Urusi inaripotiwa kuwaajiri mamluki wa Syria

Urusi inaripotiwa kuwaajiri mamluki wa Syria

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Urusi inawaajiri Wasyria wenye ujuzi katika mapigano ya mijini kupigana nchini Ukraine huku Moscow ikijiandaa kwa mapigano makali ya barabara hadi mtaa katika harakati zake za kuteka miji mikubwa ya Ukraine, maafisa wa Marekani wameliambia jarida la Wall Street Journal.

Maafisa wa kijasusi walikataa kueleza chapisho hilo ni wapiganaji wangapi wamekubali kujiunga na vita, lakini wakasema baadhi yao tayari wamesafiri hadi Urusi na wanajiandaa kutumwa Ukraine.

Kulingana na chapisho huko Deir Ezzor, Syria, Urusi imetoa wafanyakazi wa kujitolea kutoka nchi hiyo mishahara ya kati ya $200 na $300 "kwenda Ukraine na kufanya kazi kama walinzi" kwa miezi sita kwa wakati mmoja.

Maafisa huko Moscow wanasemekana kuamini kutumwa kwa wapiganaji waliopata uzoefu kwa zaidi ya muongo mmoja wa vita vya mijini katika Vita vya wenyewe kwa wenyewe vya Syria kunaweza kuongeza nguvu katika vita vyao vya kunyakua miji muhimu ya Ukraine, ikiwa ni pamoja na mji mkuu wa Kyiv.

Maveterani wa kijeshi wa Israel wameripotiwa kujitokeza kupigania Ukraine.
 
Angalieni mwanajeshi wa Ukrein na Zelenscky mwenyewe wwlivyotoa shit kwa marekani leo hahahahaha
 
Back
Top Bottom