Urinary Tract Infections ( UTIs) Imekuwa Janga

Kunawa maji ya ndoo yaliyokingwa vyooni. Inawezekana yana bacteria wengi
 

We jamaa uko vizuri sana

Ni kweli maabara za mtaani hasa hizi ambazo zipo attached na dispensary au private lab pekee zinagawa sana malaria na Uti ili wauze dawa.

Suluhisho la hili ni kwenda kupima hospitali kubwa ambayo naweza kusema kidogo ni complex unit.

Hapo juu nimeona kuna mtu anadai sex inaambukiza UTI kitaalam ni kwamba sio kweli sex haiambukizi UTI.

Usafi binafsi, usafi wa mazingira ni suluhisho la ugonjwa huu.

Kingine tuwe na utaratibu wa kufanya matibabu heavy tukigundulika kuwa na ugonjwa huu.fanya kipimo ukigundulika una UTI nenda mbele zaid kwa kufanya kipimo cha kuotesha wale wadudu kuwatambua na dawa itakayotumika kuwaangamiza(culture and sensitivity).

Kunywa maji mengi pia ni muhimu sana ili kuepuka ugonjwa huu. Kunywa maji ya kutosha na sio mpaka uhisi kiu no unaweza jiwekea utaratibu tu kwamba may be after masaa mawil nakunywa lita moja na ukihisi short call inakuita usijiulize nenda muda huo huo weka vitu jisafishe vizur.
 
Kunawa maji ya ndoo yaliyokingwa vyooni. Inawezekana yana bacteria wengi
Yes possibility ni kubwa kabisa ... angalizo hilo .... but nn kifanyike kwa changamoto hii Nena?
 
Kuchambaa kwa tissue pia ni uchafu. Maji ndo njia sahihi.
 
Hongera kwa kutoa angalizo na namna ya kutibu/ kukabiliana na UTI .... naamin wahusika watakuwa wamenufaika ...

By the way ile post ya sex kuwa source ya UTI nadhani mie nilimwelewa kuwa wahusika wanatumia njia zote 2 ... nyuma na mbele ... wajua utandawazi wawaua wengi mana sex aina hiyo iko mitandaoni .... wahusika waanza nyuma then wamalizia mbele .. ama waanza mbele then wamalizia na nyuma
 
Tulishafeli siku nyingi mtihani wa usafi maliwatoni labda turudi tukasome tena sayansikimu
Na kweli tushafeli mtihani mana sayansi kimu iligusa maisha yetu ya usafi ya kila siku .... mh. ndalichako chukua ubuyu huo
 

Sawasa mkuu nimekupata

Kitu kingine watanzania tujiepushe na hizi watu wanaita dawa mbadala na kuna matangazo kibao katika magazeti maredio na hata television.

Sikatai kama zinatibu hapana ila kumekuwa na wiz mkubwa na utapeli wa kutosha.

Kwa ushauri wangu tumia hizo dawa endapo tu utapata ushuhuda toka kwa mtu aliyeponywa na hizo dawa na si vinginenevyo otherwise tumia njia za hospitali Zilizothibitika kitaalam na kisayansi
 
urine culture nyingi walizo fanya wame isolate E. colli ila antibacteria parten nyingi zimeanza kuonyesha resiatance kuna stady ilifanyika muhimbili, ila genta bado inafanya kazi
nimeambulia kidogo ... but nmeachwa kizani sehem flan pia
 
Kwa wanaume wanywaji pombe na wanaoenda baa au kumbi za starehe watajizuia vipi na UTI ? maana unakuta vyoo vya kusimama mabomba hatatoi maji na ni lazima ukojoe maana umepiga masanga
 
Yes possibility ni kubwa kabisa ... angalizo hilo .... but nn kifanyike kwa changamoto hii Nena?
Elimu zaidi. Huyu bacteria E. coli anapatikana kwenye utumbo wa binadamu na wanyama wengine. Unapomwamisha huyu kutoka kwenye eneo lake ambapo hana madhara na kumpeleka kwengine, huko anakuwa adui. Njia za kumwamisha
1. kunawia maji ambayo tayari yana bacteria hao
2. Kunawa vibaya kutoka nyuma kwenye haja kubwa kwenda mbele kwenye uke
3. Watoto wadogo kukaa na chupi au pampers zenye kinyesi kwa muda mrefu.
4. Ku sex nyuma na mbele hata kama unatumia condom

Madhara ya uti za kujirudia ni kuharibu figo.

Mimi sio daktari na haya ni maoni ya layman
 
Imeshamiri sana kutokana na kuto kunywa maji mengi, kushea ndoo na kopo hasa kwa vyoo vyetu vya uswazi, pili wanawake wengine kupenda kujifucha kunako na kujisafisha ndani kwa sabuni zenye kemikali hii hufanya kuuwa bakteria wazuri wanaokinga na maradhi,
Na kutokana na umasikini tuliokuwa nao vyoo vya shimo ndio bomu kabisa kutokana na maumbile ya mwanamke alivyo na choo chenyewe kilivyo halafu aende achutame pale bahati mbaya choo kipumue ukiwa mule bakteria wasioonekana wanamwingia moja kwa moja kwenye maungio na wale wenye mzio sio kuwashwa huko ma dr wapo humu watatusaidia mengineyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…