Urusi yaongeza mapigo mazito huko Ukraine

Urusi yaongeza mapigo mazito huko Ukraine

HERY HERNHO

Senior Member
Joined
Mar 4, 2022
Posts
110
Reaction score
458
Mapigano katika mji wa Mashariki mwa Ukraine wa Bakhmut ambayo ni ngome muhimu, yanaongezeka na Rais Volodymyr Zelensky anasema hali huko inazidi kuwa mbaya.

Rais huyo anasema wanajeshi wa Urusi wanaharibu chochote ambacho Waukraine wanaweza kutumia kama ngao. Anasema wameendelea bila huruma, lakini majeshi yake hayajakata tamaa.

Wakati huo huo, Urusi inasema inakabiliwa na mashambulizi nchini mwao. Gavana wa eneo la Moscow alisema droni ilianguka katika mji wa Kolomna. Katika ujumbe uliotumwa kwenye mitandao ya kijamii, alidai kuwa miundombinu ya kiraia imekuwa ikilengwa.

Rais Vladimir Putin aliwaambia maafisa wa kiintelijensia jana Jumanne kwamba kumekuwa na idadi inayoongezeka ya matukio yanayohusu hujuma na ujasusi ndani ya Urusi. Ameitaka idara yake ya usalama kuchukua hatua zaidi


20230301_N01_1225551_L.jpg
 
Balaa nyingine kwa Urusi ni kuwa leo Bunge la Finland limepiga kura kwa kishindo kwa nchi hiyo kujiunga na NATO...diplomasia kwa Upande wa Urusi inahitajika sana siyo kutumia vitosho la sivyo atagombana na kila jirani.
 
Hiyo picha kwenye avatar yako, aliwai danganya bunge kuleta hati ya Muungano vp tayari alishaipeleka bungeni?
 
Ni kiburi cha Zelensky tu! Inasemekana US na NATO wamemshauri ayatoe majeshi yake kwenye mji huo! Na wakicheza siyo muda mrefu wanajeshi wa Russia wataunzingira mji huo kikamilifu.

Matokeo yake kilichotokea Moriopol city 2022 wakati kile kikosi hatari cha Ukraine Azov battalion kilivyojisalimisha ndivyo ambavyo itatokea katika mji huo!
 
Alidhani USA na NATO wataingiza majeshi kamili kama walivyofanya Kwa nchi nyingine,lkn safari hii wamekutana na kitu kizito.
 
Chapa chapa chapa murusi, MPAKA BEBERU AJIONE JOGOO.
 
Wacha wachapane uzuri Mimi ni mkulima kijijini
 
Mkuu kazi imekwisha tayari! Wagner wamemaliza kuuzunguka mji wote wameachia njia moja tu ya kuruhusu wanajeshi wa Ukraine kujitoa katika mji huo kwa hiari! Wamemtaka Zelensiky sasa awaambie waondoke kwa hiari.
 
Back
Top Bottom