Upigaji Kura za Maoni utakuwaje?

Gurtu

JF-Expert Member
Joined
May 15, 2010
Posts
1,248
Reaction score
342
Kwa wale tulizoea upigaji kura katika enzi ya vyama vingi, tofauti na wakati wa Mwl. Nyerere ambapo kulikuwa na kupiga kura ya ndiyo na hapana kwa ngazi ya urais, ni jambo la kawaida kuwa kila mgombea wa chama humweka wakala wa kusimamia kura zake hasa wakati wa kuhesabu. Baada ya kura zote kuhesebiwa na kujumlishwa wakala pamoja na mgombea husaini fomu ya matokeo katika ngazi husika. jambo kubwa linalohakikshwa hapo ni kuwa kila mgombea anatendewa haki na kwamba kura zake hazichakachuliwe kwa mfano kupewa mgombea mwingine.

Katika upigaji wa kura za maoni kutakuwa na pande mbili zitakazokuwepo, yaani watakaopiga kura ya "hapana" na watakaopiga kura ya "ndiyo". Kwa hakika kila upande utapenda kuamini kuwa msimamizi atende haki kwa kuheshimu maamuzi ya kila mpiga kura. kati enzi yetu hii ambayo tume yenyewe ya uchaguzi haiaminiki, ni utaratibu upi wa kuhakikisha kuwa kura ya kila mtu itakuwa salama? Je, kutakuwa na utaratibu wa kuwepo mawakala, na mwakala halali watapatikanaje?
 
Hapo umenena maana hatuwezi kupata matokeo sahihi ya kura hizo kwa kuwa tume ya buchaguzi ya sasa ndiyo itakayosimamia kura hizo wakati rasimu inaitaka tune hiyo iondolewe na badala yale iundwe tume HURU ya uchaguzi, Yaani tune ya sasa kukubali kuwa rasimu imekubaliwa na wengi, ni kujipiga nyundo yenyewe kwa kuwa rasimu ikipita itaundwa tume huru, siyo hii ya sasa! Je wanaweza kujipiga nyundo? ukitilia maanani kuwa rasimu hii ikikataliwa basi katiba ya zamani ndiyo itaendelea kutumika! Nadhani umenielewa mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…