Salam wanabodi,
Upigaji wa fedha za wazazi ni upigaji unaofanywa na baadhi ya viongozi wa kamati za wazazi katika shule za serikali hasa za sekondari. Karibia kila shule wazazi wamefungua account bank kwa ajili ya michango ya chakula cha watoto shuleni, mpishi, walinzi, walimu wa masomo ya sayansi, kwa makubaliano yao. Wakachagua kamati yenye Mwenyekiti, Katibu, Mweka Hazina na Mjumbe mmoja na wote wanakuwa watia saini benki katika hiyo account na ndio wenye mamlaka ya kutoa pesa kwenye hizo account kwa ajili ya malipo.
Sijui Sheria za fedha za umma zinasemaje lakini hizi account hazikaguliwi. Siyo ukaguzi wa ndani wala wa nje; mwaka mmoja, miwili, mitatu, minne, na kuendelea hazikaguliwi na ni account zinazopokea mpaka Tsh. milioni mia moja na kuendelea kwa mwaka toka kwa wazazi lakini hakuna ukaguzi (auditing).
Tatizo linakuja watoto hupeleka bank slips shuleni kuonyesha malipo yaliyolipwa na wazazi wao kwenye account lakini wanapata huduma duni ya chakula na hakuna mwalimu wa kuwatetea maana hawahusiki na upatikanaji wa chakula hicho, hata wazazi hawawezi kuhoji chochote maana hawasomewi mapato na matumizi kwenye vikao inabaki tu "Kama unataka mwanao ale, lipa hutaki usilipe".
Lakini pia pindi wapishi, walinzi na walimu wa sayansi wanahitaji mishahara huenda kudai kwa Mkuu wa Shule maana wameingia mkataba na Shule. Kulingana na bank slips za watoto zinaonyesha pesa zipo kwenye account lakini viongozi wanasema hakuna pesa na kuanza kupiga chenga huku anayesumbuliwa ni Mkuu wa Shule na yeye Wala walimu wake siyo watia Saini kwenye account hizo.
Wapo baadhi ya viongozi wanaosimamia account hizo wamekuwa miungu watu; wanakoromea walimu, wanakoromea wazazi wenzao, hawamsikilizi mkuu wa shule, na wengine unakuta ni viongozi wa CCM. Wakati wa kuchagua viongozi hao, wao hutumia ujanja wa kuwa wasemaji na wajuaji kwenye vikao ili wachaguliwe lakini Wana mipango Yao.
Hata watoto wao wanapohitimu masomo katika shule husika, Bado huazima watoto wa watu wengine na kujidai ni watoto wao au wa ndugu zao wanawasaidia ili tu wasitoke kwenye hizo nafasi za uongozi. Uendeshaji wa hizi account umegubikwa na upigaji wa fedha za chakula Cha watoto toka kwa wazazi huku huduma zikiwa duni sababu hazikaguliwi na hata hao walimu Wanaweza wakafanya kazi miezi hata mitatu hawajalipwa lakini fedha zinaonekana zimewekwa kwenye account. Hivyo kuwepo kwa migogoro ya chini chini kwenye hizo shule.
USHAURI: Mwajiri aweke utaratibu wa kukagua hizo account kila mwaka kwa maslahi ya umma ili kuboresha huduma na kuondoa hiyo migogoro ya chini kwa chini.
Au, Baraza la Waheshimiwa Madiwani chini ya Mkurugenzi na Kamati Yao ya Fedha na Uchumi wakubaliane watafute kampuni (private entity) ya kukagua hizo account kila mwaka na taarifa ipelekwe kwenye Baraza ili wale wanaokula pesa za chakula cha watoto wachukuliwe hatua stahiki. Na hao viongozi wanaotafuta nafasi za kusimamia account hizo bora walipwe posho na hao wazazi kuliko kujifanya wanajitolea halafu wanaenda kuwa wapigaji na wezi.
Naomba kuwasilisha.
Upigaji wa fedha za wazazi ni upigaji unaofanywa na baadhi ya viongozi wa kamati za wazazi katika shule za serikali hasa za sekondari. Karibia kila shule wazazi wamefungua account bank kwa ajili ya michango ya chakula cha watoto shuleni, mpishi, walinzi, walimu wa masomo ya sayansi, kwa makubaliano yao. Wakachagua kamati yenye Mwenyekiti, Katibu, Mweka Hazina na Mjumbe mmoja na wote wanakuwa watia saini benki katika hiyo account na ndio wenye mamlaka ya kutoa pesa kwenye hizo account kwa ajili ya malipo.
Sijui Sheria za fedha za umma zinasemaje lakini hizi account hazikaguliwi. Siyo ukaguzi wa ndani wala wa nje; mwaka mmoja, miwili, mitatu, minne, na kuendelea hazikaguliwi na ni account zinazopokea mpaka Tsh. milioni mia moja na kuendelea kwa mwaka toka kwa wazazi lakini hakuna ukaguzi (auditing).
Tatizo linakuja watoto hupeleka bank slips shuleni kuonyesha malipo yaliyolipwa na wazazi wao kwenye account lakini wanapata huduma duni ya chakula na hakuna mwalimu wa kuwatetea maana hawahusiki na upatikanaji wa chakula hicho, hata wazazi hawawezi kuhoji chochote maana hawasomewi mapato na matumizi kwenye vikao inabaki tu "Kama unataka mwanao ale, lipa hutaki usilipe".
Lakini pia pindi wapishi, walinzi na walimu wa sayansi wanahitaji mishahara huenda kudai kwa Mkuu wa Shule maana wameingia mkataba na Shule. Kulingana na bank slips za watoto zinaonyesha pesa zipo kwenye account lakini viongozi wanasema hakuna pesa na kuanza kupiga chenga huku anayesumbuliwa ni Mkuu wa Shule na yeye Wala walimu wake siyo watia Saini kwenye account hizo.
Wapo baadhi ya viongozi wanaosimamia account hizo wamekuwa miungu watu; wanakoromea walimu, wanakoromea wazazi wenzao, hawamsikilizi mkuu wa shule, na wengine unakuta ni viongozi wa CCM. Wakati wa kuchagua viongozi hao, wao hutumia ujanja wa kuwa wasemaji na wajuaji kwenye vikao ili wachaguliwe lakini Wana mipango Yao.
Hata watoto wao wanapohitimu masomo katika shule husika, Bado huazima watoto wa watu wengine na kujidai ni watoto wao au wa ndugu zao wanawasaidia ili tu wasitoke kwenye hizo nafasi za uongozi. Uendeshaji wa hizi account umegubikwa na upigaji wa fedha za chakula Cha watoto toka kwa wazazi huku huduma zikiwa duni sababu hazikaguliwi na hata hao walimu Wanaweza wakafanya kazi miezi hata mitatu hawajalipwa lakini fedha zinaonekana zimewekwa kwenye account. Hivyo kuwepo kwa migogoro ya chini chini kwenye hizo shule.
USHAURI: Mwajiri aweke utaratibu wa kukagua hizo account kila mwaka kwa maslahi ya umma ili kuboresha huduma na kuondoa hiyo migogoro ya chini kwa chini.
Au, Baraza la Waheshimiwa Madiwani chini ya Mkurugenzi na Kamati Yao ya Fedha na Uchumi wakubaliane watafute kampuni (private entity) ya kukagua hizo account kila mwaka na taarifa ipelekwe kwenye Baraza ili wale wanaokula pesa za chakula cha watoto wachukuliwe hatua stahiki. Na hao viongozi wanaotafuta nafasi za kusimamia account hizo bora walipwe posho na hao wazazi kuliko kujifanya wanajitolea halafu wanaenda kuwa wapigaji na wezi.
Naomba kuwasilisha.