Usajili wa kisiasa unaendelea kuigharimu Yanga

K2S7J3

JF-Expert Member
Joined
Apr 9, 2013
Posts
449
Reaction score
332
Sipendi sana kuongelea timu lakini kuna wakati nalazimika kufanya hivyo.

1. Usajili wa Kisinda na Morrison
Ni kigezo gani viongozi wa yanga walikitumia kuwarudisha hawa mabwana wawili huku wakijua kuwa haukuwa muda mwafaka kwa wao kurudi yanga? Binafsi naona kisinda hana mali tena na morrison ana mali lakini ana mentality kuwa yeye ni mkubwa kuliko yanga. Hivyo hawa hawana msaada kwa timu. SIASA

2. Usajili wa Wakongoman
Ukiangalia kikosi cha yanga kwa sasa utagundua kuna wachezaj zaidi ya watano walikuwa kikosi cha kwanza cha AS VITA iliyofungwa nje ndani na simba msimu ule simba ameongoza kundi. Kufungwa huko kulidhihirisha kuwa As vita haikuwa na wachezaji wa kushindana kimataifa, cha ajabu hao hao wakahamishiwa yanga ili waisaidie timu kimataifa. SIASA

3. Usajiri wa Stephane Aziz Ki
Simba walifanya makosa makubwa ya kutaka kumsajili Azizi ki eti kisa kawafunga kwenye hatua ya makundi. Azizi alishindwa kuivusha timu yake kwenda robo fainali. Wakati simba anahangaika ma Azizi, yanga waliruka nae juu kwa juu wakamchukua. Sawa azizi ki ni mchezaji bora wa ligi ya ivory cost msimu uliopita, kama ambapo hapa mtu fulan alikuwa mchezaj bora wa ligi yetu, lakini je, yanga walifanya vetting ya kujua mafanikio ya azizi kimataifa? SIASA

Ushauri
Timu zetu zinaposajili kwa ajili ya kimataifa zisajili watu wa kazi sio masupersta uchwara wakuja kula hela na kuruka ruka uwanjani.
 
Tumemsajili kisinda sababu amewapa Berkane kombe la shirikisho pia tumemsajili Morison sababu aliwapeleka Simba Robo fainali
 
Tumemsajili kisinda sababu amewapa Berkane kombe la shirikisho pia tumemsajili Morison sababu aliwapeleka Simba Robo fainali
Ipo hivi..Kisinda alisajiliwa kwasababu alimkimbiza Onyango, hukumbuki maneno yao hayo..?! ambapo ulipokwama usajili wake kwa muda kwisha wakaamua kuitupia lawama TFF, na Simba SC.

Kuhusu Morrison ni kuwa Kocha Nabi alivutiwa na performance yake ya Kimataifa akiwa Simba SC, kwahivyo alitamani uwezo ule auhamishie Yanga.
 
Morrison si alipiga faulo kwenye mechi ya derby akamfunga manula na kisinda si ndo alimkimbiza onyango akapata penalty iliyozaa goli na hao wa congo man si ndio wamesababisha unbeaten toka waje yanga hawajafungwa na simba wala team yoyote kwenye league kuu nchini we ulitaka mafanikio gani zaidi ya hayo.
 
Ukisoma vizur utagundua kuwa niliongea kwamba wale wakongo wa As vita walifungwa nje ndan na simba hivyo kimataifa hawajui namna ya kupambana

Kuhusu morrison nilisema ana mali lakini anajiona ni mkubwa kuliko club, nq hicho alikifanya pia simba ndio maana akapishana na barbara kipindi kile
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…