Upishi wa tembele unanishinda mwenzenu

Upishi wa tembele unanishinda mwenzenu

Kikalove

Senior Member
Joined
Feb 25, 2015
Posts
163
Reaction score
35
Kila nikijaribu kupika tembele nashindwa mwenzenu mara maji mengi, nisipoweka naunguza, mara limelepweta eti nakoroga badala ya kugeuza shida tupu.

Nisaidieni mwenzenu.
 
chambua tembele lako vizuri'kisha lioshe ,liweke kwenye kifaa lichuje maji'andaa nyanya kulingana na kias cha tembele.weka kifaa chako cha kupikia jikoni,tia mafuta kiasi,tia kitunguu ,geuza mpaka viwe kahawia'mimina nyanya zako ulizozikatakata,tia tembele lako halafu funika baada ya dkk tatu geuza taratibu .tia chumvi na limao kidogo subiri baada ya dkk nne ..tembele lako litakuwa tayari
 
Yaani katika mboga ambazo sizipendi hayo majani hayo majani siyapendi...ni bora nile ugali kwa chumvi...kuliko kula ugali na hayo makitu hasa ile migingi yake ya nyuma dahh.......
 
Chukua tembele lichambue vizuri halafu liweke kidogo juani ili lisinyae kidogo(sio lazima) baada ya hapo weka kikaangio chako tia vitunguu ndani ya mafuta then nyanya kisha tembele.Usifunike maana litakua na maji maana ya ule mvuke wa kufunikwa
 
tembele lichambue vizuriii osha uhakikishe halina mchanga bandika sufuria jikoni weka mafuta kaanga kitunguu maji kikianza kubadilika rangi weka nyanya kaanga kidogo weka chumvi kiasi nyanya zikishalainika weka tembele koroga lichanganyike acha vichemke huku unakoroga kiasi had maji yakaukie unaweza kuweka ndimu au limau ukakamulia kama unapenda mana wengine hawapendi kuweka hii koroga kuchanganya limao au ndim onja jani moja wapo kama limeiiva au mti wake ila sipendag tembele liive sana likikauka nikiona linafaa kuteguliwa nategua kama unaona bado nyunyizia maji kidogo liive baada ya hapo kazi kwako
 
Yaani katika mboga ambazo sizipendi hayo majani hayo majani siyapendi...ni bora nile ugali kwa chumvi...kuliko kula ugali na hayo makitu hasa ile migingi yake ya nyuma dahh.......
Kumbe tuko wengi namimi pia ni hivyo hivyo lakini mwenzio taste yake inanishinda na sijui swali la huyu jamaa anamaanisha namna ya kuyapika yakiwa makavu au mabichi,mbona ni rahisi sana kuipika mboga yeyote ya majani.Kama ni makavu chukuwa vitunguu uvikatekate na nyanya na kama ni mtumiaji wa pili pili weka mbichi moja na tena weka mafuta ktk sufuria yako then anza kuvikaanga hivyo vitunguu pamoja na nyanya mpaka vibadilike rangi then itupie mboga yako ndani ya hilo sufuria uichanganye na kwa pamoja na hivyo vitunguu na nyanya zilizoivya changanya kidogo kidogo na mwiko wako na halafu ongeza maji kidogo na kama una stock yeyote aidha ya kuku au nyama yenye chumvi ndani yake ongezea ili upate mchuzi na kama unayo tomato paste pia unaweza tia ili upate chuzi zito,weka lid juu ya sufuria halafu punguza moto ili iive pole pole kwa moto mdogo,mboga yako tayari kwa kulia na ugali bona apetit!!.Mr Msherwampamba:canada:
 
Chukua tembele lichambue vizuri halafu liweke kidogo juani ili lisinyae kidogo(sio lazima) baada ya hapo weka kikaangio chako tia vitunguu ndani ya mafuta then nyanya kisha tembele.Usifunike maana litakua na maji maana ya ule mvuke wa kufunikwa
Mama yangu ndiyo analipika hivyo hivyo. Yeye anaweka na pili pili pia.
 
MI huwa nikishaliosha na kulikausha maji vizuri, naunga mchuzi wa nyanya mzito afu naziweka, baada ya km dk mbili nageuza ili zishiungulie chini, naweka chumvi naacha kidogo,siivishi muda mrefu natoa jikoni,limao/ndimu sie huwa tunawekea mezani
Another option ni nakaanga kitunguu naweka Tembele nalikaanga wee likilainika flani hivi naweka chumvi, nyanya na carrot nachanganya nafunika,km baada ya dk 5/10 nakuja kugeuza napondaponda nyanya zilizobaki kuwa ngumu bado kama zipo then naipua
 
One of my favorite vegetables na ugali dagaa hivi ,nikiona majani yale km marefu hivi kuwa nakatakata km japo sio vidogo
 
Back
Top Bottom