Urais bila majority bungeni una faida?

Urais bila majority bungeni una faida?

MwanaFalsafa1

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2008
Posts
5,565
Reaction score
843
Leo kuna mdau hapa JF kasema kitu ikanifanya nifikirie hili swala. Je ikatokea chama kimoja kika shika serikali na kingine kikawa na idadi kubwa zaidi ya wabunge ina faida? Mimi naona hapa yatatokea moja kati ya haya.

1. Kutakuwa na uwiano mzuri wa madaraka yani checks and balances. Kwa maana hiyo chama kinaacho shikiria serikali haiweza kufanya ndivyo sivyo ikijua wabunge wao wata pitisha tu agenda yoyote watakayo ipeleka bungeni. Kwa maana hiyo hapa itailazima serikali kupeleka hoja bungeni ambazo zinaonekana wazi ni kwa manufaa ya taifa ambalo bunge lenyewe ni lazima lipitishe.

2. Shughulu za serikali zitasimama na uendeshaji wa serikali utakuwa wa tabu zaidi. Kwa maana hiyo kunakuwa na deadlock. Hii itatokana kama chama chenye wabunge wengi zaidi kikiamua kususia hoja mbali mbali za serikali makusudi ili serikali ionekana imeshindwa kutimiza wajibu wake.

Swali langu ni je kama hali hii ikitokea Tanzania lipi kati ya haya mawili lina nafasi kubwa la kutokea? Kwa hali yetu ya kisiasa je itatokea sababu namba moja au itatokea sababu namba mbili? Je kuna uwezekano wa kutokea scenerio tofauti na hizi mbili? Ni scenerio ipi hiyo nyingine inayoweza kutokea?
 
....

Swali langu ni je kama hali hii ikitokea Tanzania lipi kati ya haya mawili lina nafasi kubwa la kutokea? Kwa hali yetu ya kisiasa je itatokea sababu namba moja au itatokea sababu namba mbili? Je kuna uwezekano wa kutokea scenerio tofauti na hizi mbili? Ni scenerio ipi hiyo nyingine inayoweza kutokea?


Hii unajua kuwa haiwezi kutokea labda kwa generation yako ya tatu. Amka, acha kuota ndoto za majinamizi mchana kweupe!
 
..Katiba yetu inaelekeza kwamba Waziri Mkuu atateuliwa miongoni mwa wabunge wa chama chenye majority bungeni.

..pia Raisi atateua baraza la mawaziri kwa kushauriana na Waziri Mkuu.

..kwa kifupi chama chenye majority bungeni ndiyo chenye madaraka ya kuunda serikali/baraza la mawaziri.

..i believe there will be more checks and balance in our country if the President does not belong to the party that has a majority in the parliament.
 
Hii unajua kuwa haiwezi kutokea labda kwa generation yako ya tatu. Amka, acha kuota ndoto za majinamizi mchana kweupe!

Mkuu unajua maana ya "what if"? Unajua maana ya hypothetical wuestion? Mimi nimeuliza kama if this was to happen je itakua bora ama la? Inaelekea lugha tabu. Anyway asant kwa your opinion?
 
..Katiba yetu inaelekeza kwamba Waziri Mkuu atateuliwa miongoni mwa wabunge wa chama chenye majority bungeni.

..pia Raisi atateua baraza la mawaziri kwa kushauriana na Waziri Mkuu.

..kwa kifupi chama chenye majority bungeni ndiyo chenye madaraka ya kuunda serikali/baraza la mawaziri.

..i believe there will be more checks and balance in our country if the President does not belong to the party that has a majority in the parliament.

O.K. mkuu nimekupata. Ila unajua kwamba nchi nyingi zingine zenye parliament system watu hawachagui mtu kuwa raisi. Wana chagua chama halafu chama chenye majority kinamchagua mtu wao kuwa raisi. Sasa Tanzania watu mnaenda kuchagua raisi then pia mna chagua wabunge. Which means kuna possibility wabunge wa chama fulani kuwa wengi zaidi ya wabunge wa chama cha raisi. In that case what happens? Ni katika kutaka kujua zaidi mkuu.
 
Mkuu unajua maana ya "what if"? Unajua maana ya hypothetical wuestion? Mimi nimeuliza kama if this was to happen je itakua bora ama la? Inaelekea lugha tabu. Anyway asant kwa your opinion?


Acha kuota ndoto za majinamizi!
hakuna kitu kama hicho labda karne ya 22 au 23.
 
Back
Top Bottom