janjab
Senior Member
- May 28, 2015
- 172
- 56
Nina mkopo wa nmb ambao umebaki kiasi cha tzs 2,031,474.10 ambapo niliamua kwenda crdb kuona kama wanaweza kununua deni hivyo nilifika na afisa mikopo alinipigia hesabu akanambia naweza kupata tzs 9,500,000 ambapo akanipa barua ya kuomba balance ili mkopo wangu nikipewa kiasi cha pesa kingine kitumike kulipa mkopo, nmb pia makato akanambia yatakuwa 231000 kila mwezi,alinambia pia kuna makato ya bima na ya proces za mkopo bima alinambia 118000 nilipa hesab nikaona napata kama m.7 na laki kadhaa baada ya makato yote..........baada ya hapo nilienda nmb kuona nao wananambiaje nilipofika afisa mikopo alipiga hesabu akanambia kuwa naweza kupata 11,300,000 toa deni langu ambalo ni 2,031,474.10 na bima +fedha ya kuprocess mkopo ambayo ni kama 769548.14 wakanambia naweza kupata net tzs 8.498.977.76 baada ya makato yote na makato kwa mwez ni 245,117.80 na nalipa kwa miaka sita.swali langu ni je? Kwa mchanganuo huo hapo juu ni bank gani naweza kuchukua mkopo kati ya hizo hapo juu kat ya nmb na crdb