USA wanatisha!

USA wanatisha!

Pape

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2008
Posts
5,487
Reaction score
83
USA wanatisha!:lying:
 

Attachments

  • USA (2).jpg
    USA (2).jpg
    35.6 KB · Views: 268
  • USA.jpg
    USA.jpg
    33.5 KB · Views: 211
  • USA (8).jpg
    USA (8).jpg
    25.7 KB · Views: 197
  • USA (6).jpg
    USA (6).jpg
    46.8 KB · Views: 185
  • USA (12).jpg
    USA (12).jpg
    46.6 KB · Views: 518
  • USA (9).jpg
    USA (9).jpg
    14.7 KB · Views: 175
  • USA (3).jpg
    USA (3).jpg
    12.5 KB · Views: 169
  • USA (7).jpg
    USA (7).jpg
    27.9 KB · Views: 177
  • USA (5).jpg
    USA (5).jpg
    27 KB · Views: 171
  • USA (1).jpg
    USA (1).jpg
    36.6 KB · Views: 152
  • USA (10).jpg
    USA (10).jpg
    47.7 KB · Views: 157
  • USA (4).jpg
    USA (4).jpg
    26.9 KB · Views: 171
  • USA (11).jpg
    USA (11).jpg
    44.7 KB · Views: 190
sasa kile cha kwetu kilichoangukia barabarani pale segera na kuua masikini mrubani wetu kinafanana na huo mtambo? Waacheni tu hawa watanue hatuwafikii hata kwa 0.001% wamebarikiwa hawa na Mungu
 
Sawa wanatisha lakini wameshindwa kuziba mafuta yanayoharibu fukwe zao huko Gulf of Mexico!!
 
Naona picha umezichanganya sana hadi kunakosekana mpangilio mzuri.

Kama sikosei kilichotokea hapo ni kuwa:

Ile Space plane ikiondoka Florida launching station, ikishapita kama sekunde tano tu, watu wanalijua hilo dude nje na ndani ndiyo huwa wanaanza kuliongoza yaani Houston. Ndiyo maana kumezuka msemo maarufu kuwa "Houston, we have problem".
Sasa hili dude likitoka huko MAJUU ya kikweli, huwa linarudi nyumbani kwako moja kwa moja yaani Houston. Hapo huwa wanaanza kazi ya kusafisha, kubadilisha vitofali vya chini ya tumbo lake, kuangalia kila chombo kama kiko kwenye good shape na kufanya matengenezo. Wakimaliza, basi huwa inakuja hiyo Jumbo Jet ya NASA yaani Boeng 747 na kubebeshwa hilo Dege baya (Space shuttle). Wanatake off pamoja na kutua Florida kwenye Station ya NASA. Wakilifikisha hapo, wanalipeleka kwenye jengo moja refu saaana. Hapo huwa wanakibeba na kukiunga kwenye matanki ya mafuta. Wakimaliza hapo laja likifaru moja (sijui hata niliige gari?) na wanaweka kila kitu juu yake na kubeleka kwenye launching Pad na kusubiri muda muafaka. Dakika kama tano kabla, ndiyo wanajaza MAFUTA kwenye tanki kubwa na kusubiri kulilipua. Wakilirusha tu, Houston wanaanza tena kulilinda dude lao na historia hujirudia.
Jamaa unaweza kuwachukia ila kwa hili na mengine mengi, huwa nawanyenyulia mikono. USA wakiamua, kushindwa huwa kazi.
STS-130_stack.jpg

Pamoja na kwamba tank ni kubwa sana, bado kuna space juu na wanakibeba kidude na kukishusha kwa Cranes na kinaungwa kwenye Tank.
spaceShuttleDM1602_468x686.jpg


Dude na tank lake likiwa juu ya Mgari wa ajabu. Sijui hilo gari lina Hourse Power kiasi gani. Lile jengo refu la NASA Florida ndiyo mpiga picha alipiga akiwa kwa ndani. Hili jengo lazima ni refu si kawaida.

YouTube - NASA's Space Shuttle Atlantis Arrives at Launch Pad for STS-129 Mission
 
Hakuna cha kujaliwa na Mungu hapa ni matokeo ya research iliyokwenda shule hayo. Sisi hata kutengeneza redio tumeshindwa, kazi ipo!
 
Hakuna cha kujaliwa na Mungu hapa ni matokeo ya research iliyokwenda shule hayo. Sisi hata kutengeneza redio tumeshindwa, kazi ipo!
mkuu redio jamaa wanatengeneza mtaani bana tusiwaonee,kuna siku nilikua ifakara vijijini baada ya kuvuka daraja kuelekea mahenge ndani ndani
kulikua na mechi ya mpira kuna jamaa alitengeneza mitambo na akawa anabrodcast live,lakini ni around pale kijijini tu ilikua inapatikana.
 
Naona picha umezichanganya sana hadi kunakosekana mpangilio mzuri.

Kama sikosei kilichotokea hapo ni kuwa:

Ile Space plane ikiondoka Florida launching station, ikishapita kama sekunde tano tu, watu wanalijua hilo dude nje na ndani ndiyo huwa wanaanza kuliongoza yaani Houston. Ndiyo maana kumezuka msemo maarufu kuwa "Houston, we have problem".
Sasa hili dude likitoka huko MAJUU ya kikweli, huwa linarudi nyumbani kwako moja kwa moja yaani Houston. Hapo huwa wanaanza kazi ya kusafisha, kubadilisha vitofali vya chini ya tumbo lake, kuangalia kila chombo kama kiko kwenye good shape na kufanya matengenezo. Wakimaliza, basi huwa inakuja hiyo Jumbo Jet ya NASA yaani Boeng 747 na kubebeshwa hilo Dege baya (Space shuttle). Wanatake off pamoja na kutua Florida kwenye Station ya NASA. Wakilifikisha hapo, wanalipeleka kwenye jengo moja refu saaana. Hapo huwa wanakibeba na kukiunga kwenye matanki ya mafuta. Wakimaliza hapo laja likifaru moja (sijui hata niliige gari?) na wanaweka kila kitu juu yake na kubeleka kwenye launching Pad na kusubiri muda muafaka. Dakika kama tano kabla, ndiyo wanajaza MAFUTA kwenye tanki kubwa na kusubiri kulilipua. Wakilirusha tu, Houston wanaanza tena kulilinda dude lao na historia hujirudia.

Mzee unapenda sana kuangalia science channel weye
 
attachment.php



Naona jamma wameimodified (streamlined) ile shuttle kwa nyuma kupunguza
drag wakati inasafirishwa na 747. Da watu wana apply fluid dynamics pale.
 
Chamoto,
Nashukuru kwa hilo maana nilikuwa sijaliona. Imebidi niangalie tena na kugundua kuwa si kuwa wamemodify yale matundu ya injini ya Shuttle. Kama sikosei kilichofanya ni kuweka mfuniko kwa nyuma na kuyafunga. Ila yamefungwa kiasi kwamba kwa nyuma yanatengeneza shape nzuri kwa ajili ya Aerodynamics nzuri kwa upepo na pressure ku-flow vizuri. Kwa lugha nzuri niseme kuwa wanaipa ile shape inayotakiwa kwenye COANDA EFFECT.
Hili dege linanifurahisha tu kwamba pamoja na ubaya wake, linafanya kazi kibao na uwezo mwingi sana. Kiboko yake ni kuwa lina vi injini vingi tu na vingine viko pembeni na mbele ya dude ambavyo huwa vinasaidia kujipindisha kama samaki majini, bila kutumia injini kubwa za nyuma. Na Kiboko yao ni vile vitofali chini ya tumbo lake ambavyo wakati jamaa wanarudi ardhini, huwa vinachemka hadi vinakuwa vya moto (air frictions). Siku kilibanduka, wakati wana take off, wakati wanarudi ikawa AJALI na wote wakafa. Sikuamini kuwa wanakichoma hadi kinafika temp. zaidi ya 1000 Celic. Na wakikitoa kwenye moto, wakakuwekea mkononi, ni cha baridi. Vinaloose joto in highets rates.

Ukiangalia hapa chini, utaona hizo HIPS zake bado zipo ila zimefunikwa tu na kama wanavyoonyesha hapa chini, wakifika Florida, wanaifyatua kutoka kwenye Boeng 747 na yenyewe inakwenda kutua peke yake uwanjani kwa kutumia gravitation force maana huwa halina mafuta wakati linatua. Jamaa kwa hili nawasifu. Warusi wao ni wakali saana kwenye Space Station. USA walijitahidi sana wajenge ya kwao na ikawashinda. Mwisho wakaamua tu kuungana na Warusi, Europe, Japan nk ili kujenga ya kimataifa na kazi akapewa Mrusi. Kilichowahangaisha USA na hadi leo hawafahamu ni jinsi ya kusafisha maji machafu na kuyatumia tena hapohapo Space station. Warusi waliweza na kujenga SS yao ya MIR ambayo ilikuja kurudishwa duniani na wakati inaanguka, ikaungua (walitaka iwe hivyo).
YouTube - Boeing 747(SCA) with the Space Shuttle

attachment.php



Naona jamma wameimodified (streamlined) ile shuttle kwa nyuma kupunguza
drag wakati inasafirishwa na 747. Da watu wana apply fluid dynamics pale.
 
sasa icho cha juu ni nini? hii ni ndege ya abiria, ni ndege la nini haswa, manake naona ingine iko juu ya mwenzie...hahaha.
 
wese kiasi gani linaingia kwenye tank hilo?
 
sasa icho cha juu ni nini? hii ni ndege ya abiria, ni ndege la nini haswa, manake naona ingine iko juu ya mwenzie...hahaha.
...Nadhani hako ka juu ndiko huwa wanakarusha kwenda huko anga za juu kabisa. Lakini inaonekana kama vile hakawezi kenyewe peke yake kusafiri kwenda huko Huston ni lazima kibebwe na huo mdege. Kwa kweli ni mambo mazito kabisa nadhani hawa watu wanatumia pesa ndefu kabisa kwenye research za mamo haya...dah!:A S-eek::A S-eek:
 
mkuu redio jamaa wanatengeneza mtaani bana tusiwaonee,kuna siku nilikua ifakara vijijini baada ya kuvuka daraja kuelekea mahenge ndani ndani
kulikua na mechi ya mpira kuna jamaa alitengeneza mitambo na akawa anabrodcast live,lakini ni around pale kijijini tu ilikua inapatikana.

Du jamaa mkali kweli. Sasa kwa nini asiieneze mpaka mitaa ya huku mahenge?
 
Hivi ile meli-anga Columbia iliunguaje?, taarifa zilizopo ni kwamba wamebakiza safari mbili tu kwa kutumia meli-anga Endevour na baada ya hapo watakuwa wanatumia facilities za Mrusi mpaka hapo watakapo kuwa na uwezo wa kuunda meli-anga mpya!
 
Chamoto,
Nashukuru kwa hilo maana nilikuwa sijaliona. Imebidi niangalie tena na kugundua kuwa si kuwa wamemodify yale matundu ya injini ya Shuttle. Kama sikosei kilichofanya ni kuweka mfuniko kwa nyuma na kuyafunga. Ila yamefungwa kiasi kwamba kwa nyuma yanatengeneza shape nzuri kwa ajili ya Aerodynamics nzuri kwa upepo na pressure ku-flow vizuri. Kwa lugha nzuri niseme kuwa wanaipa ile shape inayotakiwa kwenye COANDA EFFECT.

Ni kweli ule mfuniko umekuwa modified aerodynamically kwasababu
kama wasinge fanya hivyo yale mabomba yangeleta turbulence kwenye
rudder.

huwa vinachemka hadi vinakuwa vya moto (air frictions).

Mambo ya "atmospheric reentry speed" hayo

Sikuamini kuwa wanakichoma hadi kinafika temp. zaidi ya 1000 Celic. Na wakikitoa kwenye moto, wakakuwekea mkononi, ni cha baridi. Vinaloose joto in highets rates.

Mambo ya hi-tech alloy
Warusi waliweza na kujenga SS yao ya MIR

MIR ilikuwa kiboko wale jamaa waliweza kukaa kule hewani kwa miaka 15.
 
Lakini inaonekana kama vile hakawezi kenyewe peke yake kusafiri kwenda huko Huston ni lazima kibebwe na huo mdege.

Haka kadude ni kama ka glider kwahiyo hakawezi paa kama ndege ya kawaida.
Hata kama kataweza kupaa itabidi katumie mafuta mengi kwahiyou haiwi efficient
kwasababu hakako aerodynamic kama ndege za kawaida.
 
Diop,
Hicho kidege juu ndiyo Space Shuttle yenyewe ikibebwa kutoka Houston kwenda Florida.

Member uliyeuliza kisa cha Columbia kuanguka ni kwamba: Wakati wana take off, kitofali kimoja/vitofali (sikumbuki idadi) kilichomoka na kuanguka. Wakaenda angani salama na waligundua hilo ila wakaamini kuwa inatosha kabisa kurudi aridhini salama. Bahati mbaya waliamua vibaya na ile sehemu kitofali hakikuwepo, ilipata moto na ikasababisha Meli-anga kuungua.

Chamoto, hayo mawe siyo ALLOY. Wanayachimba Brazil na ni mawe kweli na wanayanyia kiufundi kidogo na kuyakata. Ni Natural na siyo mchanganyiko wa vyuma/hewa/chemical. Najua ingelikuwa hivyo basi si ajabu yangelikuwa yanatoka German maana huko kuna BOSCH na ndugu zake. Wanachezea Alloy wale na mtu hata uwe na Benz au BMW, utaona kitu kama chuma ila ukianza kutafuta ni nini, basi huoni ndani.
Space+Shuttle+Endeavour+Returns+Earth+9pSahRWO_2Zl.jpg


Tank la mafuta lina uzito kama tani 30 hivi na ujazo wake ni zaidi ya tani 700. Hapo wese ni Hydrogen na Oxygen pamoja maana juu hamna Oxygen na ili vitu viwake...... huyu hewa lazima awepo.
 
Chamoto, hayo mawe siyo ALLOY. Wanayachimba Brazil na ni mawe kweli na wanayanyia kiufundi kidogo na kuyakata. Ni Natural na siyo mchanganyiko wa vyuma/hewa/chemical. Najua ingelikuwa hivyo basi si ajabu yangelikuwa yanatoka German maana huko kuna BOSCH na ndugu zake. Wanachezea Alloy wale na mtu hata uwe na Benz au BMW, utaona kitu kama chuma ila ukianza kutafuta ni nini, basi huoni ndani.

Tank la mafuta lina uzito kama tani 30 hivi na ujazo wake ni zaidi ya tani 700. Hapo wese ni Hydrogen na Oxygen pamoja maana juu hamna Oxygen na ili vitu viwake...... huyu hewa lazima awepo.

Mzee mi nakuvulia kofia maana unavyo izimia hii kitu
utazani demu vile LOL...maana unaelezea mpaka na
mimi napa midadi.

Unajua kwa akina sisi tunaopenda mashine huwa
tunafurahi kujifunza jinsi inavyofanya kazi na kwanini
ilitengenezwa hivyo na wala si vinginevyo.

Mi sikujua kwamba hayo ni mawe asante kwa ku
niweka sawa.


Ila wacha bwana kama ulivyo sema hawa wajerumani
wana fanya vitu vya uhakika katika engineering.
 
Back
Top Bottom