Shadow7
JF-Expert Member
- Sep 28, 2020
- 24,606
- 39,289
Urusi imeyaelezea madai ya idara za upelelezi za Marekani kuwa Rais Vladimir Putin huenda alisimamia juhudi za kujaribu kumsaidia Donald Trump katika uchaguzi wa Marekani wa 2020 kuwa yasiyo na msingi.
Ripoti ya ujasusi ya Marekani iliyotolewa jana imeongeza maelezo mengine kwenye tuhuma kuwa baadhi ya maafisa waandamizi wa Trump walijaribu kushirikiana na Urusi kwa kusisitiza madai yaliyotolewa dhidi ya aliyekuwa wakati huo mgombea Joe Biden na viongozi wa Ukraine wenye mahusiano na Urusi kuelekea uchaguzi wa Novemba 3.
Ubalozi wa Urusi nchini Marekani umesema katika taarifa kuwa waraka uliotayarishwa na idara ya ujasusi ya Marekani ni tuhuma nyingine zisizo na msingi dhidi ya Urusi kwa kuingilia michakato ya kisiasa ya ndani ya Marekani.
Imesema hakuna maelezo na ushahidi uliotolewa kuthibitisha tuhuma hizo. Duru tatu zimesema kuwa Marekani inatarajiwa kuiwekea vikwazo Urusi katika siku chache zijazo kwa sababu ya tuhuma hizo.
Ripoti ya ujasusi ya Marekani iliyotolewa jana imeongeza maelezo mengine kwenye tuhuma kuwa baadhi ya maafisa waandamizi wa Trump walijaribu kushirikiana na Urusi kwa kusisitiza madai yaliyotolewa dhidi ya aliyekuwa wakati huo mgombea Joe Biden na viongozi wa Ukraine wenye mahusiano na Urusi kuelekea uchaguzi wa Novemba 3.
Ubalozi wa Urusi nchini Marekani umesema katika taarifa kuwa waraka uliotayarishwa na idara ya ujasusi ya Marekani ni tuhuma nyingine zisizo na msingi dhidi ya Urusi kwa kuingilia michakato ya kisiasa ya ndani ya Marekani.
Imesema hakuna maelezo na ushahidi uliotolewa kuthibitisha tuhuma hizo. Duru tatu zimesema kuwa Marekani inatarajiwa kuiwekea vikwazo Urusi katika siku chache zijazo kwa sababu ya tuhuma hizo.