Urusi imezikatia gesi nchi za Poland na Bulgaria. Putin alivyosema walipe kwa ruble hakuwa anatania

Putin ni bogus, hakuna popote ambapo mkataba unaongelea hayo madafu yake for the terms of payment, tayari wamemwambia akaye na gesi yake kuna sources nyingi.

Kuanzia mwakani atatembeza hiyo gesi kama karanga.
utadhani wewe ndo uliwasainisha hiyo mikata.[emoji23][emoji23],watu wakishiba makande na kuvimbiwa tabu kweli kweli!!
 
Nadhani kwa hii hatua ya kuwakatia gesi mataifa ya Magharibi watashutuka kidogo na kuanza kufikiria maamzi yao ya kutuma siraha Ukraine mara mbili mbili.
Maana tuseme hawakutegemea Kama Putin angechukua maamzi ya kuwakatia gesi.
Kama walikuwa wanapima upepo wa Putin nahisi Sasa wataanza kuelewa.
 
Waliokatiwa Gasi wananunua kiasi Kidogo Sana Cha Gasi ya URUSI na hawana athari Kiuchumi kwa URUSI. Mfano,Bulgaria inatumia $ 50M kwa Mwaka kununua Gasi kutoka Russia. Poland inatumia $ 190M kununua Gasi kutoka Urusi kwa Mwaka. Baba lao Ni Ujerumani. Ujerumani inatumia $ 420M kila siku kununua Gasi ya Urusi. Hiki Ni kiasi kikubwa kwa siku moja,Kwa Mwezi pekee Ujerumani anatumia $ 17B kununua Gas ya Urusi.

MARK MY WORDS

Siku Urusi akiikatia Gas Ujeremani,Basi Uchumi wa Ulaya yote na Urusi utaporomoka kuliko unavyofikilia. Urusi itapoteza 60% ya Mapato kwenye GDP ,Uchumi wa Ujerumani Utasambaratika na Ulaya yote.

Ndio maaana nasema,Urusi atakata Gasi kote Ulaya lakini sio Ujerumani,MARK MY WORDS.
 

Ni kweli mkataba wa Urusi unaisha oktoba mwaka huu. Lakini kuelekea mwishoni mwa march Putin alisema kuanzia tarehe 1 April, atakayetumia gesi ya Urusi itamlazimu kulipa kwa ruble, ambaye hakubali huo utaratibu mpya asichukue gesi. Poland akaamua kuendelea kuchukua gesi huuu mwezi wa nne, huku akiwa hataki kulipa kwa ruble, sasa huo ni wizi. Kimsingi bei haijabadilika na hata kama kama Poland hakuwa tayari kulipa moja kwa moja kwa kutumia ruble, bado angeweza kulipa kwa dola lakini kwa kufungua kwanza akaunti mbili hapo gazprombak. Akaunti moja ya dola/euro na akaunti nnyingine ya ruble. Halafu angeweka dola au ruble zake hapo. Kisha gazprombank ingezitumia kununua ruble na kumwekea hizo kwenye akaunti yake kisha kuzituma kwa gazprom ambayo ndiyo kampuni inayouza gesi. Sasa alichokikataa ndicho kwa sasa atalazimika kukifanya yaani kununua gesi ya urusi kwa kuitumia ujerumani ambayo iko tayari kulipa kwa ruble. Kwa hiyo euro za Poland ujerumani itazitumia kununua ruble ili ilipie gesi!! Sasa hapo poland amekwepa nini sana sana bei itaongezeka maana ujerumani itamwongezea cha juu kufidia gharama yake na faida juu. Beberu hatoi huduma bure! (There isa no free lunch in Europe). Ona EU wanachosema:

EU to boost Russian gas imports through countries willing to pay in rubles – media​

The EU seeks to make up for a gas supply shortfall in member states that refuse to comply with Russian ruble requirement

© Getty Images / DarioEgidi
The European Union plans to significantly increase the purchase of Russian natural gas through countries that are ready to pay for the commodity in rubles, TASS news agency reported on Wednesday citing a government source in Brussels.
 
Sasa wanamshtaki nani Na mali za Urusi walishazitaifisha mda tu?

Na Wamechukua Gesi ya Urusi toka nchi nyengine, Leo Putin amezionya hizo Nchi zinazotoa Gas yake.

Poland Hana ujanja asilimia 53 kama unavyosema si ndogo
 
Sisi wenyewe tumekatiwa huduma na azam tv, na tcra imekaa kimya. Mimi uwa nalipia azamu na channel yangu pendwa ni russia today. Channel namba 240. Azam wameiblock. Niliwapigia simu wanajiuma uma hawana majibu.
 
Mkuu Kuna nchi zinatolea udenda hio gas, wakitoa ulaya ipo China, India, Indonesia etc wanaitaka.

Gas ya Mrusi ni bei rahisi, mfano Gas ikitoka USA ni mara 3 bei yake.

Chukulia mfano hapaTz Lita ya petrol ni 2400 then aje Mtu akuuzie Lita 7200 utamuelewa? Hata kama hio ya 2400 inatoka Kwa adui utaigombania hio hio.

Na upo sahihi kuhusu Mjerumani maana Nchi lake kubwa sana, Bulgaria ni kama dar tu, wapo milioni 6.
 
Waeleze Tatizo wanaleta ushabiki
Unajiaibisha sana Mkuu na Heshima yako humu inashuka. Kiufupi Putin amewapiga chenga moja Kali sana hao wa magharibi.

Leo na Angalia Ruble imeshafika 74.62vs usd. Mwaka Jana muda kama Huu ilikua 74.73 so vikwazo vyooote hivyo wamejipiga wenyewe Ulaya, Uingereza, Spain Na nchi kibao wanaandamana maisha yamepanda, Hela za washirika zinashuka Thamani, Yen ilikua ikijulikana kama Most Stable Currency sasa hivi imekua utopolo tayari.

Biashara baina Ya China na Urusi imeongezeka 30% hivyo vitu vyote vizuri vya Mrusi vinaenda China, na Mrusi Ana Vitu ambavyo ni crucial kwenye Dunia ya Sasa hasa upande wa energy na semiconductor.

Viwanda vingi vinafungwa ulaya Sasa Hivi, Hakuna Energy na Material, mfano Mzuri Volkswagen, Hawa watu itabidi watoke Nje ya Ulaya wakamfaidishe China.

Kiufupi Mkuu the real Winner wa hii Vita ni China na Loser ni Ulaya. Hao Ulaya wamefanywa kama Kimada na USA ila wao ndio wanaangamia.
 
Hata yesu aliambiwa anajiaibisha ni seremala mzuri hivo ajikite kwenye Ufundi Lakin akaendelea kuwapa somo haha sitafti heshima ila nasema kinachopaswa kujulikana kwenu vijana


Britanicca
 
Punguza pumba hizi.
 
Hivi muda huu mnaopata ndugu zangu watanzania kuyachambua mataifa ya mbali tungetumia kuchambua matatizo ya nchi yetu na kupendekeza njia za kutatua matatizo hayo nadhan tungekuwa mbali Sana kiuchumi ndugu zangu wamarekan wa popobawa manzese na warusi wa buza kwa mama kibonge

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
I Feel your pain!
 
Na hio Gazprom ni ya urusi, unaishitaki vipi?
 
What's wrong to human brain? did stop functioning? If they impose sanction, what would they expected in response? To get things the way it used to be. They still black mailing the country through their sanction, now are they expecting to get their gas the same way they used to. It must be something is wrong.
 
Kwahiyo ata Russia anaweza kuwastaki ambao wamesitisha kununua gas kwao kwasababu siamini kama kulikuwa na kipengele kwamba ikitokea mmeanzisha vita au kuingilia Nchi flani tutaacha kununua gas?
elewa urusi alikuwa hauz direct kwa serikali ya poland bali anafanya biashara na kampuni ya kipoland so kampuni ndo inaishitaki urusi kwa kuvunja mkataba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…