemba au Zanzibar? Nyerere hakujenga Musoma, alijenga Zaidi sehemu zenye economic priority, hakupenda Musoma?.

Halafu hizi name calling ati Mzanzibar au Mpemba zinatoka wapi, ok, hata akiwa Mpemba au Mzanzibar hawezi kufanya kosa?. Kwa nini usiende mbali useme madhara ya DPW kupewa hiyo bandari labda ni rushwa au ya Mbarawa kuwa unreasonable kwa thinking yake na siyo Upemba?

Ukiona unaanza kuweka wegde kwa kugawa watu ujue umekuwa mufilisi! Mbarawa Ntanzania kama wewe.

Mie napenda sana DPW waje kwa sababu hiyo bandari imekaa miaka yote kuwa ni chimbuko la rushwa tu.
Ila sipendi kwa kuwa sovereign kama inapotea vile, lakini ndiyo hivyo uwezohatuna, hii ni kweli .

CCM hakuna kitu wanachoweza ndiyo maana tupo hapa leo, na huyu mtawala wa sasa ni kusikiliza kila kitu, YULE mwamba kwa mambo kama haya nilikuwa namuamini alikuwa hatanii. Ingawa-----
Ndugu yangu umekuwa mfilisi sana wa uelewa.

Hivi unaelewa wizara za Muungano?

Wizara za Muungano zipo ngapi? Zitaje.

Wizara ambayo Mbarawa ni waziri ni ya Muungano au siyo ya Muungano?

Kama siyo ya Muungano, imekuwaje Rais kumweka mzanzibari kwenye wizara ya Tanzania bara?

Hivi kumwita mtu mzanzibari kuna kosa gani?

Unajua kuwa nchi yetu ina watu wenye urai wa aina ngapi?

Unataka kusema Rais aliposema yeye ni mzanzibari alikuwa amekosea?

Umewahi kuisoma katiba ya Zanzibar?

Katiba ya nchi ya Zanzibar, inatamka kuwa mipaka ya nchi ya Zanzibar ni ipi?

Raia wa nchi ya zanzibar, kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar, anaitwa nani?

Yaani watu ambao hamjui chochote, mnajiona mmefikia kuwa walimu.
 
Back
Top Bottom