Uraia wa nchi mbili: Serikali yasema haijui kama utaruhusiwa katika katiba mpya!

Uraia wa nchi mbili: Serikali yasema haijui kama utaruhusiwa katika katiba mpya!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Leo nimesoma jibu la Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Pereila Ame Silima kwa swali la Mbunge wa Mheza Helbert Mtangi, kuhusu suala la uraia wa nchi mbili, nikaishia kuisikitikia sana Tanzania juu ya viongozi tulio nao. Mtangi kauliza juu ya serikali kuwa na kigugumizi kuhusu suala la uraia wa nchi mbili, na badala yake Naibu Waziri kaweka kigugumizi kibaya hata zaidi pale alipojibu ifuatavyo;

"Jambo hilo kwa sasa bado ni gumu lakini akataka wabunge kusubiri mchakato wa katiba mpya kama utaliweka kwenye orodha ya mambo yanayopaswa kuangaliwa"


Kwa mantiki hii ni kwamba Naibu Waziri, kwa niaba ya serikali, anasema kwamba;


  • anaona utekelezaji wa uraia wa nchi mbili ni jambo gumu
  • hajui hata kama suala la uraia wa nchi mbili litaingizwa kwenye orodha ya mambo yanayopaswa kuangaliwa
  • hajui kama kama draft ya sasa ya katiba mpya inaongelea suala la uraia wa nchi mbili - ikimaanisha huenda hajui kwamba kuna hiyo draft ambayo tayari imeashatolewa rasmi na Tume ya Katiba

Nimejiuliza sana, kuwa na Waziri katika serikali anaeweza kusimama mbele ya Wabunge, na kuutangazia umma wa Watanzania jibu kama hili, kwa swali ambalo wala halikuwa la nyongeza lenye kuhitaji jibu la kutoka kichwani.

Hivi hii nchi yetu ina tatizo gani la uongozi, ni kwamba tumekosa kabisa viongozi makini hadi tunafanya nchi yetu kuwa kama kichwa cha mwendawazimu ambacho tunataka kumjaribia kila mtu kuwa kiongozi?
 
Haya ndio matokeo ya kuwa na serikali ya USWAHIBA; yaani serikali ya kishikaji inayoweza kupitisha budget ya tarakimu tu lakini haijui fedha kama itapatikana au la!!!!!!!
 
Mkuu, sitaki aseme uongo, bali kinachonisikitisha ni yeye kutojua!

Ujue kuwa idadi kubwa ya wanaCCM hasa mawaziri na wabunge hawajali maslahi ya taifa ilimradi tu wao wanaendelea kukamua.
 
Ujue kuwa idadi kubwa ya wanaCCM hasa mawaziri na wabunge hawajali maslahi ya taifa ilimradi tu wao wanaendelea kukamua.

Hewaa!!! Ndio maana Mkuu nasikitika sana kwamba tumefikia mahali tunafanya uongozi wa nchi yetu kuwa kichwa cha mwendawazimu.

Jibu la Naibu Waziri linaonyeha hajui hata nini kinachoendelea, au na hata wasaidizi wake ambao wanapaswa kumpa text ya jibu labda hakuwasiliana nao. Kwangu mie huo ni uzembe wa hali ya juu usiopaswa kuonyeshwa kwa kiongozi wa ngazi yake.
 
Hewaa!!! Ndio maana Mkuu nasikitika sana kwamba tumefikia mahali tunafanya uongozi wa nchi yetu kuwa kichwa cha mwendawazimu.

Jibu la Naibu Waziri linaonyeha hajui hata nini kinachoendelea, au na hata wasaidizi wake ambao wanapaswa kumpa text ya jibu labda hakuwasiliana nao. Kwangu mie huo ni uzembe wa hali ya juu usiopaswa kuonyeshwa kwa kiongozi wa ngazi yake.

Who cares.....in TZ kila muhuni,kibaka, mwizi,aliyepigika na maisha...,, anataka kua MBUNGE, kisha awe waziri
 
Back
Top Bottom