Uchaguzi 2020 Upotoshaji wa makusudi dhidi ya Tundu Lissu

Uchaguzi 2020 Upotoshaji wa makusudi dhidi ya Tundu Lissu

Wamkopeka

Senior Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
136
Reaction score
308
Tukiwa tumebakiwa na wiki tatu tu Watanzania tupige kura kuchagua Rais, wabunge na madiwani.

Licha ya kuwa na wagombea 15 wa kiti cha Rais lakini mpaka sasa wenye nguvu ya ushawishi ni kutoka vyama viwili vya CCM na CHADEMA.

Lakini kumekuwepo na kutumia nguvu kubwa sana kujaribu kupotosha kauli ya mgombea wa CHADEMA kwenye kampeni zake.

Wapinzani wake mara nyingi wamekuwa wakipotosha kwamba anasema kwenye uchaguzi huu lazima yeye atangazwe mshindi na kwamba asipotangazwa basi ataingiza watu barabarani.

Wenye kueneza upotoshaji huu kwangu mimi nawafananisha na maadui wa taifa hili kwasababu wanajaribu kumjengea chuki ya makusudi Mh.Lissu ili aonekane yeye yupo kwa ajili ya kuleta vurugu.

Lakini haishangazi maana watu hao hao ndio wanasema Lissu ametumwa na Mabeberu, mara akishinda atauza nchi.

Hawa ni wapotoshaji ambao kwa kiasi kikubwa wametawaliwa na ubinafsi, unafiki, na uchu wa kutawala ambao lengo lake si kwa maslahi mapana ya nchi na wananchi wote bali wao na familia zao.

Lissu mara zote ameweka wazi msimamo wake kwamba pamoja na tume kutokuwa huru lakini anachotaka ni uchaguzi wa haki na huru. Kwa maana kwamba kusiwepo na mizengwe na figisu figisu kama ilivyozoeleka kwenye chaguzi zote. Amesema akishindwa kwa haki hatakuwa na shida na yeyote na atakuwa wa kwanza kukubali matokeo, kinyume chake anesema hakitaeleweka.

Sasa unajiuliza hawa wapotoshaji wanaogopa nini kuendesha uchaguzi wa huru haki na uwazi? Kama wanaamini wanakubalika sana kwa watanzania kwa namna wanavyoongoza nchi sasa hofu yao inatokana na nini?

Ukijaribu kuitafakari kauli yao kwamba Lissu ametumwa na Mabeberu na kwamba akishinda urais atauza nchi, yaani utagundua kuwa ni kauli ya kipuuzi iliyokosa maana kabisa.

Maana Lissu ni mtanzania kama walivyo wao, tofauti yao ni kwamba wakati Lissu amepambana kwa miaka 17 kutetea raslimali za nchi hii, hao wapotoshaji walikuwepo na hawajawahi kukemea au kusema lolote juu ya ujambazi unaofanyika kwenye raslimali asili zetu kwa baraka za ccm. Zaidi sana wakamuona Lissu kama anakwamisha maendeleo wakamfungulia kesi ili wafunge.

Lissu kwa miaka yote ameonekana kuwa adui mkubwa wa serikali ya CCM kwasababu ya msimamo wake wa kutetea raslimali za nchi hii. Mpaka sasa raslimali zetu zinaendelea kuwafaidisha hao wanaoitwa mabeberu kama walivyokabidhiwa na serikali ya ccm kupitia sera waliyoibatiza jina la wawekezaji..

Wapotoshaji hao hapo huwezi kuwasikia wakisema lolote.

Watanzania tuamke usingizini, hawa wenzetu wanachokipigania ni maslahi yao na ya familia zao. Wanaona ujio wa Lissu ni tishio kwao na kwamba akishinda hivyo madhambi yao yatawekwa wazi ndio maana wanapigana kufa na kupona kumzuia asishinde ili kulinda madhambi yao.

Mtazania shtuka.
 
Watanzania tuamke usingizini, wenzetu wanachokipigania ni maslahi yao na familia zao. Wanaona ujio wa Lissu ni tishio kwao na kwamba akishinda madhambi yao yatawekwa wazi ndio maana wanapigana kufa na kupona kumzuia asishinde ili kulinda madhambi yao.
 
Tume ingekuwa huru ilipaswa kuwaonya wagombea wanaompakazia mgombea mwingine kinyume na ukweli.

Lakini kwa vile kumesheheni makubwa jinga kama yule bwana manoti wao wanashangilia.

Hata hivyo watawadanganya wale mamburula kweli kweli.
 
Nadhani neno kwamba Lissu ametumwa na mabeberu tusiwe tunalitumia saaana kwa sababu ni uwongo wa waziwazi ukisafiri katika maeneo kadhaa ndani ya nchi yetu utaona mabango mbalimbali yameandikwa barabarani hii imejengwa kwa msaada wa serikali ya Marekani.

Sasa mm najiuliza maswali hv aliyesimamia mpaka mabango haya ya mabeberu yakawekwa kwenye barabara zetu ni nani,hv kweli ni Tundu Lissu au ndio tabia ileile ya KUJIVUA AKILI MAKUSUDI au ndio ile tabia ya kujitekenya mwenyewe na kucheka mwenyewe.
 
Ndugu yangu, Lissu kuwa mtanzania haimzuii kuwa msaliti. Wasaliti ni hao hao wananchi. Hata katika ngazi ya familia, wasaliti wa mafanikio yako mara nyingi ni wanafamilia yako. Lissu alionesha madhaifu na usaliti makubwa pale alipoungana na mabeberu dhidi ya watanzania kwenye suala la madini.

Kuanzia hapo ameendeleza usaliti wa viwango vya juu kwa nchi yetu na amekuwa mtetezi wa mabeberu kwa kila jambo likiwemo na ushoga. Watanzania wanachuki sana naye kwa anayoyafanya. Ataona atakavyoadhibiwa kwenye kura. Vitisho vyake vya kuingiza watu barabarani pia havina maana. Hana watu wa kuingiza barabarani.

Asifikiri hao wachache wanaokuja kwenye mikutano yake anaweza kuwaingiza barabarani wamwage damu. Huwajui watanzania!! Alisema watu waandamane nchi nzima kupinga wagombea wao kuenguliwa, hakuna hata mmoja aliyefanya hivyo. Hana watu wa kuwaingiza barabarani. Labda barabara za kwenye facebook, tweeter na JF. Mwambieni aache vitisho, au akamuulize Mange.
 
Wewe ni MPUMBAVU, umeangalia video ya Robert Amsterdam YouTube aliyoitoa juzi anaitishia tume ya uchaguzi?.. najua mna mahaba na huyo KENGE wenu Lissu ila nakuhakikishia hawezi kuwa Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.. NEVER. Sio 2020 bali kamwe. Ni rahisi Steve Nyerere kuwa Waziri mkuu kuliko Tundu Lissu kuwa Raisi wa Tanzania. Bado siku 21 tu, Stay tuned.
Wewe unafaidika na ushenzi wa ccm acha watu walete mabadiliko ya umma tumbo lako litafuata baadaye.
 
Wewe ni MPUMBAVU, umeangalia video ya Robert Amsterdam YouTube aliyoitoa juzi anaitishia tume ya uchaguzi?.. najua mna mahaba na huyo KENGE wenu Lissu ila nakuhakikishia hawezi kuwa Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.. NEVER. Sio 2020 bali kamwe. Ni rahisi Steve Nyerere kuwa Waziri mkuu kuliko Tundu Lissu kuwa Raisi wa Tanzania. Bado siku 21 tu, Stay tuned.
Ww pimbi unapangia watanzania wooote?!
 
Nadhani neno kwamba Lissu ametumwa na mabeberu tusiwe tunalitumia saaana kwa sababu ni uwongo wa waziwazi ukisafiri katika maeneo kadhaa ndani ya nchi yetu utaona mabango mbalimbali yameandikwa barabarani hii imejengwa kwa msaada wa serikali ya Marekani.

Sasa mm najiuliza maswali hv aliyesimamia mpaka mabango haya ya mabeberu yakawekwa kwenye barabara zetu ni nani,hv kweli ni Tundu Lissu au ndio tabia ileile ya KUJIVUA AKILI MAKUSUDI au ndio ile tabia ya kujitekenya mwenyewe na kucheka mwenyewe.
Lissu ni kibaraka wa mabeberu, hakuna mtanzania mjinga anayeweza hatarisha Amani, rasilimali zetu kwa mabeberu. Wananchi wameshajua hiki Chama cha Mbowe ni utopolo mtupu, hakina ilani wala Sera. Mbeligiji huna chako Oct 28.
 
Kauli kwamba Lissu ametumwa ni uchochezi na NEC (Tume ya uchaguzi ya taifa) inatakiwa iwafungie wahusika kampeni zao kwa siku kumi na/au kufuta majina yao kwenye karatasi ya kura!
😎
👊 ✌️✌️✌️💥
 
Back
Top Bottom