Upungufu wa maji mijini ndio kelele zote hizi? Huu ndio ubinafsi wa hali ya juu

Upungufu wa maji mijini ndio kelele zote hizi? Huu ndio ubinafsi wa hali ya juu

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Wiki mbili mfululizo sasa kumekuwepo na kelele nyingi kila kona ya nchi kuhusu upungufu na mgao ya maji katika miji na majiji.

Katika maeneo ya vijijini sehemu nyingi za nchi maji limekuwa tatizo kubwa toka nchi hii inapata uhuru lakini hatujawahi kusikia kelele na mayowe kama wiki hizi mbili. Maji huko ni bidhaa adimu, ni aina fulani ya anasa. Wanawake, watoto kwa wanaume ni kawaida kabisa kutembea maili nyingi kufuata maji yasiyo safi wala salama kila siku wanayoishi chini ya jua.

Hizi kelele na yowe za wiki mbili zina tafsiri gani tofauti na ubinafsi mkuu kwa kuzingatia watu wengi wanaoishi mijini wametoka katika vijiji hivyo ila hawakuwahi kujihusisha na kupiga kelele kuchochea jitihada zozote za upatikanaji maji mpaka walipoguswa na kadhia hii?

Tanzania ni kubwa kuliko mtaa na kijiji chako, sote tunawajibika kuifanya nchi hii bora kwa kila mmoja anayeisha sasa na atakayekuja baadaye.
 
Thank you, thank you, hatimaye na sisi wa vijijini tumepata watu wa kutusemea. Mungu akubariki mkuu Yoda.

Sisi huku vijijini tunateseka sana na mahitaji ya maji, shule, barabara, zahanati nk, na hakuna anayetujali wala kutusikiliza. Kodi tunalipa wote, lakini maendeleo yote yanapelekwa mijini na majijini. Huo ni upendeleo na ubaguzi wa hali ya juu.

Ngoja na nyie watu wa mijini muonje machungu ya adha tunazoziishi kila siku huku vijijini, ili tunaposema kuwa tupatiwe hizo huduma labda mtatuelewa.
 
Viongozi wa CCM hawakai vijijini.

Wote wanakaa mijini.

Siku ukisikia pinda au Mangula amehamia kijijini Basi na ninyi mtamulikwa.
 
Thank you, thank you, hatimaye na sisi wa vijijini tumepata watu wa kutusemea. Mungu akubariki mkuu Yoda...
Kwa kuwa unajua kufurahia uovu ma uonevu wanaOfanyiwa wenye kutofautiana mawazo na nyie wanakijani, ni haki yenu wewe na wanavijiji wenye mawazo ma mitazamo kama yako, Hadi pale utakapo baini umuhimu wa uwepo was mawazo mbadala zaidi ya Yale ya wanakijani walioshindww kuwa saidieni miaka yote hiyo.
 
Hili Swala la maji Lema alishaliongea akiwa mbunge. Maji ni bidhaa inayouzika kirahisi kuliko air time. Kama makampuni ya simu yanapata faida kwa kuuza air time wekeni zabuni kwa kampuni binafsi ishuhulike na swala la maji.
Mawazo kama hayo hawataki wanayataka ya wanakijani wenzao hata kama ni mawazo ya hovyo.
 
Mawazo kama hayo hawataki wanayataka ya wanakijani wenzao hata kama ni mawazo ya hovyo.
Nchi nyingi zinavuna maji ya mvua karibu katika kila tarafa kuna water reservoir inayokusanya maji ya mvua kutoka barabara za lami. Maji haya yanatumika kwanza na maji ya mito yanakuwa secondary supply. Huwezi kutegemea maji ya mito 100%
 
Thank you, thank you, hatimaye na sisi wa vijijini tumepata watu wa kutusemea. Mungu akubariki mkuu Yoda.

Sisi huku vijijini tunateseka sana na mahitaji ya maji, shule, barabara, zahanati nk, na hakuna anayetujali wala kutusikiliza. Kodi tunalipa wote, lakini maendeleo yote yanapelekwa mijini na majijini. Huo ni upendeleo na ubaguzi wa hali ya juu.

Ngoja na nyie watu wa mijini muonje machungu ya adha tunazoziishi kila siku huku vijijini, ili tunaposema kuwa tupatiwe hizo huduma labda mtatuelewa.
Lazima uelewe kwamba anayelipa kikubwa ndiyo anayepewa huduma zaidi, huwezi kusema eti kodi mnalipa sawa..yaan walipa kodi wa wilaya kinondoni au ilala eti wapewe huduma sawa na walipa kodi wa wilaya ya kakonko au mbogwe, utakua unachekesha.
 
Maji kila mtu anatakiwa apate kadri anavyohitaji. Huwezi kufanya ubaguzi au kuweka madaraja kwenye huduma ya maji kwa sababu za ulipaji kodi.
Lazima uelewe kwamba anayelipa kikubwa ndiyo anayepewa huduma zaidi, huwezi kusema eti kodi mnalipa sawa..yaan walipa kodi wa wilaya kinondoni au ilala eti wapewe huduma sawa na walipa kodi wa wilaya ya kakonko au mbogwe, utakua unachekesha
 
Kwahiyo ulitaka wakae kimia kisa vijijin kuna shida, ndio vijijin Kuna shida kweli kweli, na mjini shida ndo hivyo, sasa nani anatakiwa kuwajibika, mwananchi au mkusanya kodi, kama ni mkusanya kodi ACHA kelele ziwafuate hukohuko waliko.

Mwanza tu ziwa liko pale ila miaka nenda ludi hapajawai kuwa na UTULIVU wa maji pale.
 
Hili Swala la maji Lema alishaliongea akiwa mbunge. Maji ni bidhaa inayouzika kirahisi kuliko air time. Kama makampuni ya simu yanapata faida kwa kuuza air time wekeni zabuni kwa kampuni binafsi ishuhulike na swala la maji.
Acha tu maji na umeme, serikali ndiyo imemonopoly soko lakini wababaishaji sana,tungekuwa na viongozi wenye maono,kubitia bills za maji na umeme tungejiendesha vizuri, viongozi wangehakikisha watu wanapata maji na umeme kwa 100% iwe mjini au vijijini na inawezekana maana pesa yake ni ndogo tu, tusingesimama kununua ndege kwanza tujikite kwenye kusambaza miundombinu ya maji na umeme nchi nzima.

Ndege sio priority maana ndege binafsi zipo.
 
Back
Top Bottom