Upi Mkakati wa Tanzania kutengeneza Ownership ya Parachichi kwa kuanza kuzibrand kama product ya Tanzania?

Upi Mkakati wa Tanzania kutengeneza Ownership ya Parachichi kwa kuanza kuzibrand kama product ya Tanzania?

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Mbunge wa Jimbo la Makete, Mhe Festo Sanga amehoji Bungeni leo kuhusu Soko la Parachichi.

Namnukuu:

"Soko la Parachichi Duniani linasomeka parachichi zinazalishwa Nchi jirani ya Kenya, ili hali Parachichi asilimia zaidi ya 50 zinazotoka Ukanda huu wa Africa Mashariki zinatoka Tanzania, Wanunuzi wanazibrand kama zinatoka nchi jirani na sio Tanzania.

Upi Mkakati wa Tanzania kutengeneza-Ownership (Umiliki) wa Soko la Parachichi kwa kuanza kuzibrand kama product ya Tanzania"?. Mwisho wa kunukuu.

Majibu ya Waziri wa Kilimo, Mhe Hussein Bashe, yameonesha kuna mpango wa Serikali kuanzisha common use facilities kwa ajili ya kuanza kuziprocess parachichi na kuziandika kuwa zinatokea Tanzania.

Lakini, amekiri kuwa ni kweli parachichi zimekuwa zikinunuliwa kama raw materials na kwenda kuandaliwa vizuri huko nje kisha kuwa branded na nchi husika.

My Take: Tulichelewa sana kwenye hili. Mbunge Sanga amefanya vizuri kulipambania. Tuhamie na kwenye mazao mengine pia.
 
Sio parachichi pekee. Ni vitu vingi sana vinaenda Kenya kisha vinakuwa vinakuwa packed au processed kisha kuuzwa kwa bei nzuri huko ulaya, uarabuni na nchi zingine.

Chanzo ni masuala mawili, sheria za nchi yetu zinaleta urasimu ambao ni vigumu kushindana kimataifa. Pili urahisi wa kupata mtaji wa kufanya hiyo biashara.

Kuexport bidhaa inabidi uwe na pesa ya kutosha pia inabidi upate international standards certificate za ISO mpaka utambulike na EU, USA sio kitu cha mzahamzaha mtaji wa jengo tu la kuprocess, kulipa wafanyakazi mishahara, mitambo ya kuprocess,kukusanya mazao, kununua ardhi ni mamilioni ya pesa kama sio mabilioni

NB: Tanzania uaminifu ni 0. Usije ukashangaa huo mradi wa Common use facility watu wakapiga hela halafu mradi usifanyike
 
Hapa tukipaweza basi jirani ataona vumbi tuu, maana sie tumekuwa kama shambani na biashara ipo kwa jirani.
 
Sio parachichi pekee. Ni vitu vingi sana vinaenda Kenya kisha vinakuwa vinakuwa packed au processed kisha kuuzwa kwa bei nzuri huko ulaya, uarabuni na nchi zingine.
Chanzo ni masuala mawili, sheria za nchi yetu zinaleta urasimu ambao ni vigumu kushindana kimataifa. Pili urahisi wa kupata mtaji wa kufanya hiyo biashara. Kuexport bidhaa inabidi uwe na pesa ya kutosha pia inabidi upate international standards certificate za ISO mpaka utambulike na EU, USA sio kitu cha mzahamzaha mtaji wa jengo tu la kuprocess, mitambo,kukusanya mazao, kununua ardhi ni mamilioni ya pesa kama sio mabilioni



NB: Tanzania uaminifu ni 0. Usije ukashangaa huo mradi wa Common use facility watu wakapiga hela halafu mradi usifanyike
Hilo sasa ndiyo jukumu la serikali kulisimamia

Ova
 
Waanze na standardization, jamaa lazima waje wacheki mnavoprocess izo parachichi
 
Avocado zinauzwa vizuri zikiwa nzima, sijui ni process gani inayotakiwa zaidi ya kuziweka kwenye box na kuweka label kuwa zimetoka Tanzania kama hizi za Mexico zinavyouzwa kwenye soko la Marekani kila moja kwa dola mbili na nusu.

Process kama kutengeza mafuta, jam au ungwa wa avocado hazina faida kama kuyauza yakiwa mabichi. Mara nyingi process hizo ni kwa yale maparachichi ambayo yanakaribia kuharibika tu.

1649850483892.png
 
Avocado zinauzwa vizuri zikiwa nzima, sijui ni process gani inayotakiwa zaidi ya kuziweka kwenye box na kuweka label kuwa zimetoka Tanzania kama hizi za Mexico zinavyouzwa kwenye soko la Marekani kila moja kwa dola mbili na nusu. Process kama kutengeza mafuta, jam au ungwa wa avocado hazina faida kama kuyauza yakiwa mabichi. Mara nyingi process hizo ni kwa yale maparachichi ambayo yanakaribia kuharibika tu.
View attachment 2186123
Haya si kama ya pale kibanda cha matunda kwa mtumishi tu.
 
My Take: Tulichelewa sana kwenye hili. Mbunge Sanga amefanya vizuri kulipambania. Tuhamie na kwenye mazao mengine pia.
  1. Mafanikio yatakuwepo tukichukua tahadhari kuingiza siasa kwenye huo mpango
  2. Diplomasia ipewe nafasi kubwa wakati wa kutafuta/kuteka hilo soko yasitukute ya choroko, korosho nk
  3. Kuanzishwe chombo maalumu cha kudhibiti ubora unaokidhi viwango vya kimataifa na kiwe na watendaji waadilifu sana.
  4. Wakulima wawekewe mazingira bora ya kuzalisha hilo zao katika viwango sahihi
 
Mbunge wa Jimbo la Makete, Mhe Festo Sanga amehoji Bungeni leo kuhusu Soko la Parachichi.

Namnukuu:

"Soko la Parachichi Duniani linasomeka parachichi zinazalishwa Nchi jirani ya Kenya, ili hali Parachichi asilimia zaidi ya 50 zinazotoka Ukanda huu wa Africa Mashariki zinatoka Tanzania, Wanunuzi wanazibrand kama zinatoka nchi jirani na sio Tanzania.

Upi Mkakati wa Tanzania kutengeneza-Ownership (Umiliki) wa Soko la Parachichi kwa kuanza kuzibrand kama product ya Tanzania"?. Mwisho wa kunukuu.

Majibu ya Waziri wa Kilimo, Mhe Hussein Bashe, yameonesha kuna mpango wa Serikali kuanzisha common use facilities kwa ajili ya kuanza kuziprocess parachichi na kuziandika kuwa zinatokea Tanzania.

Lakini, amekiri kuwa ni kweli parachichi zimekuwa zikinunuliwa kama raw materials na kwenda kuandaliwa vizuri huko nje kisha kuwa branded na nchi husika.

My Take: Tulichelewa sana kwenye hili. Mbunge Sanga amefanya vizuri kulipambania. Tuhamie na kwenye mazao mengine pia.
Ni miaka mingi sana Kenya imekuwa ikiuza parachichi wakati huku watu walikuwa hawayajui, parachichi limeanza kujulikana baada 2000.
 
Sio parachichi pekee. Ni vitu vingi sana vinaenda Kenya kisha vinakuwa vinakuwa packed au processed kisha kuuzwa kwa bei nzuri huko ulaya, uarabuni na nchi zingine.

Chanzo ni masuala mawili, sheria za nchi yetu zinaleta urasimu ambao ni vigumu kushindana kimataifa. Pili urahisi wa kupata mtaji wa kufanya hiyo biashara.

Kuexport bidhaa inabidi uwe na pesa ya kutosha pia inabidi upate international standards certificate za ISO mpaka utambulike na EU, USA sio kitu cha mzahamzaha mtaji wa jengo tu la kuprocess, kulipa wafanyakazi mishahara, mitambo ya kuprocess,kukusanya mazao, kununua ardhi ni mamilioni ya pesa kama sio mabilioni

NB: Tanzania uaminifu ni 0. Usije ukashangaa huo mradi wa Common use facility watu wakapiga hela halafu mradi usifanyike
Hakuna taifa lenye watu wapuuzi kama Tanzania. Daraja la Tanzanite halina hata miezi mitatu tangu lifunguliwe na watu wameshaanza kuiba vyuma!.

Hayo yote uliyoyaongea yanataka watu wanaojifahamu wenye uelewa na maono mapana vichwani mwao.
 
Nyie si mmelala

Serikali za wenzetu wanazunguka nje

Kuwatafutia masoko watu wao

Je serikali yetu inatufNyia hivyo au ?

Ova

Tatizo wanaona wakitoa vibali sijui tutafaidi sana

Yaani masoko ya duniani ukiangalia huwezi kuona produce za Tz wasitudanganye ooh brand
Brand my [emoji3097]
Watoe vibali waone
Sokoni Ulaya unakuta matunda na mboga za nchi nyingi na Kenya Ndio kibao na Uganda pia wanaleta sana

Hivi hata pilipili wanashindwa kutoa kibali ?
Bashe anajua yote aache danadana zake
Waswahili maneno mengi tu
 
Tatizo wanaona wakitoa vibali sijui tutafaidi sana

Yaani masoko ya duniani ukiangalia huwezi kuona produce za Tz wasitudanganye ooh brand
Brand my [emoji3097]
Watoe vibali waone
Sokoni Ulaya unakuta matunda na mboga za nchi nyingi na Kenya Ndio kibao na Uganda pia wanaleta sana

Hivi hata pilipili wanashindwa kutoa kibali ?
Bashe anajua yote aache danadana zake
Waswahili maneno mengi tu
Vibari vipo na inawezekans,sema hapa inataka ndoa halali kabisa na mzungu na taka taka zake zote.
 
Vibari vipo na inawezekans,sema hapa inataka ndoa halali kabisa na mzungu na taka taka zake zote.

Mziki wake unaujua na kuna ofisi ngapi upite?
Mzungu hana neno kabisa tena zinaingia bila tatizo na hili nalijua vizuri sana
 
Back
Top Bottom