Upigaji kwenye EFD na mashine za kutolea risiti inazotaka TRA

Upigaji kwenye EFD na mashine za kutolea risiti inazotaka TRA

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Nani asiyezijua mashine za EFD au hizi zinazotumiwa na jamaa wa parking au kwenye malipo mbalimbali?

Mashine hizi sasa ni takwa la kisheria kwa wafanya biashara vinginevyo hakuna kufanya biashara.

Uliza bei za hizo mashine. Si ajabu kusikia 600,000/- kwa moja na malipo lukuki ya mwezi kwa matumizi.

Kwamba serikali inakopeshwa mashine hizi kwa bei inflated na wananchi hawa ambao ni maskini mno wenye kusongwa na mizigo ya tozo? Kwamba kumbe eti mashine hizi ni mali ya serikali?

Kwanini serikali isizinunue yenyewe mashine hizi na kuwagawia watu badala ya kuwalazimisha kuikopesha?

Kwanini mashine hizi kama ni muhimu kwa serikali zilipiwe na serikali kwa bei ambazo ni za kitapeli?

Kwanini kama zi muhimu kiasi hicho serikali isizilete mashine hizo kwa bei zake halisi kutokea China huko?

Tutaendelea kupigwa na kunyonywa kiujanja ujanja hivi na walamba asali hadi lini?

Mnapotakiwa kuachia ngazi tambueni mna makando kando mengi. Wachawi ni nyie wenyewe.
 
Huo utakuwa mradi wa wakubwa serikalini, siku hizi wanatumia nafasi zao kwenye ofisi za umma kufanya biashara wazi bila uoga wowote.

Hapo kinachotokea, serikali itakuwa inapata kidogo na kingine wanachukua hao wajanja, taifa linazidi kuangamia kila siku na wananchi hawana wa kumlilia tena.
 
Huo utakuwa mradi wa wakubwa serikalini, siku hizi wanatumia nafasi zao kwenye ofisi za umma kufanya biashara wazi bila uoga wowote.

Hapo kinachotokea, serikali itakuwa inapata kidogo na kingine wanachukua hao wajanja, taifa linazidi kuangamia kila siku na wananchi hawana wa kumlilia tena.

Bahati mbaya ni kuwa kama taifa kila mtu anajiangalia yeye. Basi humo humo.kila mmoja anapigika kivyake.

Fikiria laki 6 kwa ki machine cha kulipia parking. Vipi TV Hisense ya laki 6? Pana cha kushabihiana?

Wizi mtupu!
 
Back
Top Bottom