USAJILI WA WACHEZAJI EPL: TOA HUYU! INGIZA HUYU! AZAM FC YAACHA WA8!

Slim5

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2014
Posts
28,203
Reaction score
37,906
Nawasalimu sana wananzengo!

Tengua Teua kama kawaida!

Matajiri wa CHAMAZI wamewaacha wachezaji hawa baada kumaliza kandarasi zao:

Wazawa:

1. Ramadhani Singano
2. Danny Lyanga
3. Joseph Kimwaga
4. Mwasapili

Wageni:
5. Steven Kingue
6. Enock Atta
7. Tafadzwa Kutinyu
8. Chirwa
 
Selemeni "NODA" wa Mbeya City amesaini Azam Fc kwa kile kinasemwa Mwl mpya wa Azam kutoka KMC amempendekeza!

Kiungo Raphael Bryson na GK Benedict Haule wameongeza kandarasi zao Azam Fc.

Abubakar Salum "SURE BOY" yuko mbioni kuongeza mkataba wk Azam Fc! Hili limewaondoa ktk mbio TP Mazembe ambao awali walionyesha nia!

Bruce Kangwa nae amerefusha Kandarasi yake Chamazi!
 
Azam wana pesa lakini hawajui wanataka nini.
Nahisi hela ya tajiri inaenda bure. Amekosa watu sahihi was kuendesha mpira. Sasa Azam haina vision. Kila kocha anakuja na lake.
Kocha aambiwe vision ya Club. Akiweza aombe kazi kutekekeza vision husika. Hawezi, asepe!
 
Singano. Nahisi sasa atakuwa anaikumbuka Simba. Maana Simba walikuwa wanampenda akaleta Kiburi.
Hata siku moja usilete kiburi na mwajiri wako wa zamani.
Mungu awabariki
Tangu aondoke simba, hajawahi kusikika tena
 
Kumradhi: Heading isomeke TPL badala ya EPL! @Mods please
 
Duh!! Mzee mwenzangu, azam fc tena ndani ya EPL..

Hahaa!! Najua umepitiwa, kukosea ndio sifa ya wanadamu.
 
Singano. Nahisi sasa atakuwa anaikumbuka Simba. Maana Simba walikuwa wanampenda akaleta Kiburi.
Hata siku moja usilete kiburi na mwajiri wako wa zamani.
Mungu awabariki

Singano angekuja Yanga huwa namhurumia sana huyu dogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…