Upungufu wa madini ya Iodine hupunguza akili kwa asilimia 10 - 15%: Takwimu za Jamii za Watanzania:

Upungufu wa madini ya Iodine hupunguza akili kwa asilimia 10 - 15%: Takwimu za Jamii za Watanzania:

Mgambilwa ni mntu

JF-Expert Member
Joined
May 30, 2017
Posts
2,869
Reaction score
3,187
Iodine ni madini yanayozalishwa baharini na kumwagwa nchi kavu ambako yanaingia chini kwenye miamba, hivyo upatikanaji wake unategemea zaidi aina ya udongo na vyakula vya baharini. Kutokana na mmomonyoko wa udongo, ardhi inazidi kuishiwa na madini hayo. Aidha, kadri unavyoingia ndani (interior) kutoka baharini na pia kadri unavyopanda mwinuko (altitude) ndivyo IDD inavyoongezeka.

Iodine
ni mojawapo ya madini muhimu kwa usitawi na ukuaji wa binadamu kwa kuwa ndiyo chakula lishe (micro-nutrients) pekee chenye athari kubwa katika maendeleo ya ubongo hasa katika hatua ya mimba (fetal brain development).
Duniani, watu bilioni moja wako kwenye risk ya kupata madhara kwenye ubongo kutokana na Iodine Deficiency Disorder (IDD) ambapo athari yake katika utambuzi (cognition) ndiyo chanzo kikuu cha utofauti wa ukuaji kati ya jamii na jamii.
Kiasili, 41% ya Watanzania in 1980s, sawa na watu milioni 10, waliishi maeneo yenye tatizo la IDD, ambalo 25% walikuwa na IDD huku 3% wakiwa na kiwango cha juu kabisa (severe). Aidha, Tanzania ni miongoni mwa nchi zilizokuwa na kiwango cha juu kabisa cha IDD duniani.
Katika baadhi ya maeneo ya Nyanda za Juu Kusini Total Goitre Prevalence (TGP) ilifikia 90% huku nusu ya watoto wakiwa na Tezi (hypothyroid). Maeneo hayo ni miongoni mwa Wilaya 27 zilizo-targetiwa kuanza kupewa iodised oil capsules. Wilaya hizo ni zifuatazo:

IMG_3394.PNG



IMG_1924.JPG


Soma baadhi ya maandiko yafuatayo:

In Raising the World’s I.Q., the Secret’s in the Salt

https://pdfs.semanticscholar.org/44...759.135366478.1525811663-689191352.1525811663
 
Hivyo kwa maeneo ya milimani, kabla ya kampeni ya dunia ya kutumia Iodated Salt (I-salt) kuanzia miaka ya 1980s, walikuwa wako disadvantaged kulinganisha na maeneo yasiyo ya milimani. Kwa leo hii tatizo hilo ni kama limeisha kwa maeneo mengi duniani kutokana na matumizi ya I-salt lakini jeni (genes) zetu bado zitaendelea ku-portray historia ya zamani kwa muda kidogo. Yaani, kwa kuwa mababu zako (Wahehe, Wabena, Wapangwa, Wakinga, Wawanji, Wasafwa, Wanyakyusa, Wandali, Wanyiha, Wamalila, Wamatengo, Walambya na Wafipa) hawakuwa na madini ya kutosha ya Iodine, athari kwenye jeni zake zitaendelea na zitakuwa zikipungua kidogo kidogo.
 
Kuna bandiko humu linaendelea likionyesha maeneo yaliyoathirika na madini ya Fluoride. Utaona kuwa, ni nadra kukuta maeneo yaliyoathirika na Iodine kuathirika pia na Fluoride. Ndiyo maana wakati centre ya Iodine ni Nyanda za Juu Kusini (Njombe), centre ya Fluoride ni ile ya Kaskazini (Arusha).
Kanda zote hizo zinaathirika kwa kiwango fulani kiakili kutokana na madhara ya madini hayo. Hata hivyo, unaweza kujiuliza kama madini hayo hasa Iodine, yanachangia kushuka akili, kwanini Kanda hizo mbili ndizo zinazoongoza kwa wasomi wengi hapa Tanzania (ukitoa Kanda ya Ziwa)?
Tufuatilie ajenda nyingine zitafuata soon.
 
Back
Top Bottom