Upepo Ukipuliza Waya Zikagongana Pale Ubungo Umeme Unakatika

Upepo Ukipuliza Waya Zikagongana Pale Ubungo Umeme Unakatika

Faana

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2011
Posts
38,657
Reaction score
44,759
Mada inajieleza, hayo maneno yalisikika yakitoka kinywani mwa mtu mwenye dhamana ya kutupa moto mara moja, nimejiuliza maswali;
  1. Wakati wa ujenzi wa hizo line, wahandisi, designers wa hizo power lines hawakujua kuwa kuna upepo hivyo wazingatie spacing ya waya?
  2. Miaka yote upepo umekuwa ukivuma na waya hazigongani na kama zilikuwa zinagongana je hapakuwepo namna ya kuondoa hilo tatizo? Hao wataalamu wanafanya kazi gani?
  3. Je ni Tanzania peke ilipotumika teknolojia iliyopo hapo Ubungo zinapogongana waya na kusababisha umeme ukatike?
  4. Ina maana wataalamu walipoweka hizo waya hawakujua kuwa zipo uchi wachukue tahadhari ili kuziepusha na migongano wanayoitaja
  5. Huo upepo mkali unaosababisha huo usumbufu umekuja na kiongozi kama yule mwingine alivyotuletea solar eclipse kule Rujewa Meya na Wanging'ombe Njombe?
YAjayo yanafurahisha.
ongezeni maswali mengine
 
Ni Tanzania tu ambapo std 7, anaweza kumpinga injinia aliyebobea kwenye umeme na kumuona zuzu!!!
 
Asante sana Mods kwa kunirekebishia heading maana tumbo lilikuwa moto nilijua naanza kurushiwa mawe
 
Walioweka hizo nyaya ni watu wenye akili zao, na ni dunia nzima ziko hivyo, sasa leo mtu mwenye elimu ndogo, anakuja kuwaona mainjinia ni wajinga, eti upepo ukipuliza tu, nyaya zitagusana!!
Hahahhah[emoji23] zinagusana ndugu.../

Walisha tuchukulia sisi ni mazezeta[emoji23][emoji23]
 
Alisema inatokea conduction, halafu alivo mweupe kichwani anajifichwa kwenye kivuli ooohh hamkupenda mama samia awe Rais au mimi kua waziri kwa mara ya kwanza nilimshusha thamani ni waziri mwenye uwezo mdogo sana sana.
 
Alisema inatokea conduction, halafu alivo mweupe kichwani anajifichwa kwenye kivuli ooohh hamkupenda mama samia awe Rais au mimi kua waziri kwa mara ya kwanza nilimshusha thamani ni waziri mwenye uwezo mdogo sana sana.
Aliongea kikujiaibisha sana
 
Ni Tanzania tu ambapo std 7, anaweza kumpinga injinia aliyebobea kwenye umeme na kumuona zuzu!!!
Ni Tanzania tu ambapo std 7 anakua na ubunifu kuliko engineer mwenye masters.
Tusiende mbali. Njoo hata barabara ya Maramba mawili. Ma engineer wamefuatia mule mule Wana Kijiji walipowaelekeza. Ndio maana barabara Ina black spot nyingi kupita kiasi kuanzia hii ya Msigani.
 
Nilimsikiliza nikaona huyu jamaa janja janja nyingi
 
Nilimsikiliza nikaona huyu jamaa janja janja nyingi
 
Back
Top Bottom